Skip to main content

WADAU HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI PEMBA WATOA RAI

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAHARAKATI wa haki za watu wenye ulemvu wakili kisiwani Pemba, wamesema wakati umefika kufanyiwa marekebisho sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai nambari 7 ya mwaka 2018, ili kuongeza kifungu kitakachowanyima dhamana, watuhumiwa watakaowadhalilisha watu wenye ulemavu wa akili.

 

Walisema, sheria hiyo kwenye kifungu chake cha 151, kimeanisha makosa yasiyo na dhamana ikiwa ni pamoja na kuua kwa makusdi, uhaini, kubaka, kusafirisha kiwango kikubwa cha dawa za kulevya, kuingilia kinyume na maumbile.

 

Makosa mengine yalioanishwa kwenye kifungu hicho, ambayo hayana dhamana ni kumnajisi mtoto wa kiume, kubaka kwa kundi, kuingilia maharimu pamoja na unyang’anyi wa kutumia silaha.

 

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema katika kifungu hicho, haikuanishwa iwapo mtu atambaka, kumnajisi, kumuingilia kinyume na maumbile mtu, mtoto, mwanamke au mwanammke mwenye ulemavu wa akili.

 

Walisema, kasoro hiyo inaweza kutoa mwanywa kwa wadhalilisha, kuendelea kuliathiri kundi la watu wenye ulemavu wa akili, wakijua wanapata dhamana mahakamani.

 



Mmoja kati ya wanaharakati hao kutoka Jumuiya kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar ‘ZAPDD’, kisiwani Pemba, Khalfan Amour Mohamed, alisema lazima kuwepo kifungu mahasusi.

 

Alieleza kuwa, kifungu hicho kiongeze kosa jingine la ubakaji, ulawiti na unajisi kwa mtu wa umri wowote, mwenye ulemavu wa akili, iwe ni kosa lisilokuwa na dhamana, kama yalivyo mengine.

 

‘’Kubaka, kulawiti na kuingilia kinyume na maumbile hata kama aliyedhalilishwa yuko sawa kwenye afya ya akili, akifika mahakamani mtuhumiwa hana dhamana, lakini iweje kwa makosa hayo akitendewa mwenye ulemavu wa akili, kuna dhamana,’’alihoji.

 

Kwa upande wake Mratibu wa TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema kasoro hiyo isiporekebishwa, kundi la watu wenye ulemavu wa akili, litaendelea kukosa haki zao.

 

‘’Kama sheria ni msumeno, na Zanzibar inaendelea kuzilinda haki za watu wenye ulemavu wa akili, lazima na hili lifanyiwe marekebisho, ili atakayemdhalilisha mtu wa kundi hilo, anyimwe dhamana,’’alishauri.

 

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati tendaji wa Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’ Hidaya Mjaka Ali, aleleza kuwa, ili kulilinda kundi hilo, lazima sheria ziwatambuwe.

 


Mama mzazi wa mtoto mwenye ulemavu wa akili kutoka shehia ya Pujini, ambae mtoto wake alidhalilishwa na mtuhumiwa Abdalla Khatib Abdalla, alisema ipo haja ya sheria kurekebishwa.

 

‘’Hata mimi nilishangaa kuwa, nasikia makosa haya hayana dhamana, lakini ukimdhalilisha mtu mwenye ulemavu wa akili, kumbe dhamana ipo,’’alihoji mzazi huyo.

 

 Mzazi mwengine wa shehia ya Kengeja wilaya ya Mkoani, ambae kijana wake mwenye ulemavu wa akili alibakwa na askari wa chuo cha Mafunzo Suleyom Idd Saleh, alishangaa baada ya kumuona, alipata dhamana.

 

Wakati akiwasilisha mapungufu ya sheria mbali mbali kwenye mkutano na waandishi wa habari ulioandaliwa na TAMWA, Mwanasheria wa serikali, Ali Amour Makame alisema, suala la marekebisho ya sheria ni jambo jema.

 

‘’Ni kweli kifungu cha 151 (1) cha sheria nambari 7 ya mwaka 2018 ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Zanzibar, imeanisha wazi makosa yasio na dhamana, ingawa la kudhalilishwa mtu mwenye wa akili, halimo.

 


Nae mwananchi Khadija Issa Mzale wa Chake chake, anashauri kuwa ingetungwa sheria moja tu ambayo itajumuisha makosa yote ya udhalilishaji, badala ya sasa kuwepo kwenye sheria tofauti kama vile ile ya kuwalinda wari na mtoto wa mazazi mmoja nambari 4 ya mwaka 2005.

 

Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saadi Khamis, alisema changamoto kubwa kwa wenye ulemavu baada ya kudhalilishawa, ni kukosa taaluma ya kuyaripoti matendo hayo.

 

Aliyekuwa hakimu wa mahakama ya watoto Pemba, Luciano Makoye Nyengo, alisema changamoto inayojitokeza hadi kesi za watoto wenye ulemavu wa akili, kutofikia pazuri ni changamoto ya ushahidi.

 

Kijana Asha Said Omar mwenye ulemavu wa viungo wa Michakaini Chake chake, alisema ni vyema kuharakishwa kwa marekebisho hayo, ili watu wenye ulemavu walindiwe haki zao.

 

Kifungu cha 30 cha sheria ya watu wenye ulemavu Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kinasisitiza wajibu wa kila mtu kulinda, kutetea haki za watu wenye ulemavu, ikiwemo pale wanapovunjiwa haki zao za msingi, ikiwemo kudhalilishwa.

 

Na kifungu cha 31 kikafafanua kuwa, watu wenye ulemavu hawatobaguliwa au kudhalilishwa, kwa namna yoyote, kwa sababu ya ulemavu wake. 

 

Lakini hata mkataba wa kimataifa wa haki za watu weye ulemavu, Ibara ya 5 imeweka usawa na kutobaguliwa mbele ya sheria, kwamba watu wote wako sawa.

 

Hayo yakijiri, hata Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kuanzia kifungu cha 11 hadi 25A kinasisitiza usawa mbele ya sheria na kwamba mtu hatodhulumiwa haki zake.

                                   Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch