Skip to main content

MJANE WA WATOTO SABA AOMBA MSAADA PEMBA

 


NA FATMA HAMAD, PEMBA@@@@

MJANE mwenye watoto saba amewaomba wahisani na watu wenye uwezo, kumpa msaada wa bati na miti, kwa ajili ya kuezekea nyumba yake, ili apate kustirika na watoto wake.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi nyumbani kwake kijiji cha Madenjani Wilaya ya Wete Pemba, leo Juni 12, 2025 mama huyo Rehema Salum,  alisema nyumba anayokaa imeshakua mbovu, mvua yote inamnyeshea ndani mwake.

Alisema anapatashida kwani mvua inaponyesha husimama barazani hata kama ni usiku mkubwa,kwa vile ndani hujaa maji na kukosa sehemu salama.

‘’Ndani hujaa maji, vitanda vyangu vyote vimeshaharibika sina hata pakulala na watoto wangu saba, naomba binadamu wezangu munisaidie nateseka,’’alilalamika.

Alieleza tayari alishajenga vyumba viwili vya matufali, ingawa ameshindwa kuezeka, hivyo ameomba asaidiwe bati pamoja na miti kwa ajili ya kuezekea, ili apate kuishi sehemu anapostahiki  binadamu.

Alifahamisha kuwa mume wake amemuacha na watoto saba, na kumuachia mzigo wa malezi, na kwa sasa hamuulizi huduma ya aina yoyote kwa watoto wao.

Alisema amesharipoti maeneo mbalimbali ikiwemo ustawi wa jamii wilaya ya Wete pamoja wizara ya Maendeleo ya Jamii, ingawa hakuna hatua aliyochukuliwa.

Katika hatua nyingine, alimuomba sheha wa shehia  kumuingiza katika miradi ya maendelo ambayo inakuja, ili iweze kuwasaidia kumoa uhakika wa chakula.

Mtoto wa mjane huyo, Bilali Mohamed Rashid (16)  anaesoma darasa la kumi, anasema ndoto zake za baadae ni kuwa waziri wa Fedha.

Alifahamisha kuwa, kitendo cha kukosa huduma kutoka kwa baba yao kinamuathiri, kwani wanashindwa kupata huduma wanazotakiwa, kutoka kwa wazazi wao, ndio maana anasoma kwa bidii.

‘’Tunakwenda skuli hatuna viatu mvua kama hizi, hatuli chochote, na tukirudi tunakuta hamna kitu, kwakweli hilo linaniathiri na linaweza kupelekea kushindwa kutimiza ndoto zangu,’’alifafanua.

Nae Nasra Mohamed Rashid ambae anasoma darasa la pili  amesema ipo haja serikali, kuweka adhabu kali kwa wazazi pindi wakizitekeleza familia zao.



Baba mzazi huyo ambae ni mstaafu wa JWTZ, Mohamed Rashid alipopigiwa simu na mwandishi wa habari alisema, sio kwasababu hataki kuwahudumia watoto wake, bali ni kutokana na halingumu ya maisha yake.

‘’Ni kweli mstaafu, ingawa ninachokipata, hakitoshelizi kukigawa nyumba mbili, inafaa kama hawa watoto atanirejeshea nipate kuwahudumia kwa chungu kimoja,’’alisema.

Mwana harakati wa kulinda na kutetea haki za watoto Pemba Tatu Abdalla Msellem alisema kuvunjika kwa ndoa isiwe sababu ya kila mzazi kufumbia macho wajibu wake wa malezi na huduma kwa watoto.

Sheikh Said Ahmed Mohamed  kutoka Ofisi ya Mufti Pemba, anasema kisheria mwanamme ndie mwenye jukumu la kutoa matunzo kwa familia yake, hata baada ya kuvunjika kwa ndoa.

Kiongozi wa Kanisa Katoliki lililopo Mkungu Malofa Chakechake Robert Miguwa Ndalami, anasema dini imeelekeza wanaume watoe huduma stahiki kwa familia zao akiwemo mama na watoto.

Ripoti ya Wizara ya Kazi, Uezeshaji, Wazee na Watoto, kwa sasa wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto ya mwaka 2017/2018, imeeleza kua, kesi 534 za utelekezaji watoto zimeripotiwa Zanzibar.

Ambapo kesi 412 ni kwa upande wa Unguja na 122 kwa Upande wa Pemba, hata hivyo ripoti hiyo haijaweka wazi sababu rasmi za utelekezaji huo.

MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...