Skip to main content

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA MCT, TAMWA, ZPC, WAHAMAZA, THRDC

 


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI SIKU YA HAKI ZA BINADAMU DUNIANI 2025 

 Kamati ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) inaungana na wanaharakati, wanahabari, na watetezi wa haki za binadamu duniani kote,  kuadhimisha siku ya Haki za Binaadamu ambayo hufanyika kila ifikapo tarehe 10 Disemba ya kila mwaka. 

 Kaulimbiu ya mwaka huu, haki za binadamu kama “Mahitaji ya Kila Siku”, inasisitiza kuwa haki hizi lazima zilindwe bila kusuasua kila siku, kwa kila mtu, na katika kila mazingira.

 Katika maadhimisho ya mwaka 2025, ZAMECO inasisitiza kwamba uhuru wa kupata na kutoa taarifa ni nguzo muhimu ya utawala bora na msingi wa kulinda haki nyingine zote za binadamu. 

Haki hii haipaswi kutazamwa kama ridhaa ya mamlaka bali kama wajibu wa kikatiba na kimataifa unaopaswa kuheshimiwa, kulindwa na kutekelezwa.

 Tunawakumbusha wadau wote kuwa tangu kupitishwa kwa Tamko la Ulimwengu la Haki za Binadamu (UDHR) mwaka 1948 uhuru wa kujieleza umeendelea kuwa nguzo muhimu katika kuhakikisha kwamba jamii inakuwa na nguvu ya kushiriki, kuuliza, na kuhoji madaraka.

 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar katika Ibara ya 18 zimeeleza haki hiyo ya kujieleza na kupata taarifa.

 Hii hupelekea upatikanaji wa taarifa sahihi, waandishi wa habari na wananchi wanapata uwezo wa kuhoji, kushiriki, kuwawajibisha watawala na kuchochea uwazi katika masuala ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

 Hata hivyo, pamoja na msingi huu muhimu, bado tasnia ya habari Zanzibar inakumbana na vikwazo vinavyozuia utekelezaji kamili wa haki hizi. Sheria zilizopitwa na wakati, mazingira ya hofu, vitisho dhidi ya waandishi, pamoja na ukosefu wa upatikanaji wa taarifa za umma kwa wakati. 

Hali hii inadhoofisha uwezo wa vyombo vya habari kufanya kazi yao kwa uhuru na uadilifu na kuwanyima wananchi haki ya kupata taarifa sahihi, jambo ambalo linaathiri ushiriki wao katika maamuzi ya nchi.

 Sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988 ilifanyiwa marekebisho mwaka 1997 pamoja na Sheria ya Tume ya Utangazaji Zanzibar ya mwaka 1997 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010 ambazo zinaendelea kutoa mamlaka makubwa kwa taasisi za usimamizi na kuathiri uhuru wa vyombo vya habari kufanya kazi kwa weledi na bila ya hofu.

 Katika taarifa yake ya mwisho kwa waandishi wa habari, kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, ZAMECO ilieleza masikitiko yake ya kuzorota kwa mazingira ya upatikanaji wa habari na ukiukwaji wa haki za kujieleza na kupata habari. 

Miongoni mwa ukiukwaji huo ni kunyimwa taarifa muhimu kwa waandishi wa habari, kutishiwa kufungiwa kwa baadhi ya vyombo vya habari kutokana na kutokulipa ada na kurusha maudhui ambayo hayakuelezwa bayana tatizo lake.

 Pamoja na changamoto hizo, ZAMECO inaona umuhimu mkubwa wa wadau wote kushirikiana kurejesha imani na kujenga mazingira salama na huru kwa uandishi wa habari. 

Tunatoa wito kwa Serikali ya Zanzibar kufanya mapitio ya kina ya sheria za habari ili ziendane na hali ya sasa ya soko huria, maendeleo ya teknolojia, matakwa ya Katiba, viwango vya kikanda na kimataifa. Katika Maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu ya mwaka huu, ZAMECO inasisitiza kuwa uhuru wa habari ni uti wa mgongo wa utawala bora na msingi wa demokrasia jumuishi. 

Hakuna maendeleo, uwajibikaji, wala uchaguzi huru bila habari huru na waandishi walio salama. Kwa msingi huo, ZAMECO itaendelea kusimama imara kutetea haki, usalama, na maslahi ya waandishi wa habari Zanzibar, huku tukihamasisha wadau wote kutambua haki zao na kuzidai pale zinapokiukwa. IMETOLEWA NA:

 Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA) Baraza la Habari Tanzania, Zanzibar (MCT, ZNZ) Jukwaa la Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania, Zanzibar (THRDC, ZNZ).

MWISHO 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...