Skip to main content

KAMATI YA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI CHAKECHAKE YAWAJIA JUU WAZAZI WANAOWARUHUSU WATOTO KUTEMBEZA BIASHARA

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KAMATI ya kupambana na udhalilishaji kwa wanawake na watoto ya wilaya ya Chake chake, imepiga marufuku kwa wazazi na walezi wilayani humo, kuwapa biashara za kutembeza watoto wao, kwani ni njia moja wapo ya kufanyiwa vitendo viovu.

Kauli hiyo imetolewa leo Mei 25, 2026 na Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Kassim Ali Omar, wakati akifungua kikao kazi, cha wajumbe hao, kilichofanyika ukumbi wa zamani wa TASAF Chake chake.

Alisema lazima kamati, isimamie hilo maana wapo wazazi wamekuwa wakiwatumia watoto wao, kutembeza biashara mitaani, na kisha huishia kudhalilishwa.

Alieleza kuwa, hasa kuelekea kipindi hichi cha sikukuu na skuli kufungwa, wazazi hutumia fursa hiyo, jambo ambalo sio sahihi.

‘’Niitake sana kamati hii, ihakikishe inasimamia sana, maana wapo wazazi na walezi, wamekuwa wakiwatumia watoto wao, kutembeza biashara majumbani, jambo ambalo ni hatari kwao,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Kaimu Mwenyekiti huyo Kassim Ali Omar, alisema bado vitendo vya ukatili na udhalilishaji vya wanawake na watoto, wanaendelea kupata maumivu ya janga hili.

‘’Sijajua kuwa, kuongezeka kwa matendo hayo ni jamii kupata elimu, au vitendo vimezidi, hili ni jukumu la kamati, kuendelea kutoa elimu,’’alifafanua.



Aidha, aliwapongeza wajumbe wa kamati hiyo, kwa kazi wanayoifanya ya kutoa elimu, katika maeneo kadhaa ya wilaya ya Chake chake.

Mapema Katibu wa kamati hiyo Rashid Said Nassor, alisema vyombo vya habari, vimekuwa na mchango mkubwa, katika mapambano dhidi ya udhalilishaji.


Akiwasilisha mpango wa kazi wa miezi mitatu iliyopita, Mjumbe wa kamati hiyo Hussna Haji Othman, alisema walizifikia skuli za Ndagoni, Pujini, Chanjaani na Wesha kuwapa elimu, ya kupinga udhalilishaji.

‘’Na sisi kamati ya wilaya, tuliwafikia wananchi wa shehia hizo, na tulifanya vikao na jamii, ambavyo vililenga kupambana na udhalilishaji,’’alifafanua.

Kwa upande wake, kiongozi wa dini Robart Migua Ndalami, alisema wamekuwa wakishirikiana na jamii, katika vita dhidi ya udhalilishaji.

Mapema Moza Massoud Amour, kutoka wizara ya Kazi na Uwezeshaji, alisema hivi karibuni, waliwarejesha skuli wanafunzi 13, kati ya 62 waliowagunda wameacha masomo katika skuli mbalimbali.

Akiwasilisha kazi za utendaji wa kazi za dawati la jinsia na ulinzi wa mtoto, Habiba Khamis Mussa, alisema waliwafikia wanafunzi 5,887 wakiwemo wanawake 3,591 na wanaume 2,296 katika skuli kadhaa za wilaya ya Chakechake kuwapa elimu.

Alisema, bado jamii inahitaji elimu kwa upana zaidi, kujua viashiria ya vitendo vya udhalilishaji, kwa wanawake na watoto wilayani humo.

Akighairisha kikao hicho kazi, Kaimu Mwenyekiti huyo Kassim Ali Omar, aliwasisitiza wajumbe hao, kuifikisha elimu waliyoipita, kwa jamii.

Moja ya majukumu ya Kamati hiyo, ni kuratibu elimu, ushauri kwa jamii, ili kuhakikisha watoto wanaishi bila ya udhalilishaji.

                         Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...