Skip to main content

WAKULIMA WA KARAFUU KUENDELEA KUPOKEA MALIPO KUPITIA SIMU

 



NA ABDI SULEIMAN, PEMBA@@@@

MKURUGENZI wa Mfuko wa Maendeleo ya Karafuu Zanzibar Ali Suleiman Mussa amesema, kutokana na kuongezeka kwa utapeli katika jamii ni vyema wakulima wa karafuu kuendelea kutumiwa fedha zao kwenye akaunti ya TigoPesa, ili zibaki kuwa salama.

Alisema, njia hiyo itaweza kuwasaidia wakulima wa zao la karafuu, fedha zao kuendelea kuwa katika hali ya usalama muda wote na sio kuchukua mkononi, kwani inahatarisha maisha yao.

Mkurugenzi huyo aliyaeleza hayo wakati akifungua mkutano wa wakulima wa karafuu Mkoa wa Kaskazini Pemba, juu ya kuhamasisha kutumia mtandao wa simu ya Tigo Pesa katika kutumiwa malipo yao baada ya kuiuzia Serikali  karafuu zao.

Aliwataka wakulima hao katika msimu wa karafuu ulioanza Agosti 3 mwaka huu, kuhakikisha wanatumia mitandao ya simu kuweka fedha zao, huku Shirika la ZSTC likiendelea na mchakato wa kuwasajili wakulima wote.

“Kutumia mitandao katika kuhifadhi fedha ni sehemu salama, kuliko kuondoka na fedha mkononi, wengi wanakumbana na changamoto za kuungua, kuliwa na mchwa au panya ikiwa fedha hizo zimehifadhiwa majumbani na hata kutapeliwa”, alisema.

Alieleza kuwa, mkulima aliyesajiliwa anapopatwa na tatizo wanampa kipaombele cha kumshughulikia kuliko asiesajiliwa, kwa sababu aliesajiliwa anatambuliwa kwake na Shirika hilo.

Nae Mdhamini wa Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) Pemba Abdalla Ali Ussi, aliwataka wakulima kukubali kulipwa fedha zao kupitia huduma ya TigoPesa na kama kuna matatizo wasisite kutoa taarifa kwa wahusika.

Alisema, ulipaji wa fedha kwa kutumia mitandao ya simu ni rahisi, kwani mtu anapata fedha zake kwa wakati na kiwango kikubwa, hivyo ni vyema kuliunga mkono Shirika kwa mfumo huo waliouweka, kwani lengo lao ni kuhakikisha fedha zote za wakulima wao zinakuwa salma.

Aidha aliwafahamisha wakulima hao kuwa, ZSTC tayari imeshafungua vituo vyake vya ununuzi wa karafuu kwa Unguja na Pemba tokea Agosti 3 na tayari tani mbili za karafuu zimeshanunuliwa.

Kwa upande wake Meneja wa TigoPesa Zanzibar Salum Nassor Mohamed alisema, tangu kuanza kwa malipo ya wakulima wa karafuu Unguja na Pemba mwaka 2021 hadi 2023, zaidi ya wakulima 10,000 wameshapokea malipo kupitia tigoPesa na zaidi ya bilioni 40 zimepelekwa kwa wakulima hao kupitia mitandao ya simu. 

Alisema, faida ya kutumia tigopesa ni njia salama ya kuweka fedha kuliko kuchukua mkononi na ikitokea bahati mbaya ya kupoteza simu, bado fedha zao zitaendelea kuwa na usalama.

Nae Meneja wa TigoZantel kanda ya Pemba Farouk Ahmed alisema, mawakala wa kampuni hiyo watahakikisha wanakuwepo katika vituo vyote vinavyohusika na mauzo ya zao la karafuu.

Aidha aliahidi kwamba, hakutokuwepo na changamoto yeyote ya kukosekana kwa mawasiliano ya mtandao, kwani wamejipanga kuendelea kuboresha huduma hizo.

Kamanda wa ZAECA Mkoa wa Kaskazini Pemba Nassor Hassan Nassir, aliwapongeza wakulima wa karafuu kwa mashirikiano makubwa walioyatoa katika msimu uliopita na akuwataka kuendelea na msimu huu.

Mkulima wa karafuu kutoka Kisiwani kwa Binti Abeid Mohamed Salum Ali, aliwapongeza Tigo Zantel kwa mikakati yao mizuri mwaka jana, kwani aliweza kupokea fedha kwa wakati muwafaka bila ya usumbufu wowote.

Aidha alisema, changamoto kubwa ilikuwa kwenye viwango vya mikato kwani ilikuwa mikubwa sana kiasi ambacho kiliwakwaza, hivyo aliwaomba kuweka wazi suala la makato kwa wakulima.

Nae mkulima Mohamed Ali Mmaka kutoka Mtambwe, aliitka TigoZantel kuhakikisha wanawafutilia matepeli wanaotumia mitandao ya simu, ili kujuwa wanaovujisha siri za wateja wao.

MWISHO


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch