Skip to main content

WAALIMU, WANAFUNZI WESHA WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI MAPAMBANO DHIDI YA UDHALILISHAJI

 



NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@

WAALIMU na wanafunzi wa skuli ya msingi ya Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, wamesahauriwa kuongeza juhudi za kupambana na vitendo vya udhalilishaji, ili wanawake na watoto wabaki salama kwa vitendo hivyo.

 

Hayo yameelezwa na Mshauri nasaha kutoka kitengo cha mkono kwa mkono cha hospitali ya Chake chake Asha Massoud, wakati akitoa mafunzo kwa wanafunzi hao, juu ya dhana ya kupambana na udhalilishaji, mafunzo yaliyofanyika skulini hapo.

 

Alisema kuwa, kupitia mafunzo anaamini wanafunzi na waalimu hao, wameshapata njia sahihi ya kuongeza juhudi za mapambano dhidi ya udhalilishaji.

 

Alieleza kuwa, kila mmoja na kwa nafasi yake, anatakiwa kukemea na kutoa elimu ya kujikinga na masuala la udhalilishaji, ili jamii na hasa kundi la wanawake na Watoto libaki salama.

 


‘’Kwanza niwatake waalimu na wanafunzi wa skuli hii ya Msingi Wesha, kuhakikisha wanaongeza makali ya kukemea na kutoa taarifa wanapoona viashiria vya udhalilishaji kwa mmoja wao,’’alifafanua.

 

Akizungumzia mbinu zinazotumiwa na wadhalilishaji na hasa kwa waatoto Mshauri nasaha huyo, alisema moja wapo ni kupewa zawadi mfano wa pesa au pipi.

 

Alifahamisha kuwa,  mwanafunzi yoyote asikubali kuitwa na mtu amsiyemjua na kukubali kupokea pesa au kitu chochote, kwani kufanya hivyo ni kuwakaribisha wahalifu hao.

 

 "Kitendo cha udhalilishaji, kwa miaka hii hakifanywi na mtu wa mbali, bali ni wale wazazi na walezi au wakati mwengine hata majirani, lakini wote hawa wakianza ishara ni vyema mkatoa taarifa,"alisema.

 



Wakati huo huo, Mshauri huyo nasaha kutok kitengo cha Mkono kwa mkono cha Hospitali ya Chake chake Asha Massoud, amewasisitiza wanafunzi hao, kuacha kuitana majina mabaya au kupigana, kwani vitendo hivyo ni sehemu ya udhalilishaji.

 

Nae Afisa Mshauri kutoka kitengo cha mkono kwa mkono cha hospitali ya Chake chake,Tatu Abass, alisema moja ya madhara makubwa kwa mtoto aliyefanyiwa vitendo vya udhalilishaji ni kukosa elimu, kupoteza afya yake na kukosa hamu ya kujiendeleza.

 



Hata hivyo, amewakumbusha Watoto wa kike, kujilinda na athari za mimba za umri mdogo, kwani athari yake moja kubwa ni kupoteza uhai, kutoakana na viungo vyake vya uzazi kutokuwa tayari kuhimili vishindo vya mimba.

 

"Mtu yeyote aliyefanyiwa udhalilishaji, anaweza kupata maradhi mbali mbali, mfano ukimwi, kwani anayemfanyia huwa hujui afya yake,’’alifafanua.

 

 Kwa upande Mshauri nasaha kutoka kitendo hichi hicho, Kurthumu Khamiss Msabaha, alisema kua kuna njia mbali mbali za kujikinga na udhalilishaji, ikiwemo kutokutumia simu ukiwa bado ni mwanafunzi na kuzurura ovyo ovyo katika maeneo mbali mbali.

 

Nae Polisi kutoka dawati la jinsia la wanawake na watoto katika kituo cha Polisi Chake chake Salama Omar, aliwataka wanafunzi, kuendelea kutoa taarifa wanapoona wanataka kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji.

 

"Musimuamini mtu yoyote ambae humjui undani wake, kwani itapelekea kuja kukufanyiwa kitendo kibaya, ambacho hujakitarajia katika Maisha yako, nakukuvunjia malengo yako," alieleza.

 

Kwa upande wake Mwalimu mkuu wa skuli hiyo Mafunda Sudi Sabur, alikishukuru kitengo hicho kwakuwapa mafunzo hayo na kuahidi kuyafanyiakazi kwa wengine, ili elimu hiyo isambae.

 

Hata hivyo aliwawambia wanafunzi wake, wawe mabalozi kwa wenzao, ambao hawapo katika mafunzo hayo, ili kuona kila mmoja amepata uwelewa.

 

                            Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch