NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@
WADAU wa habari kisiwani Pemba,
wametakiwa kutumia taaluma zao katika
kuelimisha jamii kuhusu maendeleo
yalioyopatikana ndani ya awamu ya nane ya Seikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar chini ya uongozi wa Dk. Hussein
Ali Mwinyi.
Hayo yalielezwa jana Juni 21, 2025 na Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Rashid Hadid Rashid kwenye kongamano la wadau wa habari, lililofanyika katika ukumbi wa "ZRA" Gombani Chake chake Pemba.
Alisema ipo haja ya wanahabari kutumia taaluma zao vizuri, ili kuimarisha upatikanaji wa taarifa sahihi kwa wananchi, hasa zinazohusu maendeleo, kutokana na umuhimu wa taarifa hizo.
Alieleza kua serikali ya awamu ya
nane chini ya Raisi Dk. Mwinyi imepiga hatua kubwa za maendeleo katika kuwasogezea
huduma bora wananchi wake, ya maeneo mbali mbali ya mjini na vijijini.
"Serikali ya awamu ya nane, imepiga hatua kubwa katika maendeleo nchini kwa kuwasogezea huduma mbali mbali, hivyo ni vizuri waandishi kutumia taaluma zenu, kuieleza jamii mafanikio hayo, ili iwe na uwelewa wa kutosha," alisema.
Akiwasilisha mada kuhusu wajibu wa waandishi wa habari katika jamii, Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja alisema, waandishi wa habari wanawajibu wa kutoa taarifa zilizosahihi.
Alieleza kua ili waweze kutekeleza
wajibu huo vizuri ni vyema kufuata maadili ya kazi zao pamoja na kuwashirikisha
wahusika moja kwa moja, katika kupata
taarifa na takwimu sahihi watakazo zitumia.
"Uandishi ni taaluma muhimu sana kama taalima nyengine na inamiiko na maadili yake, hivyo ni muhimu kwenu, kufuata ipaswavyo kwa maslahi ya jamii na taifa kwa ujumla," alieleza.
Kwa upande wake Afisa Mdhamini Ofisi
ya Rais - Fedha na Mipango Pemba Abdul-wahab Said Abubakkar alisema, Rais wa
Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi,
amekua akitoa kipaumbele kwa waandishi wa habari, kutokana na uwezo wao wa kuisaidia serikali kwa kuonyesha mafanikio
mbali mbali yaliofikiwa.
Akifunga kongamano hilo Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamu wa pili wa Raisi Pemba Ali Salum Matta, alitoa pongezi
kwa Afisi ya Raisi Ikulu Pemba, kwa kuandaa kongamano hilo, ambalo linaweza
kuleta tija kwa jamii, kutokana na kujumuisha wadau mbali mbali wa habari.
Washiriki wa kongamano hilo walisema, ni vyema kwa taasisi zenye jukumu la kutoa taarifa husika, kutoa ushirikiano wa kutosha, katika kufanikisha hilo ikiwemo kutoa takwimu sahihi.
MWISHO
Comments
Post a Comment