Skip to main content

UKIMNYA UNAVYOWAATHIRI WATOTO KISAIKOLOJIA WALIOFANYIWA UDHALILISHJAJI

  



NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@

MOJA ya jambo muhimu ambali wazazi na walezi waliowengi ambalo hawalifanyi hasa kwa miaka ya siku hizi, ni kukosa kuwa karibu na watoto wao.

Ni tofauti kabisa na karne zilizopita, ambapo wazazi na walezi hao walitenga muda kukaa na watoto wao, kama sio wajukuu na kuwapa maelekezo ya hatma ya maisha yao.

Wapo walikuwa wakithubutu kuwapa hadithi za mafundisho, namna bora ya kukabiliana na maisha na au wakati mwengine hata jinsi ya kupambana na adui.

 Kwa karne ya sasa wazazi hujifanya hawana nafasi hiyo, wengi wakisingizia ugumu wa maisha, na hao wachache wanaokanaa nao, hukosa kuwapa dunia ilipofikia.

Ndio maana mwanaharakati wa masuala ya kupinga ukatili na udhalilishaji Aisha Muhidin Juma wa Fuwoni, anasema kwa kule wazazi kukosa nafasi hiyo, husababisha watoto kuwa wapweke.

Kisha kinachofauta anasema ni kugubikwa na madhara makubwa kwa watoto hao, tena hasa ikiwa wameshafanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji.

Anaona wapo wazazi wamekuwa wakali kipitiliza, iwe tayari wameshagundua udhalilishaji kwa mtoto wake, au wakati anataka kugundua jambo hilo.

Hali hii inatokea kuwepo kwa ukimnya, ambao huibua madhara mengi kwa mtoto huyo, ikiwemo madhara ya kisaikolajia pamoja na kukosa haki ya sheria.

Je, unatambua madhara ya kisaikolojia ni nini?

Ni ile hali inayojulikana na mawazo yasiyo ya kawaida, hisia, na tabia hali hii humkumba mtoto na kusababishia kupata ugonjwa wa akili ikiwemo wasiwasi.

Watoto, wa kike kwa kiume, wa umri hadi wa balehe, wanachezewa sehemu zao za siri, wanabakwa, kulawitiwa na kutelekezwa kiasi cha kuzusha tatizo kubwa zaidi la umasikini na unyimaji wa haki zao za msingi.

Bint Chausiku sio jina  halisi mwenye umri wa miaka 22, sasa hivi, akiwa kidato cha tatu, alifanyiwa kitendo cha udhalilishaji na mjomba wake.

Anasimulia kuwa, tukio hilo lilitokea mwaka 2012, na kwa wakati huo anasema hakuweza kumueleza mtu yoyote nyumbani kwao, kwasababu ilikuwa naogopa.

Anasema mjombo wake huyo, alikuwa na tabia ya kwenda chumbani kwake, kwa mtindo wa kunyatia nyatia, na kuanza kumshishika shika sehemu zake za siri.

Wakati mwengine alikuwa akishtuka na kisha mjombo wake huyo, huanza kujisogeza pembeni, huku yeye machozi yakiwa yanamtoka kwa kuumia kufanyiwa kitendo hicho.

"Alikuwa haji siku zote, bali alikuwa anatenga muda nisahau na kunisogelea siku nyingine, ilikuwa ni kawaida yake kipindi chote hicho hadi mama yangu alivyo aga dunia mwaka 2017,’’anasimulia.

Sababu iliyopelekea kushindwa kutoa taarifa, ni kwasababu mama yake alikuwa ni mgonjwa wa figo, hivyo alihofia kumzidishia maumivu mingine.

Lakini hata familia yao, anasema ilikuwa na thamani ndogo mno kwa marehemu mama yake, hivyo alijiona ni mtu wa kuteseka kila siku katika maisha yake.

Bint huyo anaeleza athari alizozipata, ikiwemo kukumbuka mara kwa mara, kupatwa na hasira, kulia pamoja na kumchukia mjomba wake huyo hadi watoto wake.

"Na tukiwa tunapewa elimu kuhusina na matendo ya udhalilishaji katika makongamo yoyote ikiwemo skuli, hua nakuwa mnyonge na kujilaumu katika nafsi yangu, na kujificha mtu asijenigundua kua na mimi nishawahi kufanyia vitendo vya udhalilishaji,’’anasema,

Naye Mkuu wa Division ya Afya ya Akili wa Kidonge Chekundu Khadija Abdulrahmani Omar, anasema mtoto ambae amefanyiwa vitendo vya udhalilishaji kwa muda mrefu, bila ya tukio kuripotiwa anatakiwa kupata tiba ya afya ya akili.



“Mtu yoyote atakaefanyiwa vitendo vya udhalilishaji, anapata athari mbali mbali ikiwemo utumiaji wa dawa za kulevya, kukumbuka mara kwa mara na hasa akisikia matukio hayo kutokea, kuchukia wanaume wote,’’anaeleza.

Anasema haijalishi, hata kama mtoto alikosa kutoa taarifa kwa wakati kutokana na ukimnya wake, anaweza kupatiwa matibabu ya afya ya akili, na kurudi katika hali yake ya kawaida.

"Kituo chetu cha Mkono kwa Mkono, wapo wataalamu wa saikolojia ambao wanasaidia kuwapatia huduma ya afya ya akili, wahanga ambao wameathirika kisaikolojia na huduma hizi zipo za aina tatu ikiwemo tiba ya biolojia, sykolojia na ustawi wa jamii,’’anasema.

"Tiba ya biolojia ikiwa mtu amepata wasiwasi kutokana na tatizo hilo, anapewa dawa na kuenda kutumia, sykolojia itamsaidia kuondoa zile hisia, ambazo zinamjia  ikiwemo kujiona hana thamani kwa jamii,’’anasema.

Wameshapokwa matokeo 11, ambayo yametokea kwa muda mrefu na kwa sasa wahanga hao, wanapatiwa huduma katika kituo cha Kidonge Chekundu.

"Watoto saba, wasichana wa nne chini ya umri wa miaka18 na wa watatu wavulana chini ya umri wa 15 ndio walifanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji, kwa miezi sıta iliyopita,’’anafafanua.

Pamoja na wanawake wanne chini ya umri wa miaka 35, hawa wamefanyiwa miaka 10 iliyopita, na sasa hupata matibabu katika hospitalni hapo.

Aidha aliwasaa wazazi kuwapeleka wahanga  katika vituo vya afya ya akili, kwa ajili ya kupata matibabu kwani wanapochelewa humsababishia maradhi ya afya ya akili .



Sheha wa shehia ya Urusi Yussuf Juma Mtumwa, ansema wapo wahanga, ambao wanafanyiwa vitendendo vya udhalilishaji na kuchelewa kuripotiwa na kupelekea wahanga hao kuathirika kisaikolojia.

"Ni kweli matukio ya udhalilishaji yapo katika wilaya zetu, na wahanga wanashindwa kutoa tarifa na kupelekea kuathirika kisaikolojia, ikiwemo kujitenga na makundi ya watu,’’anafafanua.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Mtakwimu mkuu wa serikali, iliyotolewa na afisa wao, Asha Mussa Mahafudhi, anasema kwa mwaka huu pekee ya 2023, tayari kumseharipotiwa matukio  1,421.

Ambapo hii ni tofautai na mwaka jana, ambapo kulikuwa na matukio 1,361 yalioripotiwa, na wengine wa wathirika hao ni watoto sawa na  asilimia 84.4, wanawake asilimia 11.4 na wanaume ni asilimia 4.2.

Wilaya ya Magharib ‘A’ iliongoza kwa kuwa na matukio 328 ikifuatiwa na wilaya ya Mjini, iliyoripoti matukio 322 na wilaya ya Magharibi ‘B’ matukio 294.

Katika matukio yote 1,421 ya udhalilishaji yaliotokea mwaka huu, matukio ya ubakaji yaliongoza kwa kuripotiwa 682, ambapo  wanawake chini ya umri wa miaka 35 walikua 65 na wasichana chini ya miaka 18, yalikuwa 619.

Ingawa kwa upande wa makosa ya shambulio la ilikuwa 267 sawa na asilimia 18.8, huku wanawake chini ya miaka 35, yakiripotiwa 54 wasichana yalikuwa matukio 79, wavula chini ya miaka 15, yaliripotiwa 85, huku wanaume yalikuwa matukio 49 kwa wale chinia ya umri kunzia miaka 18.

Mkurugezi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Siti Abasi Ali, anasema kuna umuhimu wa kuwapatia elimu ya kisaikolojia wahanga, waliofanyiwa vitendo vya udhalilishaji.

Hii anaona itawaweka sawa na kusaidia kwa kiasi ikukubwa afya yao ya akili na kuacha kijitenga wenyewe, kw akule kufikiria ukubwa na tatizo lililowakuta.

Hata hivyo, anasema serikali imeweka waalimu maalum katika skuli zote, kwa ajili ya kutoa huduma ya kwanza ya elimu ya saikolojia, pindi wanafunzi wakikumbwa na ukatili.

Hapa akawageukia wazazi na walezi, kuwa karibu na watoto wao kwa lengo la kuweza kujua changamoto mbali mbali anayopitia mtoto huyo.

“Baadhi ya wazazi wanakuwa wakali hadi mtoto anamuogopa na kushindwa kumueleza kitu chochote, ambacho amekumbana nacho," anasema.

Mwanachi Kombo Ali Haji, anasema unapokutwa na changamoto ya afya ya akili, ni vyema kutafuta msaada kwa wataalamu, kwa ajili ya kupata ufumbuzi wa changamoto hizo.

Mzazi Aiman Juma Mlenge wa Kikwajuni anasema, kama wazazi hawakujitengea muda wa kukaa na watoto, wanaweza kuwapa wakati mgumu, hasa kwa wale waliopata shida ya ukatili na udhalilishaji.

Mkuu wa Dawati la Jinsia la watoto Inspector Mohamed Mwadini anasema kuna athari mbali mbali, zinatokea ikiwepo mtu amefanyiwa vitendo vya udhalilishaji na kukaa kiminya, ikiwemo kukosa haki yake ya msingi.

"Eneo ambalo amefanyiwa kitendo cha udhalilishaji inakua lishabadilika, kwa hiyo inakua ngumu kupata ushahidi, kupata maambukizi kwa urahisi, vilevile anaweza kuendelezwa kufanyiwa vitendo hivyo kutokana na ukiminya wake,’’anasema.

‘’Akiwahi kutoa tarifa mapema atapelekwa hospital kwa ajili ya kuangaliwa ikiwa ameshaambukizwa magonjwa ama laa, na hasa kwa vile pia zipo dawa na kumkinga na baadhi ya maradhi,’’anasema.

Elimu juu ya athari za vitendo hivi vya udhalilishaji inatakiwa itolewe kwa upana sana kwenye jamii zetu, haswa kwa wazazi kujua ni namna gani wanaweza kuwagundua watoto walio athiriwa na vitendo hivi.

Ukaribu wa wazazi kwa watoto wao, ndio nguvu kuu itakayo saidia kurudisha uhuru wa mtoto kumfikia mzazi wake na kumuelezea juu ya changamoto ambazo atakutana nazo kwa watu watakao onesha dalili zozote za udhalilishaji kwake.

                  Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch