Skip to main content

PACSO: ‘TUNATEKELEZA KWA VITENDO MAONO YA DK. MWINYI, DK. SAMIA’

 


 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MRATIBU wa miradi kutoka Mwenvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, alisema wanatekeleza kwa vitendo, maono ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, la kuhakikisha elimu ya uraia na demomkrasia inawafikia wananchi.

Mratibu huyo aliyasema hayo, wakati akizungumza na watendaji wa serikali na wanaasasi za kiraia, katika kongamano la pamoja, la kujenga ushirikiano, baina pande mbili hizo, kupitia mradi wa ‘uraia wetu’ lililofanyika Wawi Chake chake.

Alisema, mradi huo ni tokeo moja wapo la maono ya viongozi hao, ambapo wameamua kuwakusanya watendaji wa serikali na wale wa asasi za kiraia, ili kuibua changamoto zinazokwamisha ushirikiano wao.

Alieleza kuwa, washiriki wa kongamanio hilo, watapata nafasi ya kuelezea changamoto zao kikanuni, sera na kisheria ili kuona zinatatuliwaje kwa umoja wao.

‘’Sote ni mashahidi kuwa, wakati viongozi wetu wanaingia madarakani, walihimiza mno suala la kuzifahamu sheria, kuona changamoto zake na hata kuzifanyia marekebisho, ili kusiwe na mkwamo katika utekelezaji wa shughuli husika,’’alieleza.

Aidha Mratibu huyo wa miradi kutoka ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, alieleza kuwa washiriki watachambua sera, kanuni na sheria ambazo wakati wanapotekeleza majukumu yao, zinawakwaza.




Katika hatua nyingine alifafanua kuwa, PACSO imeandaa jukwaa la kuwakutanisha pamoja watendaji wa serikali na wanaasasi za kiraia, ili kujadili kwa pamoja changamoto za watu wenye ulemavu, vijana na wanawake.

Alieleza kuwa, maoni ambayo yatapatikana katika kongamano hilo, watayaandika vyema na kuyasilisha kwa Jumuiya ya wanawake wanawake wenye ulemavu Zanzibar, ambao nao watakeleza mradi kama huo, ngazi ya kitaifa.

‘’Kwenye mradi huu PASCO, inatekeleza ngazi ya kanda (zone), ingawa wenzetu wa JUWAUZA wanatekeleza ngazi ya kitaifa na kisha maoni hayo, watayafikisha kwa viongozi wa kitaifa,’’alieleza.

Akifungua kongamanio hilo, Msaidizi Naibu Mrajisi wa Asasi za Kiraia Pemba, Saada Abubakar Khamis, alisema mradi huo, unaweza kuleta tija, kwa vile unaangalia kwa upana wake, suala la demokrasia.





Alieleza kuwa, moja ya chanagamoto iliyopo ni kutoonekana kwa uhusiano mzuri, baina ya asasi za kiraia na serikali kuu, jambo ambalo wakati mwengine huchelewa kutekelezwa kwa miradi.

‘’Jambo hili lililofanywa na wenzetu ‘PACSO’ naamini litazidisha ushirikiano na uhusiano mzuri uliopo baina ya serikali na asasi za kiraia, hasa kwa vile pia litaangalia sheria na kanuni zinazokwamisha utendaji wa asasi,’’alifafanua.

Alifafanua kuwa, demokrasia ni dhana pana na wakati mwengine wapo wanaoona inahusu ngazi za juu pekee, bila ya kuona kuwa dhana hiyo, hutakiwa kuonekana hata kwenye asasi za kiraia.

Wakichangia kwenye kongamano hilo, washiriki hao walisema ushirikishwaji ni jambo jema, katika kufikia uamuzi wowote, katika nchi ama asasi za kiraia.

Afisa wa watu wenye ulemavu wilaya ya Chake chake Mwadini Ali Juma, alisema bado watu wenye ulemavu, hawajatendewa haki sana katika ajira, miundombinu na majengo ya umma.




Mwakilishi kutoka TAMWA, Asha Mussa Omar, alisema kikwazo kilichopo ni kwa jamii, kutotaka kubadili mitazamo, juu ya dhana ya mwanamke na uongozi.

‘’Wapo baadhi ya watu wanawavunja moyo wanawake, kwa kuwaambia kuwa wakiwa viongozi, watakuwa wamevunja maadili, watapewa takala, dhana hizi zinahitaji elimu kwa bidii,’’alieleza.

Akiwasilisha mada ya umuhimuwa ushirikiano baina ya asasi za kiraia na serikali, mkufunzi Juma Bakar Alawi, alisema hakuna haja ya pande mbili hizo, kunyimana taarifa.






Alieleza kuwa, asasia zote za kiraia Zanzibar, zinatekeleza miradi ambayo ni maono ya serikali kuu, hivyo ni vyema pande moja wapo inapohitaji taarifa, iwe rahisi kupeana.

Kongamano hilo la siku moja, kupitia mradi wa ‘uraia wangu’ limeandaliwa na kufadhiliwa na The Foundation for Civil Society kupitia Umoja wa nchi za Ulaya.

Mwisho    

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch