Skip to main content

THBUB YAWAPA DARSA YA HAKI ZA BINAADAMU WANAFUNZI 454 WA SEKONDARI 'ZENJ'

 


NA MWANDISHI MAALUM, UNGUJA

Maofisa kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ofisi ya Zanzibar, wamewapa elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora Wanafunzi 454 wa Skuli za sekondari kwa Mikoa mitatu ya Unguja.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti kupitia Serikali za wanafunzi wa Skuli 11 za mikoa hiyo, Maofisa hao waligusia zaidi katika mada za kukuza, kulinda, kuheshimu, na kuhifadhi haki za wengine.

Pia maofisa hao waliwaeleza wanafunzi kwa upana kuhusu THBUB, kazi na majukumu yake katika kulinda haki za binadamu sambamba na wajibu wa wanafunzi hao katika kuzitekeleza na kuziishi haki hizo.

Akiizungumzia haki ya msingi ya mwanadamu, haki ya kuisha Ofisa Sheria THBUB, Fatma Sultan Mwesimba aliwaeleza wanafunzi hao kwa haki hiyo inaaza mara moja baada ya binadamu kuzaliwa nakuongeza kuwa haki hiyo haipokonyeki ina inapaswa mtu kuendelea kuishi nayo na haipaswi kuvunjwa kwa namna yoyote ile isipokua iamuliwe kupitia sharia za nchi. Pia aliongeza kwa Tanzania hakuna sharia iliyotekeleza haki hiyo kuvunjwa lisha ya kuwa      

Aidha, Maofisa hao pia walifanikiwa kufungua klabu za haki za binadamu (Haki Klabu) kwa skuli 11 kati ya walizozitembelea na kuwateua walimu watakaokuwa walezi watakaozisimamia na kuziendesha klabu hizo.



Naye, Ofisa kutoka Idara ya Elimu Sekondari, eneo la huduma za wanafunzi Mwl. Suhuba Daudi Issa aliwasihi wanafunzi hao kutekeleza kwa vitendo wajibu wao wa kusoma kwabidii kwa kuifanyia kazi haki yao ya msinagi ya kupatiwa elimu bora.

Pia, aliwaeleza wanafunzi hao kutumia wajibu wao wa kulinda na kuzihifadhi kwa kusimamia vizuri rasilimali za skuli zao na wajibu wao wa kutii na kuziishi kanuni na taratibu za skuli zao pamoja na kuheshimu walimu wao na jamii wanazoishi.

Skuli zilizofikiwa na timu ya maofisa kutoka THBUB ni pamoja na Skuli za Sekondari Kinyasini, Kilombero, kutoka Wilaya ya Kaskazi B na, Sekondari ya Mkokotoni na Mkwajuni kutoka Wilaya ya Kaskazi A, Unguja.



Skuli nyengine ni Sekondari za Faraja na Muungano kutoka Wilaya ya Mjini, Skuli ya Sekondari Mbuzini iliopo Wilaya ya Magharibi A, Sekondari ya Aboud Jumbe Mwinyi na Maungani zote kutoka Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Magharibi.

Pia, THBUB ilifika Mkoa wa Kusini Unguja kwa kuzitembelea skuli za Sekondari za Makunduchi na Dimbani ziliopo Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja.

Skuli hizo zilizofikiwa na THBUB kwa lengo la kupatiwa elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora sambamba na kufunguliwa haki klabu, jumla ya klabu 11 zilifunguliwa katika Skuli hizo.





Zoezi la ufunguzi wa Klabu hizo lilianza tarehe 18 Mei, 2026 na linatarajiwa kukamilika tarehe 05 Juni, 2026 kwa kufunguliwa klabu nyengine 19 na kufanya idadi ya klabu 30 zilizopangwa kufunguliwa kwa Mikoa mitatu ya Unguja ikiwemo Mkoa wa Mjini Magharibi, Kusini na Kaskazini Unguja kwa kuwajengea wanafunzi utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu na misingi ya utawala bora.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...