Skip to main content

MCHANGO WA WANAUME HUU HAPA KUWASAIDIA WANAWAKE KUPATA ARDHI

 


 NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@

UPO usemi maarufu kuwa, uchumi wa mwanamme ni wake pekee, lakini wa mwanamke ni wa jamii

Wacha tuone, ushahidi wa hili, maana Mwanaisha Haji Makame (78) wa shehia ya Mchanga mdogo, anasema huo ndio ukweli.

‘’Haikuwa ni methali tu hizi za watu wa kale, bali ukweli wake upo na unanafasi hadi kwa wanawake na jamii ya leo.

Anafafanua kuwa, mwanamke anapokuwa na mali, huwa ni jamii, kutokana na huruma na upeo wake wa maisha ya sasa na baadae.

Hili linaungwa mkono na Mchanga Said Shamisi (55) nae wa Mchanga mdogo wilaya ya Wete, akisema ukitaka jamii isiishi na umaskini, wawezeshe wanawake.

Makame Ussi Makame (40), nae wa eneo hilo, ijapokuwa mitheli hiyo haikuikubali kwa asilimia 100, lakini haikatai kwa asilimia hizo pia.

Aisha Hassan Mohamed (19), anasema misemo ya watu wa zamani, ilikuwa na ukweli, na na hiyo inaendelea kuishi hadi sasa.

‘’Kwa mfano Chama cha waandishi wa habari Tanzania TAMWA-Zanzibar, ilipoendesha mafunzo ya kilimo msitu, nilipata posho, nilijumuika na wanafamilia,’’anafafanua.

Kassim Mohamed Kassim (22), yeye hakubaliana na hilo, alisema mali ya mwanamme ndio huwa ya jamii, kwa kule kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja.

‘’Mimi pesa yangu kwa mfani huenea kwa wake zangu wanne, na wao kama wanafamilia wanaweza kupata, kupitia yangu, jee,’’anahoji.

Mkurugenzi wa TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anakubali moja kwa moja, kuwa mali ya mwanamke inaweza kuwa ya familia.

Anasema kwani, wanawake ni nyenzo Madhubuti na kiunganishi cha familia moja na nyingine, na kwa kule kuwa madbubuti na imara wa uchumi, jamii hula kupitia yeye.

‘’Ndio maana fedha ya mwanamke, ikipatikana inaweza kuzaa mali nyingine, kuliko ya awali,’’anasema.

 Pamoja na kuwepo mafanikio na juhudi za wanawake katika sehemu kadhaa, ikiwemo za kiuchumi, na kijamii bado inaonekana suala la mabadiliko ya tabianchi, linaendelea kuwa na madhara makubwa kwa wanawake. 

Wanawake wanazidi kuonekana kama watu walio katika hatari zaidi ya kuathirika na mabadiliko ya tabianchi, kuliko wanaume, kwani wengi wao ndio wategemezi.



Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), wanawake pia ni watu wa kwanza kuhisi madhara ya mabadiliko ya tabianchi.

Kwa mfano chini Kenya, baadhi ya wanawakewanalazimika kutembea zaidi ya kilomita 10, kutafuta kile wanachohitaji, ili kulisha familia zao pamoja na kutafuta maji. 

Matumaini ya wanawake wa kisiwa cha Pemba shehia ya Chwale Wilaya ya Wete ni kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi, kwa kujikita katika kilimo msitu. 

Wanawake hawa, wameweka matumaini makubwa juu ya umuhimu wa kilimo msitu huku wakiamini ndio mkombozi mkubwa wa maisha yao.

Ingawa wanawake hao ni wale waliomo kwenye mradi unaoendeshwa na Jumuiya ya Uhifadhi wa misitu Pemba ‘CFI’ na ‘CFP’ wanaofanyakazi kwa karibu na TAMWA Zanzibar, na hasa baada ya serikali ya Canada kutoa fedha na Serikali ya Zanzibar kuridhia. 

Pamoja na kwamba mradi huo imeanza kwa shehia nane  kwa Unguja na Pemba, ikiwemo wanawake wa shehia za Mchanga mdogo, Kambini, Kiuyu minungwini na Chwale kwa Pemba.  

Sasa wanawake wa maeneo hayo wameshaamka na kujikita katika harakati za kilimo hicho, ambacho wanasema iwapo watakiendeleza watakuwa na uhakika wa kuyamudu maisha yao.

Kilimo msitu amabacho ni mchanaganyiko wa mazao mbalimbali kama migomba, minanasi, mbazi, michikichi, njugu, mahindi na miembe. 

Rehema Salim Issa wa Chwale Weete anasema, kilimo msitu kinawapa uhakika wa chakula katika maisha yake. 

Ingawa kilimo hicho kimekabiliwa na athari kubwa ya mabadiliko ya tabianchi bado wanaendelea nacho.

Anaona pamoja na kuonesha juhudi, kubwa katika kilimo hicho bado mabadiliko ya tabianchi yanawaathiri, ikiwemo jua kali na kupelekea kilimo chao kuharibika.

