Skip to main content

MADEREVA GARI ZA ABIRIA PEMBA WANG'AKA NAULI MPYA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MADEREVA na makonda wa gari za abiri kisiwani Pemba, wamewalalamikia abiria, kuendelea kutoa nauli za zamani, na kuacha nyongeza ya shilingi 100, iliyoongezwa na serikali mwaka jana.

Walisema, baada ya serikali kuongeza nauli mwaka jana wastani wa shilingi 100, kutoka nauli za zamani, bado baadhi ya abiria wamekuwa wazito, kutimiza haja hiyo ya kisheria.

Wakizungumza na mwandishi wa habari mjini Chake chake, walisema kwa mfano nauli ya kutoka Chake chake hadi Mtambile ni shilingi 1,300, bado abiria wanalipa kati ya shilingi 1000 hadi shilingi 1,200.

Mmoja kati ya dereva huyo, Mohamed Khamis, anayefanyakazi barabara ya Chake chake –Mkoani alisema, hata nauli mpya ya shilingi 1,800 kutoka Chake chake hadi Mkoani, abiria waliowengi wanalipa shilingi 1,500.

‘’Ukiwauliza kuwa mbona hawalipi nauli mpya, anakujibu kuwa hana chenji, lakini hajui kuwa sisi tunapokwenda sheli kutia mafuta, hilo jambo hilipo,’’alisema.

Nae dereva Abdalla Omar anayefanakazi Mwambe- Chake chake alisema, hata nauli ya kutoka Mwambe hadi Mtambile kwa sasa ni shilingi 600, ingawa abiria wanalipa shilingi 500.

‘’Mafuta yapenda na ndio maana serikali, iliamua kupandisha nauli kidogo, ingawa bado abiria wanalipa kwa nauli ya zamani,’’alilalamika.

Nae dereva anayefanyakazi barabara Chake chake –Wete Himid Khalfan, anasema wamekuwa wakishambuliana na abiria, ndio baadhi yao, hulipa nauli kamili mpya.

‘’Tumebandika ndani ya gari zetu nauli mpya zilizotangaazwa na serikali tokea mwaka jana, lakini bado abiria wanapuuza nauli hizi na kutulipa za zamani,’’alieleza.

Abiria Aish Mjaka Haji wa Kiwani alisema, sio sahihi kuwa wanalipa nauli kongwe, bali wanachokifanya baadhi ya makondakta, ni kuongeza zao za juu.

‘’Kwa mfano nauli kutoka Chake chake hadi Mgagadu ni shilingi 800, lakini ukiwapa shilingi 1,000 hawarejeshi chenji, na ukiwauliza wanasema mafuta yamepanda,’’alieleza.

Nae Mwanakhamis Haji Mcha wa Mwambe alisema, kwa sasa baadhi ya makondakta wanawalipisha nauli ya shilingi 700 kutoka Mwambe hadi Mtambile, badala ya shilingi 600 ya iliyotangaazwa.

Zuhura Khamis Omar na mwenzake Mwanaisha Kheir Nassor wanaotumia barabara ya Konde -Chake chake, walisema makondakta katika barabara yao, nauli zao hazitabiriki.

‘’Abiria wakiwa wengi na gari chache, au kama siku ya kuja meli hapo nauli hupandishwa na kuivuuka ile elekezi ya serikali,’’alisema Zuhura.

Katibu wa Jumuiya ya wamiliki wa gari za mizigo na abiria mkoa wa kusini Pemba, ‘PESTA’ Hafidh Mbarka Salum, amerejea kauli yake ya kuwataka wananchi, wanaonyanyaswa na makondakta kuwaripoti kwao.

Aidha, amesema dereva ambaye atabainika kukiuka maagizo ya serikali, kwa makusudi, ‘PESTA’ asitegemee kuwa itasimama kumtetea, na badala yake sheria, itachukua nafasi yake.

Katika eneo jengine Katibu huyo, amewataka abiria kukamilisha nauli iliyowekwa na serikali, na sio nyingineyo, kwani gari hizo, zinatumia gharama kubwa hadi kuweko barabarani.

Mwezi Septemba mwaka 2022, serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ilitangaaza kupandisha nauli mpya kwa gari za abiria, wastani wa ongezeko la shilingi 100, kufuatia kupanda kwa bei ya mafuta, ambapo mara mwisho kutangaazwa nauli, mpya ilikuwa ni mwaka 2019.

Nauli mpya iliyotaangazwa mwaka jana, ilikuwa kwa daladala zenye umbali wa kilomita 1 hadi 12, imepanda kutoka shilingi 400 hadi shilingi 500.

Ambapo kwa umbali wa kilomita 19 hadi 21, nauli imepanda kutoka shilingi 800 hadi shilingi 900, wakati kwa zenye umbali mfupi wa kilomita 1 hadi kilomita 14, imepanda kutoka shilingi 500 hadi shilingi 600 na kwa umbali mrefu wa kilomita 60 hadi 70 nauli imepanda kutoka shilingi 2,300 hadi shilingi 2,500.

                     Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch