Skip to main content

PACSO YAWAONESHA NJIA YA MALEZI WAZAZI, WALEZI PEMBA

 



NA MWANDISHI WETU, PEMBA

JAMII kisiwani Pemba, imetakiwa kufahamu changamoto na viashiria vya udhalilishaji kwa watoto, ili kuwalinda na vitendo hivyo.

 

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Asasi za Kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Ali Khamis, mara baada ya kuutambulisha mradi wa kujadili changamoto zinazowakabili watoto, katika ukumbi wa kiwanda cha Makonyo Wawi Chake chake Pemba.

 

Alisema, jamii inapaswa kuwa karibu mno na watoto wao, ili kujua haraka viashiria vya kudhalilishwa, na sio kusubiri hadi janga liwakumbe.

 

Mwenyekiti huyo alieleza kuwa, hilo litakuwa rahisi ikiwa wazazi na walezi watatenga muda wa kuwa karibu na watoto wao.

 

‘’Kama tunajiona tuko na harakati nyingi za maisha na kusahau kukaa na watoto wetu, wanaweza kukumbwa na janga kama la udhalilishaji na tukachelewa kufahamu,’’alieleza.

 


Akielezea lengo la mradi huo Mwenyekiti huyo wa PACSO, alisema ni kuwazindua wazazi, kufahamu viashiria na changamoto na namna ya kuwasaidia watoto wasifanyiwe matendo hayo.

 

Akifungua mafunzo hayo, Mratibu katika ofisi ya usajili wa asasi za kiraia Pemba, Ashrak Hamad Ali, alisema baadhi ya wazazi wanakosa muda wa kukaa na watoto wao, ili kusikiliza changamoto zinazowakabili.

 

Aidha aliwataka wazazi kujenga utamaduni wa kukaa na watoto wao ili kuwapa fursa ya kuwasikiliza sambamba na kufuatilia nyenendo zao za kila siku.

 



Katika hatua nyingine, Mratibu huyo, aliwataka waandishi wa habari kushirikiana na viongozi wa dini, kutoa elimu kwa wanandoa, ili kupunguza talaka za kiholela.

 

‘’Wakati mwengine wapo watoto wetu wanakumbana na changamoto za kimaisha na kisha kudhalilishwa ama kutelekezwa, moja ya sababu ikiwa ni wazazi kutengana,’’alifafanua.

 

Akiwasilisha mada kwenye mkutano huo kuhusu changamoto zinazowakabili watoto, Mratibu kutoka Chama cha waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA– Pemba Fat- hyia Mussa Said, alisema watoto wana haki ya kushiriki na kushirikishwa kwenye ngazi za kijamii.

 


 Akizitaja baadhi ya haki hizo kupitia mkataba wa kimatifa wa mwaka 1988 ni pamoja na ya kuishi, kuendelezwa kwa mujibu wa sera ya maendeleo ya mtoto Tanzania, kulindwa na vitendo viovu pamoja na haki ya kushirikishwa.

 

Nao washiriki wa mkutano huo, Aisha Abdallah Juma na mwenzake Abdurr-azak Imam Juma, walisema ni hatari kwa wazazi kupuuzi taarifa wanazopewa na watoto wao.

 


Sheha wa shehia ya Pembeni wilaya ya Wete Saumu Ali Hamad na mjumbe wa sheha shehia ya Wambaa Amini Haji Makame, walisema kukosekana kwa uthubutu wa wazazi, kuwakemea watoto kuiga mitindo ya kigeni ni moja ya chanzo cha kutokea kwa changamoto hizo.

 

Awali, Mratibu wa miradi kutoka PACSO Mohamed Najim Omar, alisema kama jamii haikuungana kama ilivyokuwa zamani kwenye malezi, watoto wataendelea kukumbwa na changamoto.

 




Aidha aliwataka washiriki wa mkutano huo, kuisambaaza elimu walioipata, ili kuona wazazi na walezi wanakuwa na mamko wa malezi kwa watoto wao.

 

Mradi huo wa miezi sita unatekelezwa kwa ufadhili wa Shirika la Irish Aid, unaendeshwa na Mtandao wa Asasi za Kiraia Pemba ‘PACSO’.

                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...