Skip to main content

WATU WENYE ULEMAVU PEMBA WAKASIRISHWA KUBANDIKWA MAJINA 'FEK'

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

SHERIA ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar nambari  8 ya 2022 kifungu cha 45 kinakemea udhalilishaji kwa watu wenye ulemavu.

Kwa kueleza mtu yeyote atakae mdhalilisha au kumkandamiza mtu mwenye ulemavu, kwa kumuita jina lisilofaa kutokana na aina ya ulemavu wake, atakua ametenda kosa.

“Atakae tiwahatiahi kwa kufanya kosa hilo, atalipa faini isiyopungua shillingi 100,000 na isiozidi shillingi million 1, au kifungo kwa kipindi kisichopungua mienzi miwili au vyote wiwili”, kimefafanua.

Mkataba wa kimataifa wa watu wenye ulemavu wa mwaka 2006 ibara yake ya 17, inazungumzia kuhusu kuheshimu tofauti za kimaumbile.

“Kila mtu mwenye ulemavu anayo haki ya kuheshimiwa kwa ukamilifu wake kimwili na kiakili kwa misingi ya usawa na watu wengine,” imeeleza ibara hiyo.

Ieleweke kua katika jamii, lugha ina nguvu kubwa katika kuunda mitazamo na hisia kuhusu makundi mbali mbali ya watu.

 Hata hivyo, matumizi ya majina na lugha zisizofaa, yanaweza kuathiri vibaya jinsi tunavyo watendea wingine, hasa wale wenye ulemavu.

Pamoja na kuwepo kwa sera kanuni na sheria zinazotaka watu wenye ulemavu kuheshimiwa na kuthaminiwa kwa kutofanyiwa udhalilishaji wa aina yeyote, bado jamii haijaliafiki hili.

 Sheria za kuwalinda watu wenye ulemavu ni muhimu sana katika kuhakikisha haki zao zinaheshimiwa na wanapata fursa sawa katika jamii, ingawa hazifuatwi ipasavyo.

Kwani wapo wanao wadhalilisha kimwili, hata kiakili kwa matumizi yao ya lugha iliyojaa kejeli , ikiwemo kuwaita majina kutokana na aina ya ulemavu wao na kuacha jina halisi.

WATU WENYE ULEMAVU

Zuhura Haji mwenye ulemavu wa uziwi anasema, jina lake sasa halitiliwi maanani katika jamiii inayo mzungumka, na badala yake huitwa jina kutokana na aina yake ya ulemavu.

Amekua akipambana na hili kwa muda mrefu na hadi sasa ameamua kukaa kimya ingawa si jina linalo mridhisha.



Said Saleh Sultan mwenye ulemavu wa viungo, anasema katika jamii yake aina  ya ulemavu imekua  umaarufu au utambulisho wake, ingawa haridhishwi na hafurahishwi na hilo.

Aneleza pamoja na kukataa na kuelimisha jamii juu ya athari ya jambo hili, bado jamii haijakubali kuwapokea watu wenye ulemavu, kutokana na walivyo.

“Watu hutumia aina yangu ya ulemavu kama ni utambulisho wangu, na jina langu kamili limesahaulika kabisa, si pendi iwe hivi ila jamii haijakubali utofauti wa kimaumbile tulionao” anaeleza.

Rehema Juma Makame mwenye ulemavu wa uoni anasema sio yeye tu, hata watoto wake huitwa jina lililoambatana na aina ya ulemavua alio nao.

Anasema hili halimuathiri yeye pekee, bali hata watoto wake kwani wanapokua mitaani na watoto wingine, watu hutumia ulemavu wa mama yao, kama ni adhabu kwao.


Halima Ahmada Hussein ni mzazi mwenye mtoto mwenye ulemavu anasema, mtoto wake mwenye ulemavu wa viungo, hukataa kujumuika na wenzake na kunawakati alikataa kwenda skuli kutokana na watu kumdhalilisha.

JAMII

Habibu Khatib Faki wa Mjimbini Mkoani Pemba anasema, suala hili mara nyingi huanza katika ngazi ya familia.

Anaeleza baadhi ya wazazi walezi au watu wa karibu na watu wenye ulemavu, huwatambulisha kwa majina yatokanayo na aina ya ulemavu wao badala ya majina yao ya kuzaliwa.

“Katika hili familia zinamchango mkubwa, kwani baadhi yao hutumia majina yatokanayo na ulemavu wa mtu katika kumtambulisha, na hapo jamii hujenga mazoea”, anafafanua.

Khulayta Hamad Shapandu wa Micheweni  anasema, hali hii pia husababishwa na uwelewa mdogo wa jamii kuhusu unyanyapaa na athari zake, kwa yeyote atakae fanyiwa.

Anaeleza kuwa, jamii haina uelewa wa nini maana ya unyanyapaa, na wingi wanadhani unyanyapaa ni wa kimwili pekee na mengineyo hunaona ni kawaida.



JUMUIYA ZA WATU WENYE ULEMAVU

Maryam Mohamed Salim Afisa watu wenye ulemavu Pemba wa ‘UWZ’ anasema hili ni miongoni mwa tatizo kubwa linalowakumba watu wenye ulemavu.

Anaeleza changamoto hii, ni ya muda mrefu ingawa kila siku jamii inaelimishwa juu ya athari za jambo hili.

Mratibu baraza la watu wenye ulemavu Pemba Mashavu Juma Mabrouk anasema, hali hii husababisha watu wenye ulemavu kujitenga na kujiona wamekosa thamani.

Huathirika saikolojia ya watu wenye ulemavu na kusababisha  kujikataa na mwisho kuvunja ustawi wao.

NINI KIFANYIKE?

Hidaya Mjaka Ali ni mwenye ulemavu wa viungo anasema vizuri  jamii kuanzia ngazi ya familia, kulipiga vita suala hilo, kwa kuhakikisha kila mmoja anakua  na uelewa kuhusu athari za unyanyapaa.

Mashavu Khamis Omar wa Kangani Pemba anasema, vizuri taasisi zinazohusika kushiriki katika kutoa elimu kwa jamii kuhusu nini unyanyapaa.

Afisa Ustawi wa Jamii wa taasisi ya Early Childhood Program Zanzibar (MECP-Z) Haji Ali Hamad anasema, ni vizuri, jamii kukubali tofauti za kimaumbile zilizopo, ili kukuza utu na heshma ya kila mtu katika jamii.

MWISHO

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...