Skip to main content

WAANDISHI HABARI PEMBA WAPEWA NENO RISITI ZA KIELEKTRONIKI

 



NA HANIFA SALIM, PEMBA@@@@

AFISA Mdhamini wizara ya maendeleo ya jamii jinsia, wazee na watoto Pemba Hafidh Ali Mohamed, amewataka waandishi wa habari watumie kalamu zao katika kuelimisha jamii juu ya ulipaji wa kodi na matumizi sahihi ya risiti za elektroniki.

Alisema kuwa, waandishi wa habari ndio daraja la mawasiliano hivyo, ni vyema kuitumia taaluma yao ya uwandishi wa habari katika uwandaaji wa makala na vipindi vya kila siku kwa lengo la kuielimisha jamii.

Aliyasema hayo alipoua akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari, huko ukumbi wa TASAF Chake chake uliyoandaliwa na klabu ya waandishi wa habari wa Pemba (PPC) kwa ufadhili wa mamlaka ya mapato Zanzibar ZRA.

"Maadhimisho haya ni muhimu na elimu mutakayoipata hapa itasaidia sana kuwajengea uwelewa juu ya masuala ya kodi, yatawasaidia kuandika habari za kweli, zenye uweledi na zilizofanyiwa utafiti wa kutosha, naomba tuyatumie mafunzo haya kwa vitendo", alisema.

Aidha alisema, serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na dk. Hussein Ali Mwinyi inahimiza sana ulipaji wa kodi kwa kupitia mifumo mipya, ambapo ni jambo muhimu na inahitaji wananchi wengi kujengewa uwelewa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari wa Pemba (PPC) Bakar Mussa Juma alisema, PPC ni miongoni mwa klabu 28 zilizopo Tanzania chini ya mwevuli wa umoja wa vilabu vya habari (UTPC).



Alieleza, PPC katika kuadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari imeamua kuwapatia elimu ya kodi na umuhimu wa matumizi ya risiti za elektroniki waandishi wa habari ikiwa ni njia moja ya kuhakikisha mapato yanaingia katika sehemu husika.

Akiwasilisha mada Afisa kutoka mamlaka ya mapato Zanzibar ZRA Pemba Khairat Said Soud alisema, changamoto zinazotokana na biashara katika ukusanyaji wa kodi ni wafanyabiashara wengi kutokufanya usajili na kupelekea uvunjaji wa mapato.

"Vile vile wafanyabiashara kutokutoa risiti na wananchi kutokua na mwamko wa kudai risiti, kutoa taarifa za mauzo zenye viwango vya chini ni miongoni mwa changamoto ambazo mamlaka inakabiliana nazo wakati wa ukusanyaji wa kodi", alisema.



Kwa upande wao waandishi wa habari walisema, suala la ulipaji wa kodi linahitaji uzalendo hivyo, ni vyema ZRA ikaandaa utaratibu wa kutoa elimu kwa jamii ili ipate uwelewa mpana juu ya ulipaji wa kodi na kudai risiti pale wanaponunua bidhaa.



Maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani huadhimishwa kila ifikapo Mei 3 ya kila mwaka, ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ya siku hiyo ni "KUUNDA MUSTAKBALI WA HAKI, UHURU WA KUJIELEZA KAMA KICHOCHEO CHA HAKI NYENGINE ZA BINAADAMU".

                           MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch