Skip to main content

Posts

BARABARA OLE-KENGJA BAADA YA MIAKA MINNE SASA YAWEKEWA ALAMA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MADEREVA na wananchi wanaotumia barabara ya Ole-Kengeja, iliyofunguliwa mwaka 2020 na aliyekuwa Rais wa Zanzibar na Dk. Ali Mohamed Shein, wamefurahia baada ya zoezi la uwekaji wa alama za barabarani kuanza . Walisema awali, barabara hiyo iliyofunguliwa miaka minne sasa, haikuwa na alama za barabarani, jambo ambalo lilikuwa likiwapa ukakasi, wanapokuwa barabarani. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema kwa sasa wamefurahishwa na uamuzi wa serikali wa awamu ya nane, chini ya Rais Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuitaka wizara husika, kuiwekea alama barabara hiyo. Walisema kuwa, kukosekana kwa alama za barabarani, kulikuwa kunatishia maisha yao na watembea kwa miguu, kutokana na kukosekana la alama hizo muhimu. Mmoja kati ya madereva hao, Mohamed Khamis Hasnuu alisema, walikuwa wakipata shida hasa kwa wao wageni wa barabara hiyo, jambo ambalo lingeweza kusababisha ajali. ‘’Hujui wapi kuna skuli, soko, hospitali, mpindo na muunganiko ...

WAZIRI MKUCHIKA AVUTIWA NA PBZ, KUWASAIDIA WAKULIMA LINDI, MTWARA

  Na Mwandishi wetu, Lindi@@@@ WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Raisi, Ikulu (kazi maalum) Kapten George Huruma Mkuchika amevutiwa na huduma zinazotolewa na Benki ya watu wa Zanzibar tawi la Mtwara ambapo ameipongeza benki hiyo.  Akizungumza alipotembelea banda la maonyesho ya nanenane kanda ya kusini yanayofanyika katika viwanja vya ngongo mkoani Lindi amesema kuwa ni benki yenye gharama nafuu.  Amesema kuwa unafuu huo umekuwa ukiwasaidia wakulima kupata malipo yao ya korosho na ufuta kwa wakati.  Akizungumza mbele ya  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Raisi, Ikulu (kazi maalum) Kapten George Huruma Mkuchika,  kwenye Maonyesho ya Nane Nane yanayofanyika katika viwanja vya ngongo kwenye Mkoa wa Lindi Mwakilishi wa Benki hiyo katika maonyesho hayo Nassoro  Mohamed Zaid  amesema kuwa huduma hizo zitawezesha wakulima kuhudumiwa popote walipo.  Amesema kuwa uwepo wao katika maonyesho hayo ni kuhamasisha wakulima na wafugaji kuweza kutumia benki hiyo ambayo imewez...

TAMWA -ZANZIBAR INGALI MACHO HADI IPATIKANE SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHERIA iliyodumu miaka 36 sasa inatajwa kutokuwa rafiiki na uhuru wa habari, ni ile nambari 5 ya mwaka 1988 ya Magazeti, Vitabu na Mawakala wa Habari Zanzibar. Ni miaka 36 sasa, sheria hii inaendelea kutumika Zanzibar, na kutajwa kuathiri na kutishia utendaji kazi wawaandishi wa habari na vyombo vyao hapa visiwani. Maana wadau na waandishi wa habari, wanakubali kuwa, upatikanaji, usambaaji wa habari ni haki ya kikatiba. Kwa Katiba ya Zanzibar yam waka 1984, kwenye kifungu cha 18, kimebainisha hilo sambamba na ile ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania yam waka 1977, kwenye Ibara kama hiyo nayo, imewekwa. HISTORIA YA UPATIKANAJI SHERIA MPYA ZANZIBAR Sheria hiyo tokea mwaka 2010, ilianziwa harakati za kutaka kufutwa, kwa wadau wa habari kujikusanya pamoja, ili sasa iwe na sheria moya ya habari. Kwa wakati huo, tasisi za Baraza la Habari Tanzania ‘MCT’ –ofisi ya Zanzibar, vyama vya waandishi wa habari, taasisi za haki za binadamu na wizara h...

WIKI YA MWANANCHI, MAMBO NI MOTOOO....MASHABIKI BAGAMOYO WATOA MSAADA WA MADAWATI

  Na Mwandishi Wetu@@@@ Kuelekea wiki ya Mwananchi, Mashariki wa klabu ya Yanga wa Kijiji cha Buma kilichopo Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani,  wamejitokeza kutoa misaada mbalimbali ya kijamii ikiwamo madawati. Mashabiki hao walikabidhi madawati hayo katika  shule ya Msingi Buma iliyopo kijijini hapo ikiwa ni mwendelezo wa kutoa misaada kwa jamii kuelekea siku ya Mwananchi inayotarajiwa kufanyika Agosti 4 Mwaka huu katika Uwanja wa Benjamin Mkapa maarufu 'Lupaso'. Akizungumza katika makabidhiano hayo, Mwenyekiti wa Klabu hiyo Tawi la Buma Ismail Omary amesema kuwa, wanachama  wamekua na utaratibu wa kutoa misaada mbalimbali kwa jamii, lengo ni kurudisha hisani kwa wananchi wanaowazunguka kutokana na mwendelezo mzuri wa timu yao. " Leo tumejitokeza kwenye viwanja vya shule ya msingi Buma lengo ni kutoa msaada wa madawati ili wanafunzi waweze kuyatumia wakati wa masomo, huu ni utaratibu wetu wa kurudisha fadhira kwa wananchi kutokana na  hamasa tunqzozipata za tim...

'MAREKEBISHO KANUNI ZA MAADILI VYAMA VYA SIASA KUJALI USAWA WA KIJINSIA'

  ZANZIBAR                                                                                             Naibu Msajili wa vyama vya siasa Mohammed Ali Ahmed amesema sheria na kanuni za maadili ya vyama vya siasa zinaendelea   kufanyiwa marekebisho kwa lengo la kuweka usawa wa kijinsia pamoja na kukuza uwajibikaji na kuzuia unyanyasaji dhidi ya wanawake ili waweza kushiriki kikamilifu katika siasa na   demokrasia nchini. Akizungumza kwa niaba ya Naibu Msajili wa vyama vya siasa, Afisa sheria Mwandamizi kutoka ofisi hiyo Abdulrazak Ali kwenye mkutano wa tathmini iliyoangalia vikwazo vinavyowakwaza wanawake katika kugombea na kushiriki masuala ya kisiasa   uliofanyika   ukumbi wa ZURA Maisara mjini Unguja, ambao uliowashirikisha wadau mb...

BONANZA LA MAZOEZI PEMBA: MAKAMU WA KWANZA ATOA RAI KUNDOA DHANA POTOFU MICHEZONI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Massoud Othman, amevishauri vilabu ya mazoezi nchini, kujitengenezea kanuni, zitakazowavutia watu wingi zaidi kujiunga kwenye mazoezi, ili kuondoa dhama potofu ya mazoezi ni uhuni. Alisema, kama kundi kubwa la watu wanadhana kuwa mazoezi ni uhuni na kuvunja maadili, ni wakati sasa kwa vilabu vya mazoezi na michezo, kuwa na kanuni zitakazofuta dhana hiyo. Makamu huyo wa Kwanza, aliyasema hayo leo Julai 28, 2024 uwanja wa michezo Gombani Chake chake, kwenye bonanza la miaka 10, tokea kuanzishwa kwa ‘Gombani Fitness Club’ lilioandaliwa kwa pamoja na TAMWA-Zanzibar na Shirika la Bima. Alieleza kuwa, kwa vile mozoezi ni jambo muhimu kwa kila mmoja, ni vyema kuwepo na kanuni ndogo ndogo, ambazo zitawavutia wengine, kushiriki katika kupata kinga ya miili yao. Alifahamisha kuwa, ni kweli kama kuna viashiria vya uvunjifu wa maadili, inaweza kuwa sababu kwa baadhi ya watu, kuona sio sehemu salama, ingawa ...