Skip to main content

MKAGUZI WA POLISI JAMII AMWAGA VIFAA KWA WANAFUNZI WANAOJITAYARISHA NA MITIHANI

 



NA SAID ABDULRAHMAN, PEMBA@@@@


 WANAFUNZI wa skuli ya msingi na sekondari Pandani pamoja na sekondari Wete ambao wanajitayarisha na mitihani yao ya taifa, wamepatiwa msaada wa tochi na bablbu vyenye thamani ya shilingi 23,5000 kwa ajili ya kuwasaidia wakati umeme unapozimwa.

 

 Msaada huo umetolewa na Mkaguzi wa Polisi Jamii shehia ya Pandani, Inspector Khalfan Ali Ussi baada kutembelea kambi ya wanafunzi hao na kuona hali halisi ilivyo wakati unapozima umeme, jambo ambalo linawapa usumbufu wakati wanapopitia masomo yao.

 

Akizungumza baada ya kukabidhi vifaa hivyo alieleza kuwa, vitaweza kuwasaidia wanafunzi hao katika kujisomea wakati umeme unapokata kwenye mabweni yao.

 

Inspector Khalfan aliwataka wanafunzi hao kujitahidi katika masomo yao, ili waweze  kufaulu vizuri na kuwa wakombozi katika familia zao na taifa kwa ujumla.

 

Aidha alieleza kuwa, wako tayari kufuatilia nyenendo za wanafunzi hao na yeyote ambae atapatikana na hatia ya kutohudhuria kwenye masomo, adhabu kali itatolewa dhidi yake.

 

"Kwa wanafunzi ambao mnakaa kambi katika skuli zetu hizi, ni vyema tukafuata muda ambao umepangwa ili kuondosha matatizo ambayo yanaweza kuepukika", alieleza.

 

"Kwa wale ambao wamekimbia skuli, niwaombe wazazi na walezi kuhakikisha kuwa watoto hao wanarudi skuli kuendelea na masomo yao na hili sio ombi ni lazima", alifahamisha Khalfan.

 


Sambamba na hayo Inspekta huyo aliwasisitiza wanafunzi hao kuacha rushwa muhali kwani inarudisha nyuma maendeleo yao na jamii kwa ujumla.

 

"Pale ambapo kutatokezea tatizo lolote ambalo liko kinyume na maadili yetu, ni vyema tukatoa taarifa mapema ili jambo hilo liweze kuchukuliwa hatua na wala tusione aibu kusema ukweli", alisema Inspekta Khalfan.

 

Mapema Mratibu wa Polisi Jamii Mkoa wa Kaskazini Pemba Inspekta Makame Ali Makame alifahamisha kuwa, lengo la kuanzishwa Polisi jamii nchini, ni kuhakikisha wanaondosha vitendo vya uhalifu ambavyo vimekithiri katika jamii.

 

Inspekta Makame alieleza kuwa, katika jamii kumekuwa na matukio mbali mbali ya uvunjifu wa amani, hivyo aliwasisitiza wanafunzi hao kutoa taarifa kwa wakubwa wao pale ambao wataona kuna viashiria vibaya.

 



Sambamba na hayo Inspekta Makame aliwasisitiza wanafunzi hao kutumia muda wao mwingi katika kushughulikia masomo yao, kwani ndio msingi bora wa maisha yao ya baadae.

 

Nae Kaimu mwalimu Mkuu wa skuli ya msingi Pandani Halima Khalifan Said aliupongeza uongozi wa Polisi jamii hehia ya Pandani kwa kuwapatia wanafunzi hao msaada, ambapo umewapa faraja na furaha.

 

Aidha Halima aliahidi kushirikiana pamoja na uongozi wa Polisi Jamii shehia ya Pandani, ili kuona kero ambazo zipo katika skuli zao zinatatulia kwa mashirikiano ya wote.

 

"Tunamshukuru sana Inspekta Khalfan kwa msaada wake aliotupatia, hii inaonesha dhahiri kuwa ana upendo wa dhati kwetu", alisema Halima.







 

Nae mwanafunzi Fatma Salim alitoa shukrani kwa niaba ya wanafunzi wenzake na kusema kuwa kutatuliwa changamoto hiyo iliyokuwa ikiwakabili, imewapa matumaini makubwa kuendelelea na masomo yao.

 

"Tulikuwa tunapata shida sana wakati unapozimwa umeme, hivyo kwa vifaa hivi ambavyo tumepatiwa , tutavitunza ili kuona kwamba vinadumu kwa maslahi yetu ote”, alisema mwanafunzi huyo.

 

                                                     MWISHO 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch