Skip to main content

HIZI HAPA SABABU ZA KUNAWIRI MATUKIO YA UDHALILISHAJI, MOJA KUKIMBIA WATUHUMIWA

 

  NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@

UDHALILISHAJI ni kile kitendo ambacho hufanyiwa mtu yoyote bila ya ridhaa yake.

 

Na wakati mwingine kitendo hicho, kikashusha hadhi, thamani, utu, kuvurugika kwa ajili, kimwili, kijamii na hata kiuchumi kwa mtendewa.

 

Katika ulimwengu wetu wa sasa, kesi za udhalilishaji zimezidi kushamiri kila siku zikenda mbele, watuhumiwa wanaongezeka mitaani kwa kila leo. 

 

Tatizo kubwa linalowakumba wanajamii ni kuoneana muhali kutokana na watendaji wa matukio hayo aidha ni watu wa karibu na familia, hivyo ikigundulika  kua ni baba au mjomba aliebaka basi kesi  inamalizwa kifamilia.

 

Haya si matukio mapya masikioni mwetu, ambayo yanafanyika na badala yake watuhumiwa wanakimbia na kupelekea waathirika kushindwa kupata haki yao.

 

 WALIOPATA UKATILI WA UDHALILISHAJI WA KUBAKWA 

Kwa mujibu wa mama mzazi wa Halima Juma (si jina lake halisi) mkaazi wa kijiji cha Kidemeni wilaya ya Chake Chake, alisikitishwa kutokana na tukio kama hilo, ambalo amelipata mwanawe, kwa kufanyiwa na baba yake mzazi.

 

Akizungumza na mwandishi wa makala hii, anasema, alipata mitihani huo kwa mwanawe mwenye umri wa miaka 22, ambae alikua akifanya kazi kwenye ofisi ya mjomba wake.

 

Ingawa baadea mjomba wake kujua kama amefanyiwa udhalilishaji na kapata ujauzito, aliamua kumfukuza kazini hapo.

 

"Ndio nilifanyiwa na baba yangu mzazi na alikua akinipa vitisho vya kutaka kuniuwa, akawa ananambia nimeweza kukuzaa kwa hiyo na kukuua naweza, hivyo ukija ukimwambia mamako au mtu yoyote nakuua," alieleza huku akifuta machozi.

 

Anaeleza kuwam kutokana na kutishwa huko, aliendelea kunyamanza hadi alipopata ujauzito, ndipo ilipogundulika na hasa baada ya kuhojiwa.

 

Baada ya kujulikana kuwa ni mjamzito, baba yake alikimbia na yeye alifukuzwa kazi na mjomba wake, kwa madai ya kushindwa kutoa taarifa mapema ya udhalilishaji aliokuwa anafanyiwa.

 

“Baada ya yote kutokea, mzazi wangu alikimbia na kutuacha pekeyetu, na hata kule nilipokuwa nafanyia kazi, nilifukuzwa eti kwa sababu sikusema mapema niliyokuwa nafanyiwa,” anaeleza.

 

Kwa upande wake mama mzazi wa kijana huyo, anasema aliumia kutoka na madhila aliyoyapata mwanawe, baada ya kusikia kuwa baba yake ndiye mhusika wa ujauzito huo.

 

‘’Niliumia sana kitendo hiki na hasa kufanyiwa na baba yake, ambae amemzaa, maana nilitarajia awe mlinzi wa kweli na mwadilifu kwa mtoto wetu, leo amemvunjia ndoto na maisha yake,’’anasema.

 

Alifuatilia sana kesi hiyo, kwa muda mrefu lakini alivyoona hakuna matumaini ya mtoto wangu kupata hake, kisha nilikata tamaa na kuendelea na shughuli zangu nyingine,’’anasimulia.

 

Sasa anasema ni kazi ya serikali kuu, kuongeza nguvu na kuwasaidia waathirika kuwafuatilia watuhumiwa wa kesi hizo wanaokimbia, ili wakamatwe na kurejeshwa kwa lengo la kuwezesha haki kupatikana.

 

Anaona kuendelea kwa utamaduni wa muhali katika jamii, inachangia kwa kiasi kikubwa kesi hizo, kushindwa kufikia hatua nzuri kutokana na watu kufichiana maovu.

 

"Tatizo letu kubwa bado tunaoneana muhali na tuna uwelewa mdogo juu ya suala kama hili, tunalichikulia kama kawaida tu, kwasababu mbakaji anatoka ndani ya familia japokua watoto wetu wanaathirika kiakili na kimwili,” alieleza.

 

KUTOKA MAHAKAMANI

 Kwamujibu wa Mrajisi kutoka mahakama maalum Chake Chake, Faraji Shomar Juma, anasema kwa miaka ya karibuni, hakujawahi kupelekwa kesi kama hizo na itatokea mtuhumiwa akitoroka, kiupande wao kesi hawaifuti.

 

"Hukumu nyingi za watuhumiwa kutoroka zipo kwasababu wanahusika huwatafuta na wakiwapata huwarudisha mahakamani ili kusomewa adhabu yake ili wakatumikie vifungo vyao,” anaeleza.

 

Aliitaka jamii kuripoti kwa wakati tukio linapotokea, ili kudhibiti watuhumiwa kukimbia na kuwezesha kuchukuliwa hatua kabla ya kukimbia.

 

KUTOKA AFISI YA MKURUGENZI WA MASHTAKA

Mwendesha mashtaka wa ofisi hiyo, Ali Amour Makame anasema kwa mwaka 2022, kesi kama hiyo ilitokea moja (1), ambayo mtuhumia alitoroka ndani ya mikono ya Jeshi ka Polisi, baada ya kufika katika kituo cha Polisi Chake chake.

 

Anasema kesi kama hizo, zinakwamisha wahanga na kujikuta wapo katika kipindi kigumu cha maisha na wengine hata kuamua maamuzi mabaya katika maisha yao.

 

‘’Kwa ujumla kesi ambazo zimefika mahakamani, ikiwa zimesomwa na kupatiwa hukumu, mwaka jana zilikua 40, na mwaka huu wa 2023 hadi sasa zimefika kesi 48, ingawa hizi za kutoroka mwaka huu hatujapata hata moja,’’anaweka wazi.

 

WANAHARAKATI WA HAKI ZA WANAWAKE NA WATOTO

Nae Mkurugenzi mtendaji wa Jumuia ya TUMAINI JIPYA Tatu Abdalla Msellem anasema wameweka mfumo wa kutoa taaluma kwa jamii, kwa sababu bado ina uwelewa mdogo kuhusiana na mambo ya udhalilishaji.

 


Wametshatoa taaluma katika sheihia mbali mbali kwenye mkoa wa Kusini na Kaskazini Pemba, ingawa hawajawahi kupokea kesi ya mtuhumiwa kutoroka. 

 

Alisema ikiwa taasisi yake inatimiza miaka mine ya kushughulikia kesi hizo katika wilaya ya chake chake, mkoa wa wakusini Pemba wamepata shehia 14 na kwa upande wa mko wa kaskazini wilaya ya Micheweni wamepata shehia nne, ambazo wamefikisha taaluma hiyo.

 

Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema jamii kama haijaamua kwa vitendo, wadhalilishaji wataendelea kukosekana kila siku.

 



‘’Zipo baadhi ya familia, mara linapotokezea tukio huanza kukaa chini pamoja kutafuta sulhu, na ikishindikana wanakimbilia Polisi na mtuhumiwa anapa mwanya wa kukimbia,’’anasema.

 

Wamekuwa na miradi mbali mbali ikiwemo ya kuwawezesha waandishi wa habari, namna bora ya kuandika habari hizo kwa ufanisi, jamii ipate kujua njia za kupunguza matendo hayo,’’anaeleza.

 

Akaligeukia Jeshi la Polisi kuzidisha kasi ya ufuatiliaji wa matukio hayo, ili jamii ipate kuwaamini na kuona ni sehemu salama ya kukimbilia, yanapotokezea matendo hayo.

 

‘’Tunachoomba kwa jamii na vyombo vya sheria, ni kuzidisha ushirikiano na TAMWA, ili kile ambacho tunakifanyaka kama kuiunga mkono serikali kuu, kifanikiwe,’’anasema.

 

Mratibu wa Jumuia kwa ajili ya watu wenye Ulemavu wa akili Zanzibar ZAPDD, ofisi ya Pemba Khalfan Amour Mohamed, anasema mzigo wa udhalilishaji na kisha watuhumiwa kukimbia, zaidi huwaathiri ambao ni walemavu wa akili.

 

‘’Hata familia inapotokezea aliyedhalilishawa ni binaadamu mwenye ulemavu wa akili, ushughulikiaji wa kesi hiyo, huwa hafifu na hata ikifikishwa mbele ya vyombo vya sheria, mwisho wa siku hufutwa,’’anasema.

 

Mratibu wa Baraza la taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar ofisi ya Pemba Mashavu Juma Mabarouk, anasema athari ya wadhalilishaji kukimbia, lazima itafutiwe suluhisho la kudumu.

 

KUTOKA KITENGO CHA MKONO KWA MKONO

Afisa mshauri kutoka Wizara ya Afya Hospitali ya Chakechake katika kitengo chamkono kwa mkono, Tatu Abass Machano anasema kesi nyingi zinazohusu familia zinazoripotiwa kituoni hapo, zinafika kwa kuchelewa na kupelekea ushahidi kupotea.

 

‘’Kwa mfano mtoto kabakwa tangu Oktoba 3, wazazi watuleta baada ya siku10 au kuzidi, wanakua kwanza wakijishauri nini wafanye na hata wakija kwetu, zile alama za muda ule alofanyiwa lile tendo hazipo tena, jambo linalokwamisha upatikanaji wa ushahidi,”anasema.

 

Ndio maana anaiomba serikali na wadau wingine, kuendelea kutoa taaluma kwa jamii, kupitia makundi mbali mbali, ili ielewe umuhimu wa kuripoti kwa wakati matukio ya udhalilishaji.

 

 MWALIMU WA MDRASSA

 Mwalimu mkuu wa Madrassatu Nurul -Huda iliopo kijiji cha Mjengo wa banda shehia ya Wawi, Omar Mohamed Omar, anasema bado jamii inashindwa kulitatua suala hili, kwa sababu wao wanalichukulia kawaida.

 

‘’Kutokana na visa kama hivi, sisi walimu wa Madrassa tunaziomba taasisi zote kuongeza juhudi ya kutoa elimu kwa umma, ili kukomesha vitendo vya udhalilishaji wa watoto,”anafafanua.

 


Hivyo basi serikali ihusishe mashirika mbalimbali nayo yaweze kuendelea kutoa elimu juu yasuala hili kwani baadhi ya matukio ya udhalilishaji, huhusishwa na imani za kishirikina.

 

VISA NA MIKASA YA UDHALILISHAJI

Khamis Ali Diri wa Ukunda shehia ya Kengeja wilaya ya Mkoani, hadi sasa anatafutwa na Jeshi la Polisi, kwa tuhma za kumpa ujauzito mmoja wa shemegi yake ambae ni mwanafunzi wa darasa la nne.

 

Haji Mjaka Hashim wa Wawi, sasa anatimiza miaka minne, akiwa hajarudi kwao, tokea alipodaiwa kufanya tukio la udhalilishaji kwa mtoto mwenye ulemavu mchanganyiko kijijini hapo.

 

Hassan Iddi Othman na wenzake wawili nao kwa sasa wanatafuta na Jeshi la Polisi baada ya kudaiwa kubaka kwa kundi, eneo la Wesha miaka miwili iliyopita.

 

Ingawa Mossi Othman Mossi wa shehia ya Mchakwe Mwambe wilaya ya Mkoani, baada ya kikumbia kwa mwaka mmoja, hivi karibuni alikamatwa na Jeshi la Polisi, na kufikishwa mahakamani akikabiliwa na tuhma za kumpa ujauzito mara mbili shemegi yake.

 

MWISHO.

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch