Skip to main content

BARABARA OLE-KENGJA BAADA YA MIAKA MINNE SASA YAWEKEWA ALAMA

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MADEREVA na wananchi wanaotumia barabara ya Ole-Kengeja, iliyofunguliwa mwaka 2020 na aliyekuwa Rais wa Zanzibar na Dk. Ali Mohamed Shein, wamefurahia baada ya zoezi la uwekaji wa alama za barabarani kuanza.

Walisema awali, barabara hiyo iliyofunguliwa miaka minne sasa, haikuwa na alama za barabarani, jambo ambalo lilikuwa likiwapa ukakasi, wanapokuwa barabarani.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema kwa sasa wamefurahishwa na uamuzi wa serikali wa awamu ya nane, chini ya Rais Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuitaka wizara husika, kuiwekea alama barabara hiyo.

Walisema kuwa, kukosekana kwa alama za barabarani, kulikuwa kunatishia maisha yao na watembea kwa miguu, kutokana na kukosekana la alama hizo muhimu.

Mmoja kati ya madereva hao, Mohamed Khamis Hasnuu alisema, walikuwa wakipata shida hasa kwa wao wageni wa barabara hiyo, jambo ambalo lingeweza kusababisha ajali.

‘’Hujui wapi kuna skuli, soko, hospitali, mpindo na muunganiko wa barabara moja na nyingine, maana alama ndio hasa mwelekeo wa barabara,’’alisema.

Nae dereva Abdalla Mohamed Othman, alisema walikuwa wakipata tabu, wakati wanapokua kazini, jambo ambalo likuwa hawaliwapi raha ya kazi yao.

‘’Kama barabara haina alama za barabarani, inakuwa kama vile jangwa, hujui wapi kuna daraja kubwa, ndogo, mpindo, skuli jambo ambalo, linaweza kuchangia ajali zinazoepukika,’’alifafanua.

Muendesha piki piki ‘boda boda’ eneo la Kenya- Chambani Mohamed Omar Hassan, alisema alishapata ajali mara mbili, wakati anaaza kuitumia barabara hiyo.

‘’Nilipofika eneo la kwa mlima kwa Mtora, kumbe mbele kuna njia ya kuingia skuli ya Ukutini, sasa kuna wanafunzi wanafukazana, nilibidi niingie msingi kwa kuwakwepa,’’alifafanua.

Alieleza kuwa, alikuwa haoni alama yoyote ya barabara hiyo mpya, jambo ambalo linaweza kupoteza mwelekeo, hasa kwa madereva wapya wa matumizi ya barabara hiyo.

Abiria Asia Mwalimu Mohamed na mwenzake Maryam Muhene Issa wa Chambani, walisema wanategemea baada ya zoezi la uwekaji wa alama za barabara, ni madereva kuziheshimu.

Walisema kutokana na matumizi mabaya ya bara bara, hasa kwa gari za abiria na waendesha boda boda, hawatarajii alama hizo kusaidia.

‘’Kazi ya kuziweka alama za bara barani ni jambo jema kwetu, lakini hatua ya pili ni kwa madereva hao kuziheshimu alama hizo,’’walisisitiza.

Mapema Afisa Mdhamini wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Pemba Ibrahim Saleh Juma, alisema kazi hiyo inafanya na kampuni ya M/S. Engineer Grade Sign LDT, kutoka Tanzania bara.

Alieleza tu, kampuni imepewa kazi hiyo kwa miezi sita, kwa barabara za Unguja na Pemba, ambapo pia inahusika na uwekaji wa matengenezo ya pembezoni mwa barabara ili idumu zaidi.

Alisema, serikali ya awamu ya nane, imeona bora kuiwekea alama barabara hiyo, ili kuepusha ajali zisizokuwa za lazima, hasa pale madereva wanapoamua kuzifuata.

‘’Uhai na ustaarabu wa barabara ni kuwepo kwa alama za barabarani, ambazo hizi huwasaidia madereva kujua daraja lipo wapi, mlima upo kilomita ngapi, soko, skuli, hospitali ili kupunguza mwendo na kwenda kwa tahadhari,’’alisema.

Hata hivyo, Afisa Mdhamini huyo, ameendelea kuwanasihi wananchi, kutosogelea hifadhi ya bara bara wakati wanapoendesha ujenzi wa nyumba za makaazi, biashara au nyumba za ibada.

Bara bara hiyo yenye urefu wa kilomitya 35, ndio barabara refu kwa Zanzibar, imepitia wilaya za Chake Chake na Mkoani na shehia 15, ikiwemo Ole, Vitongoji, Mfikiwa, Ukutini, Chambani, Kendwa na Kengeja.

Bara bara hiyo ina upana wa mita 7.5 na imejengwa kwa kiwango cha lami ya moto, ina uwezo wa kutumiwa na gari zenye uzito wa tani 10, inayo madaraja 16 na culvert ndogo ndogo 118, pamoja na miundombinu ya kupitishia huduma za kijamii ikiwemo mabomba ya maji.

Gharama za ujenzi huo ulifanywa kupitia mkopo wa Benki ya wanachama wa nchi zinazotoa mafuata kwa wingi duniani (OFID), ikishirikiana na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ambapo hadi kukamilika kwake imegharimu shilingi bilioni 30.935, kati ya hizo mkopo kutoka OFID, ni shilingi bilioni 24.2 na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imechangia shilingi bilioni 6.735.

                             Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan