Skip to main content

WANANCHI MLETENI: 'MARUFUKU MGENI KUINGIA PASI NA TAARIFA'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa kijiji cha Mleteni, shehia ya Kisiwani wilaya ya Wete Pemba, katika kukabiliana na dawa za kulevy na wizi, wameendelea kupiga marufuku kwa mgeni yeyote, kuingia kijijini hapo, pasi na taarifa kwa uongozi wa kijiji.

Walisema, hawatomvumilia mgeni wala mwenyeji aliyefuatana naye, ikiwa watabainika ameingia kinyemela kijijini hapo na hakuna taarifa rasmi.

Walieleza kuwa, kwa sasa kijiji chao cha Mleteni, kiko salama kiasi, kwa dawa za kulevya na hata wizi, ndio maana wanawasisitiza wenyeji wanaotembelewa na jamaa zao, kutoa taarifa rasmi, kwa uongozi wa kijiji.

Mmoja kati ya wananchi hao Salim Mussa Ali, alisema ingawa utumiaji wa dawa za kulevya bado uko chini, lakini wanaendelea kuwataka wenyeji, wanaoingia na wageni wao, kutoa taarifa rasmi.

‘’Tumeshagundua kuwa, wapo wageni wengine wanakuja na nia mbaya katika kijiji chetu, sasa tukigundua na ikawa ana mwenyeji wake wa kijiji cha Mleteni, tutamfikisha mbele ya vyombo vya sheria,’’alieleza.

Nae Yassir Said, alisema bado kijiji chao kiko salama na utumiaji mkubwa wa dawa za kulevya, na ndio maana kila mgeni anayeingia, wamependekeza, kuwepo kwa taarifa zake kamili.

‘’Inawezekana ile mikakati yetu ya kila wakati, ikawa inasaidia kupunguza wimbi la vijana kuzurura ovyo, na baadhi ya wakati ndio wanaojihusisha na utumiaji wa dawa za kulevya,’’alieleza.

Akizungumzia juu ya wizi wa mazao kijijini hapo, mwananchi Alawi Said Yussuf, alisema wizi ni mkubwa kiasi, ingawa kwa sasa wanajiandaa kuanzisha kamati maalum.

Alisema, mifugo kama kuku na mazao kama ndizi, mihogo imekuwa ikiibiwa hasa nyakati za usiku, ingawa wamebaini ni watoto wao na sio wageni.

Kwa upande wao Asha Ali Sharif na mwenzake Aisha Nassib Shehe, walisema bado mkakati wa kweli na endelevu haujakuwepo wa kudhibiti vitendo vya wizi.



‘’Ni kweli utumiaji, usambaazaji na uuzaji wa dawa za kulevya kwenye kijiji chetu cha Mleteni haupo, lakini kama tukishindwa kudhibiti wizi, kisha dawa za kulevya zitafika,’’walisema.

Kaimu sheha wa shehi ya Kisiwani wilaya ya Wete, Bahati Juma Mtwana, aliwataka wananchi hao wa kijiji cha Mleteni, kuanzisha haraka ulinzi shirikishi kijijini hapo.

Alisema, kwa sasa karibu kila kijiji kwa Unguja na Pemba, kimeshaathirika kwa wizi, dawa za kulevya, vitendo vya udhalilishaji, hivyo kama kijiji chao cha Mleteni kiko salama na dawa za kulevya, waendelee kudhibiti.

Kaimu sheha huyo alisema, ingawa kwa sasa wamo katika kuufufua ulinzi shirikishi, lakini sio vibaya kijijini hapo wanao watakuwa na kamati yao.

Katika hatua nyingine, Kaimu sheha huyo wa shehia ya Kisiwani, amewakumbusha wananchi kuendelea kutoa taarifa Polisi, pindi wakibaini kuwepo kwa vitendo vya kihalifu.

‘’Kwa mfano kuna ubakaji, wizi, dawa za kulevya au jambo jingine lolote linaloashiria uvujivu wa amani, wasijaribu kuchukua hatua mikononi na badala yake, wawasiliane na mamlaka husika,’’alisisitiza.

Hata hivyo, amewataka wananchi hao kuwashajiisha watoto kuhudhuria masomoni, kwani serikali imesikia kilio chao cha ujenzi wa skuli ya maandalizi.

Mkuu wa wilaya ya Wete Dk. Hamad Omar Bakar, alisema wakati umefika sasa wa kuendelezwa kwa kamati za ulinzi shirikishi katika shehia.

                                  Mwisho   



Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch