Skip to main content

ELIMU MJUMUISHO KEKI YA TAIFA INAYOLIWA NA WANAFUNZI WASIOONA, WAIPA TANO SMZ

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

TUPO katika ulimwengu ambao mara nyingi mafanikio ya mtu kimaisha huhusishwa na elimu.

Sio tu ya utambuzi wa mazingira, bali na ile ipatikanayo  darasani.

Kupata elimu hiyo kwa Zanzibar si changamoto hasa baada ya kufanya mapinduzi yake mwaka 1964, na kuanza kujitawala.

Kwani katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu 10 (f), kinasisitiza kuwa Serikali inawajibu wa kutoa  fursa  za kielimu kwa watu wote katika madaraja yote.

Katika hili, hakuna aliebaguliwa  kwa  sababu yeyote ile, lengo likiwa ni kumjumuisha kila mtu wakiwemo wenye ulemavu.

Kwani baadhi ya watu, walidhani kwa watu wenye ulemavu  kusoma  ni anasa na sio muhimu.

Ndipo mikataba ya kimataifa na kikanda, sheria, pamoja sera mbali mbali zikazungumzia haki ya elimu kwa watu hawa.

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu wa mwaka 2006, katika ibara ya 24 imezitaka nchi wanachama kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata elimu.

"Nchi wanachama zihakikishe mfumo wa elimu hauwatengi watu wenye ulemavu na watoto wenye ulemavu hawabaguliwi kwa misingi ya ulemavu wao", kimeeleza kifungu cha 2 (a) cha ibara hiyo.

Sheria ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya 2022 kifungu  cha 28 (1) (a) kimeeleza, watu wenye ulemavu wanastahili haki zote za msingi za kibinaadamu, kama ilivyo kwa wingine ikiwemo ya elimu.

Aidha, sera ya elimu ya Zanzibar ya 2006 inasisitiza Wizara ya Elimu itahakikisha haki na fursa za elimu inazotoa kwa wazanzibari wote, zinatolewa kwa misingi ile ile kwa watu wenye ulemavu.

“Ulemavu kwa kadri itakavyowezekana hautakua kikwazo wala sababu ya kumnyima mwanadamu haki ya elimu, " imeeza sehemu ya sera hiyo.

Kwa bahati nzuri haki hii haikutolewa kwa mtu mwenye aina fulani ya ulemavu, ikiwa na maana ulemavu wa aina yeyote si kikwazo cha mtu kupata elimu.

Je? utekelezaji wa hili ukoje kwa wanafunzi wenye ulemavu wa uoni?

Said Salum Khamis mwanafunzi wa skuli ya Elimu Mjumuisho Pujini mwenye ulemavu wa uoni hafifu anasema, haki ya elimu kwasasa wanaipata.

Anasema ipo skuli anayosoma inamiundombinu rafiki kwao, ikiwa ni waalimu wenye taaluma, vifaa na miundombinu rafiki ya majengo.

Nasria Ali Salim mwanafunzi mwenye ulemavu wa uoni katika skulini hapo, anasema anafursa ya kujifunza kwa uhuru, kama ilivyo kwa wanafunzi wingine wasio na ulemavu.

Anaeleza kuwepo kwa skuli hiyo inayowajumuisha kunawawezesha  kujifunza na kutimiza ndoto na malengo waliyojiwekea.

“Wenye ulemavu wa uoni tunafaraja kwani tunajifunza  kama ilivyo kwa wingine wasio na ulemavu, na naamini  ni fursa ya kutimiza ndoto tulizojiwekea”, alieleza.

Anaipongeza serikali kwa kuanzisha skuli hiyo kwani inaonyesha kujali kwao umuhimu wa upatikanaji wa elimu kwa kila mtoto katika jamiii.

WAZAZI

Salim Kassim wa Tasini Mkoani Pemba ni mzazi wa mwanafunzi mwenye ulemavu wa uoni anasema, ujumuishaji watu wenye ulemavu katika elimu umekuja kuwakomboa watoto wao.

Maana kabla walikua na hofu ya kutopatikana haki ya  elimu kwa watoto wenye ulemavu wa uoni, kwa kutokuwepo miundombinu rafiki ya kujifunzia katika skuli za kawaida.

Sabiha Issa Mohamed wa Mjimbini ni mzazi wa  mwanafunzi mwenye ulemavu wa uoni anasema,  juhudi za kuwajumuisha watoto wenye ulemavu katika elimu zinafanyika na  zimewapa faraja.

Kwa sasa watoto wanapata fursa ya kujifunza bila kujali hali zao na maeneo wanayoishi, kutokana na kuanzishwa skuli ya elimu mjumuisho.

"Kwa sasa watoto wetu wenye ulemavu wa uoni wanayo fursa ya kusoma, hii inaleta faraja kwetu wazazi, kwani elimu ndio urithi pekee wa kuwaachia watoto", anaeleza.

WAALIMU

Hanifa Abeid Ali mwalimu wa wanafunzi wenye ulemavu wa uoni skuli ya Elimu Mjumuisho Pujini anasema, uanzishwaji skuli hiyo, ni miongoni mwa juhudi za utekelezwaji sera ya elimu mjumuisho.

Anasema katika kuhakikisha wenye ulemavu wa uoni wanapata haki yao ya elimu, skuli imekua ikisajili wanafunzi wenye ulemavu huo, kila mwaka tokea kuanzishwa kwake.

Hadi sasa skuli  ina wanafunzi 17 wenye ulemavu wa uoni , nane kati yao ni wasioona kabisa  na tisa ni wenye uoni hafifu.

Tamima Mohamed Said mwalimu wa wanafunzi wasiiona katika skuli hiyo anasema, vipo vifaa mbali mbali vya kufundishia na kujifunzia, kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu wa uoni.

Vifaa kama mashine za kuandikia, fremu za A4, vibao maalumu vya kusomea  vyenye nukta nundu, vifaa vya kukuzia herufi (magnifier) pamoja na mashine za kutolea vivuli kwa ajili ya kutayarishia mitihani.

CHANGAMOTO NI ZIPI

Moja ni uchakavu wa baadhi ya mashine hizo na upungufu wa karatasi za rangi za kuandikia kwa wenye uoni hafifu.

"Upatikanaji elimu hapa unawazingatia wanafunzi wasiiona na wenye uoni hafifu, na wanafursa ya kujifunza, tunavifaa vya kufundishia na kujifunzia,’’anasema mwalimu huyo.

Nae Mwalimu Anipae Ameir Manallah wa skuli hiyo  anasema, wanawekaweka uangalizi wa hali ya juu wanapokua darasani wanafunzi hao, kwa kuingia waalimu wawili wawili, ili kila mwanafunzi apate uwelewa wa kutosha.

Anasema katika ufundishaji wao  huzingatia mahitaji ya kila mwanafuzi kwani darasa lao ni jumuishi.

WIZARA

Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Pemba Mohamed Nassor Salim anasema, serikali imeweka mazingira wezeshi na vifaa kwa wanafunzi wenye ulemavu wa uoni vya kujifunzia na kufundishia.

Anasema katika skuli zenye wanafunzi hao wameweka  mashine za nukta nundu za kuandikia, vibao malumu vyenye nuktanundu kwa ajili ya kujifunzia, fremu za A4 na vifaa vyengine muhimu.

Wizara itahakikisha inatatua changamoto zilizomo katika skuli hizo ikiwemo ya vifaa chakavu, maana elimu ni haki ya msingi kwa wote.

Hutuba ya bajeti ya wizra hiyo ya 2025/2026 iliyosomwa katika baraza la wawakilishi na waziri wa wizara hiyo Lela Muhamed Mussa, anasema, mazingira ya kujifunzia na kufundishia kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum yameimarika.

Sehemu ya hutuba hiyo inaeleza, idadi ya walimu waliopatiwa mafunzo ya elimu mjumuisho na stadi za maisha kwa mwaka imeongezeka kutoka 1,066 mwaka 2024/25 hadi 1,774 mwaka 2025/26.

JUMUIA ZA WATU WENYE ULEMAVU

Mashavu Juma Mabrouk Mratibu wa Baraza la watu wenye ulemavu anasema, upatikanaji haki ya elimu kwa wenye ulemavu unaendelea kumarika hasa kwa skuli za elimu  mjumuisho.

Anasema ni vyema serikali ikaongeza nguvu katika skuli za kawaida, ili  wenye ulemavu wajumuishwe  kwa kila kitu kinachofanyika kupitia skuli wanazosoma.

MWISHO

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Katika Makala haya tunawaangazia baadhi ya watu wenye ulemavu ambao wamekuwa mashuhuri kwa kushinda changamoto ya ulemavu na kufikia mafanikio ya hali ya juu katika Nyanja zao. Hawa ni baadhi yao.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...