Skip to main content

ZIJUE POSA ZA MICHEWENI ZINAVYOTOFAUTIANA NA MAENEO MENGINE

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

‘’NILIVUNJIKA mkono, baada ya kuparamia nyumba kumkimbia muume mtarajiwa alipokuja kwetu, ili tusionane,’’anasema Saada Khsmi Kombo (65) wa Micheweni.

Hadi leo mkoni wake mmoja wa kushoto, eneo vilipootea vidole hapako sawa,baada ya ajali hiyo.

Kwa utamduni ulivyokuwa enza hizo, ilikuwa mwanaume hata kwa ambae alishabisha hodi na kuweka nia ya kufunga ndoa, haikuwa rahisi, kukutana na mtarajiwa wake.

Ndio maana Saada anasema, alilazimika kwenda mbio nyingi, kwani hakuwa na hamu ya kukutana na mume wake mtarajiwa, hasa kutokana na malezi yalivyokuwa.

KWANINI ILIKUWA HAWAONANI?

Rehema Faki Sheha (60), baada ya muume kuweka nia na posa kufuata, hapo mwanamke hukosa hamu hata ya kula, na hakukua na jambo la ushawishi la kukutana nae.

Anasema huo ndio utamaduni wa Micheweni, na wao wakiurithi tokea enzi na karne, ingawa hayo anasema ilitokana na mafundisho ya wazazi wao.

Walikuwa wakielezwa, kuwa mara baada ya mtoto wa kike kufikia utuuzima (kuvunja ungo), na kama akikutana na mwanamme na kufanya nae tendo la ndoa, atawapotezea heshima wazazi wake.

‘’Sio tu kwamba ilikuwa tunafunzwa madhara ya kupata mimba, au kuondoa uke, kujishusha thamani, lakini ilikuwa tukielezwa kuwa ni kuuvua nguo ukoo,’’anasema Saada Said Kombo (60).

Aisha Simba Mkasha (55) anasema, suala la kukutana na mwanamme hata kwa mazungunzo, kwao ilikuwa ni marufuku, labda iwe eneo la kutafuta elimu.

Haya anasema yalipelekea, kuanzia saa 12:00 jioni ilikuwa ni marufuku kwa mtoto wa kike wa Micheweni, kutembea nyakati hizo bila ya sababu za msingi.

‘’Mimi mara moja mama alinituma nyumba ya tatu, kumpelekea mtoto dawa, basi nilipokutana na mjomba, alinichapa bakora tatu na mama nae aligombwa na kuwekewa kikao,’’anasilimulia.

Anasema mjomba, yengewezekana kwenda katika eneo jingine, je mama yake engejuaje, akimaanisha ililazimika kufuatanishwa na mtu mwengine.

Hayo yote anasema, yalipelekea hata baada ya mwanamme kuweka nia ya kufunga ndoa, isiwe rahisi mtoto wa kike kukutana nae kwa mazungumzo.

Mwanaimani Khamis Juma, (45) anasema hata kwa umri wake, posa za Micheweni, anaziona zikoa tofauti na maeneo mengine, kaunzia siku ya kwanza hadi ndoa.

KWA UPANDE WA BWANA HARUSI MTARAJIWA

Faki Khamis Kai (59) anasema, hakuwa na uhuru wa kukutana na mke wake mtarajiwa, na hasa baada ya kamati ya maamuzi ya wazazi, kumkubali rasmi.

Muume mtarajiwa, baada ya kuchunguuzwa kwa mwezi mmoja na jawabu kupatikana kuwa amekubaliwa, alikuwa akitoa huduma kama za chakula na kitoweo.

‘’Lakini anaepeleka huduma hizo kwa mtarajiwa sio muume, bali ni baba yake, kaka, shangazi au mtu mwengine kutoka kwenye familia yake,’’anasema.

Hii ilihofiwa, mtarajiwa kuhamia ndani ya nyumba ya mchumba wake na kupelekea mdhara ya kuingiliana kimwili, kabla ndoa kufungwa.

Hamad Mbwana Shaame, (55) anasema, wakati mwengine wazazi wa mtoto wa kike, wanaweza kumualika mkweo wao mtarajiwa, kwa mfano kujumuika pamoja kwenye chakula.

‘’Usishangae wakati muume mtarajiwa anaalikwa, mke wake mtarajiwa ameshamishiwa kutoka kwao, kwenda kwa ndugu na jamaa zake wengine,’’anasema.

Hapa anamaanisha kuwa, suala la mke mtarajiwa na muume mtarajiwa, kamwe hawaonani mpaka siku ya harusi.

‘’Mimi ndoa yangu ilifungwa miezi minne baada ya posa, na muume ilikuwa tunakaa jirani, lakini nilimuona sura yake hasa, baada ya sikua saba ndoa kufungwa,’’anasimulia Mtumwa Khatib Omar.

Chakushangaaza utamaduni wa Micheweni ikiwa, suala la kuekesha mke, tokea akiwa na umri kati ya miaka saba hadi 10, na kuanza harakari za kupelekea huduma, unakubalika.

‘’Kwetu jambo kama hili wala halisababisha mtoto wa kike kukosa ufahamu wa masomo, wala kutembea tembea, maana ni urithi tokea wazazi wetu,’’anasema Hidaya Kombo Kassim.

NDOA/HARUSI ZA MICHEWENI ZA ASILI

Mke mtarajiwa, kwa siku saba kabla ya siku ya harusi, huhamishwa kutoka kwao kwenda kwa shangazi yake au mtu mwengine.

Akiwa huko hufunzwa namna ya kuishi maisha ya ndoa, ili awe mvumilivu, mstahamilivu, mwenye Imani, kujenga mapenzi na wakwe zake.

Rehema Faki Sheha, anasema lengo ni kuhakikisha anakuwa rafiki na mazingira yoyote atakayokutana nayo kwa muume wake, na hasa suala la ugumu wa maisha.

‘’Mafunzo aliyokuwa akipewa mtoto wa kike hayahusiani na uvulivu wa muume mwizi, mlevi, mpigaji bali hasa ni kupambana na maisha mapya ya ndoa na kumbadilisha muume kitabia,’’anasema.

Halima Haji Hamad anasema mafunzo hayo, pia yalikuwa yakiwasisitiza wanawake hao, namna ya kutimiza wajibu kwa muume, ikiwa ni pamoja na kumuhimiza usafi.

Khamis Othman Kombo, anasema mafunzo yalikuwa yakisaidia mno kuhakikisha ndao zinadumu, na kujiepusha na migogoro.

‘’Kwa mfano mke niliyenaye sasa huu ni miaka 46, lakini tunapokosana kabla mimi sijajua, alikuwa ananiaga kwenda kwao, kumbe anakimbia changamoto iliyojotokeza na akirudi maisha yanaanza upya,’’anasema.

Kuhusu sherehe ya ngoma, wanasema ilikuwa ni ngoma aina ya msondo pekee, na kwa asilimia kubwa, ukiwahusisha wanawake na watoto.

Ngoma hii ilikuwa ikipigwa siku moja kabla ya harusi na siku husika, na kutoka hapo siku ya tatu familia hujiandaa kumpelekea mtoto wao vyombo.

‘’Tukifika kule, sisi hufua nguo za harusi na kumpikia maana, siku ile huwa yule aliyempeleka ‘kungwi’ hutakiwa kupumzika, baada kufanyakazi nyingine,’’anasema Mwajuma Hamad Khamis.



POSA NA NDOA ZA LEO ZA MICHEWENI

Fatma Hamad Ali, anasema huo umeanza kupotea kwa kasi, hasa baada ya uwepo wa utandawazi ulioambatana na demokrasia uhuru wa kujieleza.

‘’Sasa kila mmoja awe mtoto wa kike au kiume anamtafuta mtarajiwa wake na kumpeleka mbele ya wazazi, na shida zaidi kama atakataliwa,’’anasema.

Alishashuhida ndoa tatu katika maisha yake, kuvunjika siku moja kabla, baada ya wazazi kumpokea muume kinyume na matakwa ya mtoto wao.

Issa Juma Haroub (30) anasema, sasa watoto wa kike na kiume wanakaa kwenye baraza na kupanga mipango ya harusi, aina ya nguo, vyombo na hata mahari.

Zuwena Mkasha Khalfan (26), anaona kuna athari kubwa ya kuacha utamaduni wa wazazi wa kumchagulia mke au muume mtoto wake.

‘’Wapo wanawake wenye umri kama wangu, wameshaolewa na waume wanne, kwa kule kujichagulia wenyewe waume, na kisha wanayokumbana nayo hawana pakwenda,’’anasema.

WAZEE

Hamada Shaame Khamis (73) kila muacha utamaduni anaweza kuyumba katika moja ya maeneo, aidha kwenye malezi ya watoto, uchungaji wa ndoa, heshima kwa majirani.

Sharifu Massoud Hamad (60) anasema, sasa ndoa kudumau kwa miaka 30 hadi 45 ni jambo la maajabu, na anaona hazipo.

‘’Mimi nimedumu ndani ya ndoa kwa miaka 35, kabla muume wangu kufariki, na ilikuwa kila mmoja anamvumilia mwenzake, kwani yeye kapewa mimi na mimi nimepewa yeye na wazazi wetu,’’anasema.

Anasema sio rahisi kurudi tena kwa ile ya Micheweni asili, ambayo watoto walikuwa wanatii kwa wazazi wao, jambo lililoongeza baraka na mapenzi ndani ya familia.



WANAHARAKATI WANASEMAJE?

Wanasema, haki ya muume kuchagua mke amtakae, ndio hasa inayokuza maelewano, ushirikiano, uaminifu miongoni mwa wanandoa.

Tatu Abdalla Msellem, wa Chake chake anasema, kama utamaduni haukwazi upande mmoja, unafaa kuendelezwa na kukuzwa, kwani msingi wa maisha ni kuishi kwa amani.

Asha Khamis Juma wa Mkoani, anasema kila eneo huwa na utamaduni wake, ingawa la kuzingatia ni kuhakikisha hakuna udhalililishaji na ukatili.

‘’Kwa mfano ikiwa eneo la Micheweni walikuwa na posa hadi ndoa zinazofuata utamaduni na ndoa zinadumu bila ya manung’uniko ni jambo jema,’’anasema.

VIONGOZI WA DINI YA KIISLAMU

Sheikh Said Ahmad, anasema dini ya kiislamu, inaridhia mwanamke mtarajiwa kuonekana na mume mtarajiwa, uso na viganja chini ya familia yake.

Kwa mfano muume mtarajiwa anataka kumuona mtu aliyependekezewa na familia yake, iko ruhusa ya kumuona, ingawa wasio wao wawili peke yao.

Sheikh Mohamed Issa Ali, anasema hata kama anataka kuona nywele, ngozi, mguu, mkono anaweza kuwatuma dada zake au shangazi zake.

SERIKALI KUU INASEMAJE?

Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Zanzibar Tabia Maulid Mwita, anasema moja ya jukumu la Idara ya Utamaduni na Sanaa, ni uhifadhi, uendelezaji na ukuzaji wa shughuli za utamaduni kwa wananchi.

Aidha waziri huyo anasema, kazi jukumu jingine ni utoaji wa elimu ya utunzaji wa utamaduni ambao unalenga kuendeleza jamii husika.

                                 Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch