NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
SHIRIKA la Umoja wa mataifa la UN-Women, limesema litaendelea
kufanyakazi na taasisi ya FAWE Zanzibar, kwa maslahi ya kuwasaidia wajasiriali
wa mazao, yanayolimwa baharini na nchi kavu.
Hayo yameelezwa jana Febuari 17, 2026 na Mwakilishi wa shirika hilo upande wa
Tanzania Emile Kivugo Mwakafundu, alipokuwa akiwasalimia wajasiriamali, wanaoendelea
na mafunzo ya mnyonyoro wa thamani, yanayofanyika kituo cha elimu mbadala Wingwi
Micheweni Pemba.
Alisema UN-Women ni mdau mkuu wa maendeleo ya jamii, wakiwemo
wajasiriamali wa uzalishaji muhogo, majongoo bahari, mwani pamoja na wakulima wa
migomba, ili kuziongezea thamani biadhaa hizo.
Alisema, shirika hilo linawajali wajasiriamali hao, ili kuhakikisha
wanaziongezea thamani bidhaa zao kwa lengo la kukuza pato lao.
Alieleza kuwa, haiwezekani kwa mkulima, baada ya kuvuna mazao yake,
kwenda kuyauza sokoni kama yalivyo, bali ni kuyachakata, ili aongeze pato lake.
‘’UN-Women inaendesha maradi huu wa pamoja kwa lengo la kuhakikisha
sasa mkulima ama mjasiriamali, anakuza pato lake,’’alifafanua.
Aidha mwakilishi huyo wa UN-Women alisema mradi huu unaendeshwa
mkoa wa kaskazini Pemba na kaskazini Unguja, ili kuwafikia wajasiriamali
walioekeza kwenye vilimo hivyo.
Mkufunzi wa mafunzo hayo Shadrack Kikoti, alisema mnyororo wa
thamani kwa wajasiriamali wa migomba, mwani, majongoo bahari na muhogo ni
muhimu kwa ajili ya kuongeza pato lao.
‘’Muhogo ukilimwa na kisha kuuza kama ulivyo, hauwi na thamani kwa
mkulima na hatopata kipato kikubwa, na ndio maana tupo kwenye mafunzo haya
kuelekezena hilo,’’alifafanua.
Kwa upande wake Afisa Miradi kutoka FAWE- Hija Hamad Issa, alieleza
kuwa washiriki wa mafunzo hayo ni wale wenye mawazo ya biashara, ambao
wameshaanza ama bado, ili kujifunza.
Alifafanua kuwa, FAWE imegundua wajasiriamali waliowengi wanawekeza
kwenye uzalishaji, ingawa upatikanaji wa kipato chao, uko chini.
Alieleza kuwa, FAWE inayomatumani makubwa, baada ya kumalizika kwa
mafunzo hayo, ikiwemo jamii ya wakulima kuongeza pato lao.
‘’FAWE imewaalika wajasiriamali wanaolima muhogo, ndizi, majongoo
bahari na mawani, ili kuona mnyororo wa thamani unaongezeka kwao,’’alifafanua.
Hata hivyo aliwataka washiriki hao kuhakikisha, wanakuwa makini
darasani, ili kufahamu wanachoelekeza mataalamu, kwa maslahi hayo hapo baadae.
Mapema Afisa Kilimo wilaya ya Micheweni Is-hak Khamis Shaame,
alisema ardhi ya Micheweni iliyojengeka ya mawe, haina madhara ya upandaji wa
migomba.
‘’Hata kama ardhi ya Micheweni imeumbwa kwa mfano wa mawe, lakini
kama ukipata maji kwa kilimo cha migomba ndio pahala pake,’’alifafanua.
Nae mshiriki wa mafunzo hayo Katija Mbaoruk alisema, mafunzo hayo
ni mazuri, maana wamekuwa wakitumia nguvu, katika uzalishaji na kupata pato
dogo.
Mjumbe wa kikundi cha upandaji migomba cha ‘tujitegemee’ cha shehia
ya Majenzi wilaya ya Micheweni Fatma Juma Abdalla, alisema sasa wanakwenda
kuongeza pato lao.
Alisema, walidhani wai hawawajibiki kuzichakata na kuzisarifu
ndizi, kwa ajili kuongeza pato lao, ingawa baada ya mafunzo hayo, amepata
uwelewa.
‘’Mafunzo haya yaliyotayarishwa na FAWE-Zanzibar, kwetu sisi
wakulima wa zao la ndizi, yametusaidia mno, maana sasa tumeshaelewa namna ya uchakataji
na usarifu,’’alifafanua.
Mafunzo hayo ya siku nne kwa
wajasiriamali hao 20, yanalenga kuimarisha na kuzipandisha thamani bidhaa zao,
ikiwemo ya mwani, majongoo bahari, muhogo na indizi.
Mwisho
Comments
Post a Comment