NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
SHILINGI milioni 107,190,000 zilizotarajiwa kukusanywa na Baraza la Manispaa Chake chake Pemba, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka huu, hazikupatikana, baada ya wajasiriamali kugoma kukitumia kituo chao cha Michakaini, kwa wakati.
Imebainika kuwa, kituo hicho kipya kilichojengwa kwa
ajili yao, kina milango 63 ya maduka, ambapo kila mmoja Baraza lilikusudia
kuukodisha kwa shilingi 50,000 ili lijipatie shilingi milioni 3,150,000 kwa kila
mwezi mmoja.
Ingawa imebainika, baada ya wajasiriamali hao kukataa
kuingia kituoni humo, Baraza hilo, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka
huu, limeshapoteza shilingi milioni 85,050,000.
Aidha mapato ya shilingi ya milioni 22,140,000 nayo hayakukusanywa
na Baraza hilo kwa kipindi hicho, yaliokuwa yatokane na vizimba ‘vikuta’
82, ambapo kila kimoja, kilitarajiwa kukukodishwa kwa shilingi 10,000 kwa
wajasiriamali.
Ikafahamika kuwa, vikuta hivyo kama vyengepata wajasiriamali,
kwa mwezi mmoja Baraza lingekusanya shilingi 820,000, sawa na jumla shilingi
milioni 3,970,000 ijumuisha na kodi ya milango 63.
Ndani
ya kituo hicho kilichofunguliwa mwezi Novemba mwaka 2023, Baraza la Manispaa
lilitarajia wajasiriamali wa nguo za mtumba na wauza viatu, wakitumie kituo
hicho, na kuanza kulipia vikuta 82 na milango 63.
Na ndio
maana baada ya wajasiriamali hao wa mji wa Chake chake kugoma kikutimia kituo
hicho, walilisababishia Baraza la Manispaa hilo, kupoteza mapato ya zaidi ya shilingi
milioni 107.190 kwa fremu 63 za milango na vizimba 82.
Uchunguzi ulibaibi kuwa, baada ya kufunguliwa kwa kituo hicho mwezi Oktoba mwaka 2023, mwezi uliofuata Baraza hilo la Manispaa, lilianza kuwahamisha wajasirimali, hasa wauza mitumba na viatu kuhamia kituoni hapo.
Kwa wakati
huo Askari na uongozi mzima wa Baraza la Manispaa, lilihamia ndani ya mji wa
Chake chake, ili kuwasaka wajasiriamali, wanaopanga bidhaa zao chini na
kuwaomba kuingia kituoni hapo.
Msaidizi
Ofisa Mapato wa Baraza hilo, Said Mabrouk Juma, alikiri kuwa, kulikuwa na ugumu
kwa wajasiriamali wa nguo za mtumba, viatu na urembo kukitumi kituo hicho.
‘’Pamoja na kuwatumia
hata askari wa jiji na wakati mwingine na Mkurugenzi kuwapitia, lakini walikataa
na sisi kuendelea kupoteza mapato,’’alifafanua.
Alieleza
kuwa, baada ya kugoma kuingia kituoni hapo, waliwaomba tena kwa mara nyingine,
kwa sharti la kuwaondolea kodi, na kuwaomba kuchangia fedha ya umeme shilingi
20,000 na kukubali.
‘’Wapo
waliokubali kuingia kituoni hapo, ingawa walituomba na kukubalia nao, kwamba
wasitozwe kodi na badala yake wachangia huduma ya umeme, na hadi sasa hilo linaendelea,’’alifafanua.
Mkurugenzi
wa Baraza hilo Shida Kombo Mohamed, alisema kuanzia mwezi Januari mwaka 2025,
rasmi walipokubaliana na wajasiriamali hao, kuchangia gharama za umeme, kwa
kila aliyekodi mlango.
‘’Ni
kweli wakati wanahamia kituoni hapo, hata biashara ilikuwa chini kwa kukosa
wateja, na ndio maana tuliwaomba kuchangia huduma umeme, kwa shilingi 20,000 kwa
mwezi,’’alifafanua.
Hata
hivyo, Mkurugenzi huyo alisema wanampango kuanzia mwezi ujao, kila mlango
mmoja, kuuwekea mita yake ya umeme, ili kuondoa changamoto ya matumizi kama yaliyopo
sasa.
‘’Kwa
sasa mchango wa umeme uko sawasawa kwa kila mjasiriamali, ingawa baada ya kushauriwa
kuhusu kila mmoja kuwa na mita yake, tumelikubali na harakati zimeshaanza,’’alifafanua.
Baadhi
ya wajasiriamali waliopo kituoni hapo, walikiri kuwa walikosa uwelewa na
kuchelewa kuhamia ndani ya kituo hicho, jambo lililochelewa kupanua biashara
zao.
Hija
Omar Khamis, alisema kwa sasa biashara eneo hilo imetononoka, baada ya wateja
kuzoea kituoni hapo, tokea walipohamia mwezi Januari mwaka jana.
Kwa upande
wake Khadija Sultan, alisema umaarufu wa bidhaa za nguo za mtumba kituoni hapo,
kinaendelea kukua, kadiri siku zinavyosonga mbele.
‘’Ni
kweli pale mwanzo, tulipokuwa tukiondolewa ndani ya mji wa Chake chake, tuliona
kama tunaonewa, ingawa sasa biashara imechangamka kiasi,’’alieleza.
Kituo
hicho cha wajasiriamalia Chake chake, ambacho kina milango 63 na vizimba 82, kilifunguliwa
mwezi Okatoba mwaka 2023, kimejanga na serikali ya awamu ya nane, kwa lengo la kuwapa
utulivu wajasiriamali.
mwisho


Comments
Post a Comment