Anasema suala la jua kali limechangia kutokuwa na maji na vipando kupotea kwa haraka, jambo ambalo hukabiliwa na ongezeko la umaskini. 

"Kilimo hichi tunakitegemea kujikwamua na umaskini kwani tunapata chakula, ila jua kali limetukosesha kupata maji na imechangiwa miti kufa,’’anasema.

 Mkulima kiongozi Hadia Omar Haji wa kijijini hapo, anasema kilimo hicho kinawanufaisha kwa muda tofauti ikiwemo muda mfupi, kati na mrefu.



Kumbe, ili waweze kunufaika kama ilivyo maumbile ya kilimo hicho, huduma ya maji ya kumwagilia ni muhimu.

“Kusema kweli tatizo la mabadiliko ya tabianchi yanatuweka katika hali ngumu, kwani sasa ni jua hatujui ikija mvua itakuwaje,’’anaeleza.

Kwa vile wanawake ndio wakaaji wa nyumbani kuliko wanaume, hutumia muda mkubwa kuwashughulikia watoto kwenye mambo mengi, ikiwemo kula.

"Wenzetu wanaume si sana kuteswa na njaa kwani wao si wakaaji wa nyumbani, kama tulivyo wanawake na watoto wetu yeye akitoka hupata cha kujitafunia,"anasema.  

Bikombo Khamis Hamad anasema kuwekeza kwa wanawake na wasichana, kunaleta matokeo makubwa ambayo yanaigusa jamii, na maarifa waliyonayo wanawake yanahitajika sasa kuliko wakati mwingine.

WANAUME WANAMCHANGO UPI KUSIAIDA WANAWAKE KUPATA ARADHI

Ali Khamis Juma wa shehia ya Mchanga mdogo, anasema baada kumuona mke wake, anahangaika kusaka ardhi ya kilimo, alikopa fedha na kumnunulia.

''Nilimnunulia mke wangu ardhi na nimemuandikia yeye, na sasa ameshaanza kilimo mseto, akiwa na ardhi yake, ingawa ni upana wa uwanja wa mpira nusu,''anasema.



Khalid Juma Makame wa Kambini, anasema mradi wa ZANADAPT, umekuja kuwakumbusha wajibu wao, na sasa baada ya kufariki baba yao miaka mwili, wameamua kurithi.

''Ni kweli sasa tumsharithi na mdogo wangu Aisha amepata ardhi yake na ameshalima miparachichi 10 na migomba ya mkono 20,''anasema.

Nae Hija Khamis Khamis anasema, ijapokuwa hawajakamilisha taratibu za kurithi, lakini kwa sasa wako mbioni ili kuhakikisha dada yake anapa haki yake ikiweko ardhi.

Kassim Juma Hemed na Haji Makame Haji, wanasema  ijapokuwa hawana ardhi za kurithi wala uwezo wa kununulia wake zao ardhi, lakini wamewapa ushauri.

''Kwa mfano mimi mke wangu, tumepanga mwakani tukodi mikarafuu, na fedha tutakayoipata tununune ardhi kwa ajili ya kilimo,'amasema Haji.

 FAIDA YA KILIMO HICHO

Mkulima anaweza kunufaika na kilimo msitu kwa kumpatia mahitaji yake ya msingi kama vile kuni, matunda, kurutubisha udongo malisho ya mifugo, dawa za asili.

Nyingine ni usindikaji wa bidhaa zitokanazo na mazao ya misitu kama vile juisi, jamu na asali.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya uhifadhi wa misitu  Pemba Mbarouk Mussa, anasema  kutopatikana kwa mvua, kukata miti ni jambo jingine linaloendelea kuathiri.

Anasema athari mbalimbali za ukataji wa miti kwa shughuli za kijamii, zimekuwa zikijitokeza  katika maeneo tofauti,  huku jumuiya hiyo  ikiendelea kutoa elimu.



Afisa kilimo kutoka CFP Saada Juma,  anasema kupitia mradi huo haujabaguwa, ingawa lengo ni kuwainuwa wanawake  katika shughuli za kujitafutia kipato. 

Afisa mdhamini Wizara ya kilimo, umwagiliaji  Maliasili  na Mifugo  Muhandisi  Idriss Hassan Abdulla, anafafanuwa kuwa,  wameandaa mpango maalum wa kuhakikisha  wanazalisha kupitia kilimo msitu.

WANAUME WANASEMAJE

Hamad Ali Suleiman, anasema wanatambua mchango mkubwa wa wanawake, katika kukiendesha kilimo msitu kwani hawako nyuma katika kuhakikisha kinaendelea. 

Juma Omar Hassan, anawashauri wanaume kuwaruhusu wanawake, kujiingiza katika kilimo hicho na ili waweze kujikwamua na maisha.



Chama cha waandishi wa Habari wanawake TAMWA Zanzibar, nao husimamia kidete  haki za upatikanaji wa usawa wa kijinsia na kuwashirikisha wanawake. 

Mkuu wa mawasiliano na Habari TAMWA Sofia Ngalapi anawataka wakulima hao, wasikae kimya, katika kueleza changamoto zinazowakwaza katika kilimo chao. 

mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...