NA MWANDISHI MAALUM, UNGUJA
Maofisa kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
(THBUB) ofisi ya Zanzibar, wamewapa elimu ya haki za binadamu na misingi ya
utawala bora Wanafunzi 454 wa Skuli za sekondari kwa Mikoa mitatu ya Unguja.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kupitia Serikali za
wanafunzi wa Skuli 11 za mikoa hiyo, Maofisa hao waligusia zaidi katika mada za
kukuza, kulinda, kuheshimu, na kuhifadhi haki za wengine.
Pia maofisa hao waliwaeleza wanafunzi kwa upana kuhusu THBUB,
kazi na majukumu yake katika kulinda haki za binadamu sambamba na wajibu wa
wanafunzi hao katika kuzitekeleza na kuziishi haki hizo.
Akiizungumzia haki ya msingi ya mwanadamu, haki ya kuisha
Ofisa Sheria THBUB, Fatma Sultan Mwesimba aliwaeleza wanafunzi hao kwa haki
hiyo inaaza mara moja baada ya binadamu kuzaliwa nakuongeza kuwa haki hiyo
haipokonyeki ina inapaswa mtu kuendelea kuishi nayo na haipaswi kuvunjwa kwa
namna yoyote ile isipokua iamuliwe kupitia sharia za nchi. Pia aliongeza kwa
Tanzania hakuna sharia iliyotekeleza haki hiyo kuvunjwa lisha ya kuwa
Aidha, Maofisa hao pia walifanikiwa kufungua klabu za haki za
binadamu (Haki Klabu) kwa skuli 11 kati ya walizozitembelea na kuwateua walimu
watakaokuwa walezi watakaozisimamia na kuziendesha klabu hizo.
Naye, Ofisa kutoka Idara ya Elimu Sekondari, eneo la huduma
za wanafunzi Mwl. Suhuba Daudi Issa aliwasihi wanafunzi hao kutekeleza kwa vitendo
wajibu wao wa kusoma kwabidii kwa kuifanyia kazi haki yao ya msinagi ya
kupatiwa elimu bora.
Pia, aliwaeleza wanafunzi hao kutumia wajibu wao wa kulinda
na kuzihifadhi kwa kusimamia vizuri rasilimali za skuli zao na wajibu wao wa
kutii na kuziishi kanuni na taratibu za skuli zao pamoja na kuheshimu walimu
wao na jamii wanazoishi.
Skuli zilizofikiwa na timu ya maofisa kutoka THBUB ni pamoja
na Skuli za Sekondari Kinyasini, Kilombero, kutoka Wilaya ya Kaskazi B na, Sekondari
ya Mkokotoni na Mkwajuni kutoka Wilaya ya Kaskazi A, Unguja.
Skuli nyengine ni Sekondari za Faraja na Muungano kutoka
Wilaya ya Mjini, Skuli ya Sekondari Mbuzini iliopo Wilaya ya Magharibi A,
Sekondari ya Aboud Jumbe Mwinyi na Maungani zote kutoka Wilaya ya Magharibi B
Mkoa wa Mjini Magharibi.
Pia, THBUB ilifika Mkoa wa Kusini Unguja kwa kuzitembelea
skuli za Sekondari za Makunduchi na Dimbani ziliopo Wilaya ya Kusini, Mkoa wa
Kusini Unguja.
Skuli hizo zilizofikiwa na THBUB kwa lengo la kupatiwa elimu
ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora sambamba na kufunguliwa haki
klabu, jumla ya klabu 11 zilifunguliwa katika Skuli hizo.
Zoezi la ufunguzi wa Klabu hizo lilianza tarehe 18 Mei, 2026
na linatarajiwa kukamilika tarehe 05 Juni, 2026 kwa kufunguliwa klabu nyengine
19 na kufanya idadi ya klabu 30 zilizopangwa kufunguliwa kwa Mikoa mitatu ya
Unguja ikiwemo Mkoa wa Mjini Magharibi, Kusini na Kaskazini Unguja kwa
kuwajengea wanafunzi utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu na misingi ya
utawala bora.
Comments
Post a Comment