Skip to main content

AHMED ABUBAKR AWA WA KWANZA KUCHUKUA FOMU CCM

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

ZOEZI la uchukuaji wa fomu za kuomba ya kuteuliwa kugombea nafasi za ubunge, uwakilishi na viti maalum kupitia chama cha Mapinduzi ‘CCM ‘wilaya ya Chake chake, linaendelea vyema.

 

Zanzibar leo ambalo lilifika ofisi ya CCM wilayani humo majira ya saa 2:00 asubuhi, liliwashuhudia wanaccm wakijitokeza mfululizo kuchukua fomu hizo, kwa nafasi kadhaa zilizotangaazwa.

 

Mtinia wa kwanza kwa nafasi ya uwakilishi kutoka Jimbo la Chonga Ahmed Abubakar Mohamed, alifika ofisini hapo majira ya saa 2:40, na kufika chumba cha kwanza, kwa ajili ya usaili, kabla ya kukutana na Katibu wa CCM na kukabidhiwa fomu.

 

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi ya CCM mjini Chake chake, mtia nia huyo alisema, ameamua kuchukua fomu hiyo, ili kuunga nguvu za Rais wa sasa wa Zanzibar, ya kuwaletea maendeleo wananchi.

 

Alisema, amekuwa akivutiwa mno na kasi ya Dk. Mwinyi jinsi anavyowafanyia wananchi wake maendeleo, na ndio maana miongoni mwa sababu zake za kuchukua fomu hiyo, ni hilo.

 

‘’Fomu hii nimekuja kuichukua ili kumsaidia kazi Dk. Hussein Ali Mwinyi, katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo la Chonga, pindi chama kikinipendekeza na kushinda,’’alisema.

 


Aliitaja sababu nyingine ya kutia nia hiyo, ni kutumia demokrasia komavu iliyomo ndani ya CCM ya kuwaruhusu wanachama wake kugombea, nafasi waipendayo.

 

‘’Unajua CCM ni ndio mwalimu wa vyama vingine kidemokrasia, na hili ndilo lililonivutia, kuona nimtumie haki yangu ya kuomba kuchaguliwa hapo baadae,’’alifafanua.

 

Akizungumzia vipaumbele vyake, pindi vikao vya chama vikirejesha jina lake na kugombea nafasi hiyo ya uwakilishi wa Jimbo la Chonga na kushinda kwenye uchaguzi mkuu, ni pamoja na elimu, afya na huduma za kijamii.

 

Kuhusu ikiwa anauzoefu kwenye uongozi, mtia nia huyo kwa nafasi ya uwakilishi, Ahmed Abubakar Mohamed, alisema alianzia akiwa skuli ya sekondari na kisha kua rais ngazi vya vyuo vikuu Tanzania.

 

Alisema, eneo jingine ni kushika nafasi ya utumishi wa umma kama vile PBZ na kuwa Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kwa miaka mitano sasa.

 

‘’Mimi kwenye uzoefu wa kuongoza sina shaka, nimeshakuwa mzoefu na ndio maana, kama vikao vya chama vitarejesha jina langu na kisha kushinda, sina hofu kuongoza jimbo,’’alisema.

 

Hata hivyo, alisema pamoja na kwamba hii ni mara yake ya tatu kugombea nafasi hiyo, lakini ataheshimu na kuthamini mno uamuzi wowote wa chama juu yake, kwani kipaumbele chake ni chama, kisha uongozi.

 

Nae mtia nafasi kwa nafasi ya ubunge jimbo la Chake chake Ashura Abdalla Simai, alisema ana nia hiyo, ili kuona anataka kwenda bungeni kuwatetea wanawake.

 

‘’Wanawake wamekuwa wakikosa mtetezi kwa kina, kwa mambo yanayotuhusu, hivyo nimechukua fomu, kujaribu bahati yangu kwa mara nyingine,’’alisema.

 

Kwa upande wake mtia nia nafasi ya ubunge jimbo la Ziwani Othman Kassim Juma, alisema sababu za kuchukua fomu hiyo, ni kutaka kulikomboa jimbo hilo.

 




Hata hivyo mtia nia kwa nafasi ya ubunge jimbo la Chake chake Issa Mohamed Kassim ‘mzee wa nyungu’ alisema kwa sasa, hana cha kuwaambia wananchi, kama uamuzi wa chama haujafanyika.

 

‘’Mimi ni mwanaccm damu, sihofii kutorejeshwa kwa jina langu, maana maamuzi ya chama iwe ni ya halmashauri kuu au kamati kuu, naayamini na nayaheshimu, kwa dhati ya moyo wangu,’’alisema.

 

Mapema mtia nafasi kwa nafasi ya viti maalum kwa watu wenye ulemavu, Awena Khamis Rashid, alisema kundi hilo linamuhitaji yeye kwa ajili ya kulikomboa.

 

‘’Nimeona watu wenye ulemavu hawajapata mtetezi, na ndio maana nimetumia haki yangu ya kikatiba kupitia chama changu cha CCM, ili kuomba kuteuliwa,’’alifafanua.’

 

Aidha mtia nia kwa nafasi ya ubunge jimbo la Ole Burhan Khamis Juma, alisema kilichomvuta kuchukua nafasi hiyo, ni kutaka kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kazi.

 


Awali Katibu wa CCM wilaya ya Chake chake, Nicholaus Samson Chibwana, alisema kwa jana waliwapokea na kuwapa fomu watia nia 12 kwa nafasi ya ubunge 12 na wanne kwa nafasi ya uwakilishi.

 

Alisema, hio ni kuonesha kuwa, CCM imepevuka kidemokrasia, kwa wanachama wake kuitumia haki yao nyingine, na sio ile walioizea ya kuchagua pekee.

 

Zoezi la uchukuaji fomu kwa nafasi za unbunge, uwakilishi na viti maalum, lilianza juzi Juni 28, likitarajiwa kumalizika Julai 2 mwaka huu.

                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...