Skip to main content

KIJALUBA, MRADI UNAOLENGA KUKUZA PATO LA WATU WENYE ULEMAVU

 



NA HAJI NASSSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI 1876, wakiwemo wanawake 1,122 na wanaume 750, kutoka shehia za wilaya ya Chake chake Pemba, wengi wao wakiwa watu wenye ulemavu, wanatarajiwa kufikiwa na taaluma ya kujikomboa kiuchumi, kupitia mpango wa kuweka akiba.

Watu hao, watawezeshwa kupitia vikundi maalum vitakavyoanzishwa katika kila shehia ya wilaya hiyo, ambapo kila kikundi, kitakuwa na wastani wa wanachama kati ya 25 hadi 30.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Msaidizi afisa mradi wa kijaluba Mohamed Salim Khamis, alisema watu hao wanatokea kwenye vikundi 72, ambavyo vyote vitawezeshwa kimafunzo.

Alieleza kuwa, vikundi hivyo baada ya kuanzishwa kitaalamu namna ya uwekaji akiba, kisha vitapewa elimu ya ujasiriamali, pamoja na kuunganishwa na taasisi za kifedha.

Alifafanua kuwa, mradi huo unakuja kuondoa dhana kuwa watu wenye ulemavu hawezi, badala yake unakuja kuwawezesha, kuanzia mafunzo na kimbinu.

Alifahamisha kuwa mradi huo, utakuja kuionesha jamii namna ambavyo watu wenye ulemavu, wanaweza kupata mafanikio, kupitia fedha zao walioziweka kama akiba.

Alisema, fedha hizo watafundishwa namna ya kuziendeleza kwa ajili ya kujikwamua na umaskini, kupitia vikundi vya uzalishaji watakavyoviendesha wenyewe.



‘’Mradi huu ambao utajumuisha pia watu wasiokuwa na ulemavu, watafanyakazi kwa pamoja, na lengo ni kuona kuwa watu hao, wanaweza kujikomboa,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Msaidizi huyo afisa mradi huo, alifafanua kuwa, pamoja na kuwawezesha kiuchumi watu wenye ulemavu, lakini pia wataongezewa, uwelewa juu ya uongozi.

‘’Kwa mfano, katika nafasi sita za uongozi kwenye vikundi hivyo vya kuweka akiba, nafasi nne, lazima zishikiliwe na watu wenye ulemavu,’’alieleza.

Alisema hilo linatokana na kwa sasa, kutengwa na jamii, juu ya suala la uongozi, na kuonekana kama vile hawana hadhi ya kuwa viongozi.

Hata hivyo alisema, ndani ya vikundi hivyo, kutakuwa na mfuko maalum wa jamii, ambao utawasaidia pale wanapokumbwa na majanga mbali mbali, katika maisha yao.

Kwa upande wake, afisa utawala kutoka shirikisho la jumuiya za watu wenye ulemavu SHIJUWAZA kisiwani Pemba Aisha Abdalla Juma, alisema wamefurahishwa, na ujio wa mradi huo.

Alieleza kuwa mradi huo, utakwenda kuwaamsha watu wenye ulemavu, juu nafasi yao katika jamii, katika kujikwamua na umaskini unaowakabili.



Nae mwezeshaji wa vikundi vya watu wenye ulemavu ‘CRP’ Fatma Abrahman Ali wa shehia ya Ole wilaya ya Chake chake, alisema anasimamia vikundi tisa, vyenye wanachama wastani wa 25 hadi 30 kwa kila kimoja.

Alisema, katika vikundi hivyo kwa mfano chenye wanachama 30, ni lazima 20 wewe wenye ulemavu, kwani ndio hasa malengo ya mradi huo.

‘’Kwa saa tunaendelea na mafunzo sisi waalimu, kisha tutakwenda kwa jamii, kuwahamasisha namna ya uundaji wa vikundi vya kuweka akiba, ili sasa wapate kujikomboa,’’alifafanua.

Nae mwalimu wa vikundi hivyo kutoka ‘SHIJUWAZA’ Fatma Abdalla Issa, alifafanua kuwa, kutokana na mafunzo waliokwishapatiwa, sasa wako tayari kwenda shehiani.

‘’Tunakwenda kuvifundisha vikundi jumuishi vya kuweka akiba, ili sasa wapige hatua kwenye kukua kiuchumi, kwa kule kuanzisha biashara ndogo ndogo hapo baadae,’’alieleza.



Mratibu wa TAMWA-Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema kazi yao kubwa katika mradi huo, ni kuwaunganisha waandishi wa habari katika mradi huo, ili kutoa habari mbali mbali.

‘’Sisi kama TAMWA, tunawajibu wa kupatia haki zao watu wenye ulemavu, na ndio maana tunafanyakazi kwa karibu na vyombo vya habari, ili sasa kuutangaza mradi na nafasi ya watu wenye ulemavu, katika kukuza pato lao,’’alieleza.

Mradi wa Kijaluba, ni jumuishi unaolenga kuwawezesha watu wenye ulemavu kiuchumi, kwa kule kuwajengea uwezo kuhusu maisha yao na jamii zao.

Mradi huo unatarajiwa kukuza uwezo wa kundi hilo, samba mba na kujenga mitazamo chanja, juu ya ushiriki wao, kujiingiza katika shughuli za kujipatia kipato.

Aidha mradi huo wa ulioanza mwaka 2022, ukitarajiwa kumalizika mwaka 2024, utakwenda kushughulikia vikwazo vinavyowarudisha nyuma, watu wenye ulemavu.

Kwa sasa mradi huu, anatekeleza wilaya ya Kusini Unguja na Chake chake kisiwani Pemba, kama eneo la majaribio, ambapo walengwa wakuu ni watu wenye ulemavu wakiwemo vijana, watoto kwa asilimia 60 na 40 na watu wengine.

                               Mwisho      

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch