Skip to main content

CFP, CFI, TAMWA-ZANZIBAR: ‘MRADI WA ZANADAPT WAMALIZA KIU WANAWAKE, WAANDISHI WA HABARI’

 



NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@@

SERIKALI kwa kushirikirikiana na wadau wa ndani na nje, wanayo mikakati ya kweli ya kuhakikisha, kilimo mseto kinawanufaisha wanawake Pemba.

Kwa sasa mradi wa kuwawezesha wanawake kukabiliana na mabadiliko tabia nchi, na kukidhi maisha yao, unaendeshwa na taasisi kadhaa na TAMWA ukiwemo upo shehia nne kwa Pemba.

Kati hizo ni za Mchanga mdogo, Kambini zote zikiwa mkoa wa kaskazini Pemba, ndani ya wilaya ya Wete.

Hili lilikuja baada ya tafiti kadhaa, kuonesha maeneo hayo ndio makuu yalioathiriwa na mabadiliko tabia nchi, yawe yale ya asili au yaliosababishwa na harakati za mwanadamu.

Kilimo mseto kilitajwa na wataalamu kuwa, ndio mwarubaini wa kukabiliana na mabadiliko tabia nchi, kwa kule kuhifadhi mazingira na kujipatia kipato.

KWANI KILIMO MSETO NI KIPI?

Mitandao inaelekeza kuwa, ni mfumo wa kilimo cha mseto hujumuisha mambao kadhaa, yakiwemo, ukuzaji wa mimea na miti ya aina fulani kwa pamoja kwenye shamba.



Mfumo huu waweza kuandaliwa kwa zamu au hata kujumuishwa kwa pamoja bila kuzingatia msimu.

Ikaelezwa kuwa, mifugo na mimea ya chakula hujumuishwa kama sehemu ya mfumo huo, ili kuhakikisha mkulima anaendesha kilimo bila ya njaa.

 Kumbukuka kuwa, ni muhimu kufahamu kwamba hakuna njia moja ya kuimarisha na kufanikisha kilimo, bali mbinu za kila aina zapaswa kutekelezwa.

Mbinu hizi zaweza kujumuisha jamii nzima katika kupanda miti ya kienyeji, miti mingine yenye manufaa, mbinu za kutunza udongo.

Na njia nyinginezo za kuimarisha kilimo cha mseto, ambapo faida yake nyingine ni kunufaisha sehemu kame, zile zisizotumika kwa kikamilifu au hata zile za tindikali au udongo wa chumvi nyingi.

SERIKALI INAFANYA NINI

Afisa  mdhamini wizara ya  kilimo  Umwagiliaji  Maliasili  na Mifugo  Injinia Idriss  Hassan Abdulla anasema kilimo msitu kitawapa faida wanawake, kwani kitaifanya ardhi kuwa na rutba na kupatikana mazao kwa wingi.

‘’Unapolima kilimo mchanganyiko kutasaidia kupatikana kwa mvua, na kusaidia kupatikana kwa mazao kwa wingi,’’anaeleza.

Kama wizara wamekua wakitoa elimu kwa vikundi mbalimbali ya utunzaji mazingira ili kuona wanawake wanapiga hatua kupitia kilimo msitu.

 

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba  Salama Mbrouk Khatib amasema, kilimo msitu (mseto) kitawainua kwa kiasi kikubwa wanawake kiuchumi.

‘’Ukilima tembere utapata mboga, ukipanda miembe utavuna embe utauza utapata pesa za kununua mahitaji mingine ya nyumbani,’’anafahamisha.

Juma Bakar Alawi mdau wa mazingira, anasema  wanawake ndio wathirika wakubwa wa athari za mabadiliko ya tabianchi.



Anasema kupitia mradi huo wa uhifadhi mazingira utawasaidia wanawake kujikwamua na umasikini.

‘’Kwakweli jambo wanalolifanya Jumuia ya uhifadhi wa misitu Pemba ‘CFP’ na wenzao wa kimataifa wa ‘CFI’ la  kuleta mradi huu, ni jambo jema.



Kwani anasema wanawake watajipatia mahitaji ikiwemo kuni, na fedha za kujikimu kimaisha, kwani ndio wahanga ya umaskini,’’anasema.

Rehema  Abrahman  Alawi  ni  Afisa  kutoka CFP  anasema  mradi  wao  umelenga zaidi  kwa  wanawake  kwani  wao  ndio  waathirika  wakubwa wa  mabadiliko  ya  tabianchi.

Wamekuwa wakiwapatia elimu  pamoja  na  miche waweze kulima kilimo msitu, kwa ajili ya kujiinua kiuchumi.

‘’Unapomwambia mama apande  miti ya misitu katika shamba lake, atajipatia  mahitaji  muhimu, ikiwemo fedha kidogo anakuelewa,’’anafafanua.

 Hashim Haji Omar, anasema kilimo msitu kitawasaidia wanawake kujikomboa na umasikini, huku wakiimarisha familia zao.

Wanapolima mazao mchanganyiko katika mashamba yao, watapata chakula,  pesa,  pamoja na kupata hewa safi.

‘’Kwakweli kilimo msitu kitawafanya wanawake wapige hatua, kwani watavuna mazao kwa ajili ya  chakula, biashara, pamoja na kufahamu umuhimu wa kutunza mazingira,’’anafafanua.

Kisiwa cha Pemba ni moja ya kisiwa ambacho kimekua ni muhanga mkubwa wa masuala ya mabadiliko ya tabianchi.

Mkurugenzi  wa  Jumuia  ya ‘CFP’ Mbarouk  Mussa  Omar  anasema  kama  hakutochukuliwa jitihada zozote,  juu  ya  mabadiliko  ya  tabianchi, itakuja kusababisha baadhi ya vijiji kuhamwa kutokana na maji ya bahari kupanda kwenye majumba.



‘’Katika kijiji cha Mjini kiuyu kila ifikapo mwezi 13,14, na 15 maji ya chumvi yanaigia ndani ya majumba,’’anasema.

  Nairat  Abdulla  Ali  Afisa  kutoka  Chama  cha wandishi  wa  habari  wanawake TAMWA   Zanzibar  anashauri, kwa wanawake walionufaika na taalum, kuiendeleza.

Anasema, kinyume chake watarudi tena kwenye umaskini, huku wakipata msongo wa mawazo, kwa athari za mabadiliko tabia nchi.

 Mradi  ambao  umefadhiliwa  na  Serikali  ya  Canada na kuridhiwa na serikali ya Mapinduzi,  kuona  wanawake wamepiga  hatua.

Kwani lengo hasa la  mradi  ni  kuwainua  wanawake kiuchumi,  kupitia  mradi  huo  wa  uhifadhi  wa mazingira.



 Kufikia  Desemba  mwaka   2022,  kumekuwa  na  kesi 2,180  zinazohusiana  na  mazingira,  zilizowasilishwa kwa  taasisi  za  sheria  65  kote duniani:

Ripoti  ya  Benki  ya  Dunia  inasisitiza  umuhimu wa  kuunganisha  masuala  ya  tabianchi  katika mipango  ya  maendeleo  ya  Tanzania  kupitia  Dira  ya  Taifa  ya  Maendeleo  2050

Ambapo moja ya mkakati wa ripoti hiyo ni kusaidia  jamii zilizohatarini,  kuwa  na  uwezo  wa  kuhimili  mishituko ya  tabianchi.

Aidha  kunaweza  kusababisha  watu  milioni 2.6  kuingia  kwenye  umasikini,  na  wengine  milioni 13 kulazimika  kuhama  makazi  yao  nchini. 

TAMWA, imekuwa na nafasi kubwa ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari, katika mradi huu ulioukingoni, na sasa wameshawiva.

Fatma Hamada wa blog ya Pemba ya leo na Habiba Zarali wa Zanzibar leo, wanakiri kuongeza uweledi kwenye kuandika bahari za mabadiliko tabia nchi.

mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...