Skip to main content

BAADA YA KUTOFIKIWA NA ELIMU CHANJO YA UVIKO19, VIZIWI PEMBA WATOA RAI

 


 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KUNDI la watu wenye uziwi kisiwani Pemba, limetoa raia kwa mamla husika, kuacha kuwachanganya na wengine bila ya wakalimani, wanapowafikishia taaluma za kitaifa.

Wanasema, wamekuwa wakiishia kucheka na kupiga kofi, kwenye vikao na mikutano ya kutoa elimu, kwa kule kukosekana kwa mkalimani.

Wameonya kuwa, kwa mfano kwenye elimu ya ugonjwa wa Uviko19, samba mba na ujio wa chanjo yake, hawakutengewa mikutano yao ya kielimu, wakiwa na wakalimani.

Asha Suleiman, mkalini anayetambulika kisiwani Pemba, anasema hakuwahi kushirikishwa na wizara husika, juu ya kuwakusanya viziwi kupatiwa elimu hiyo.

Hilo, anasema lilisababisha kundi la viziwi kukosa taarifa za sahihi za chanjo ya Uviko19, jambo ambalo liliwakoseha kufanya uamuzi sahihi.

‘’Shughuli kadhaa za kitaifa huwa nashirikishwa na kundi la watu wangu, lakini kwenye elimu ya chanjo ya Uviko19, hautukuwahi kuitwa,’’analalamika.

WANATOA RAIA GANI KWA SERIKALI

Anasema, kama mikataba iliyosainiwa ina malengo ya kweli na kundi hilo, wasisite kuwashirikisha katika vikao na mikutano maalum ya elimu.

‘’Inawezekana kundi la viziwi lilishirikishwa, lakini halikupata ushirikishwaji, maana walichanganywa na wengine na wao wakaishia kupiga kofi,’’anasema.

Anaona njia iliyotumiwa na wizara ya Afya ya kuvamia makundi ya watu na kuwapa elimu, katika vijijini pasi na kuzingawatiwa kwa viziwi, haikuwasaidia.

Mohamed Khamis Shehe Mratibu wa Chama cha Viziwi Zanzibar ‘CHAVIZA’ wilaya ya Chake chake, anasema njia rahisi ni kuwashirikisha.

 Anaziomba mamla husika, kuvitumia vyama vyao moja kwa moja, wanapotaka kutoa elimu ya kitaifa, na sio kuwachanganya na makundi mengine.

‘’Tunaweza kuchangaywa na makundi mengine, lakini lazima waandaji wawasiliane na mkalimani wetu,’’anashauri.

Asha Haji Hassan wa kisiwa cha Makoongwe wilaya ya Mkoani, anasema hata watoa elimu ngazi ya vijiji ‘CHV’ ni vyema wakawezeshwa, ili kuwafikia.

‘’Kwa mfano CHV’ wamekuwa wakijitahidi kusambaaza elimu ya chanjo ya Uviko19, lakini tunaposhiriki na sisi ili tuhapati elimu, huwa vigumu maana hawajui lugha ya alama,’’anasema.

Mzazi mwenye vijana watatu wenye uziwi mkaazi wa Kisiwa Panza wilayani humo, anasema alilazimika kuwapatia elimu ya juu juu vijana wake.

‘’Ni kweli kundi la wenzetu wenye uziwi, halikupata elimu ya moja kwa moja ya chanjo ya ugonjwa wa Uviko19, na ilitulazimu sisi wazazi tuwaelekeze,’’anasema.



Mjumbe wa Kamati tendaji ya Jumuiaya ya wanawake wenye Ulemavy Zanzibar ‘JUWAUZA’ Hidaya Mjaka Ali, anasema, njia ya wenzao wenye uziwi kufikiwa ni kuendesha mafunzo chini ya mkalimani.

‘’Wenzetu wenye uziwi ni tofauti na sisi watu wenye ulemavu wa viungo, albinazim hawa wanawakalimani wao, kila kwenye vikao wawepo,’’anashauri.

Mratibu wa Baraza la Taifa la watu wenye Ulemavu Zanzibar ofisi ya Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, anasema, iwapo taarifa za kitaifa zitakosa wakalimani, kundi la viziwi litaendelea kuzikosa.

Anakiri kuwa, ile elimu rasmi ya Uviko19 na hasa inayoambatana chanjo, kutoka kwa wataalamu wa afya, watu wenye uziwi imefika kwa kundi dogo mno.

WIZARA YA AFYA

Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali, anasema walichokifanya ni kukutana na wakuu wa Jumuiya za watu wenye ulemavu, ili kuwapa elimu.

‘’Naamini katika elimu ya kujikinga na Uviko19, hakuna mtu aliyeachwa nyuma, na hasa wenzetu wa makundi maalum, tulikuwa na mkakati malum,’’anasema.

Anasema, jambo ambalo linawezekana kuwa, wale wakuu wa jumuiya za watu wenye ulemavu, hawakuwashushia elimu hiyo, wenzao wenye ulemavu, licha ya wizara kukutana nao.

Eneo jingine, hadi leo hii wameweka utamaduni wa kuyataka makundi yote, yawaalike wataalamu wa afya popote walipo, ili wapatiwe elimu ya Uviko19.

‘’Inawezekana, kwa mfano, wenye uziwi wapo kisiwani na kufika mjini ni shida, kwa mujibu wa mazingira yao, sasa wawasiliane na maafisa wetu wa afya wa wilaya na watafuatwa walipo,’’anasema.

Ingawa upande mmoja, Mratibu wa kitengo cha elimu ya Chanjo cha wizara hiyo Pemba Bakar Hamad, anasema utaratibu wao ulikuwa, ni kuyaenda makundi kuyapa elimu.

‘’Kwa mfano tunakwenda kwa vikosi vya ulinzi na usalama, wanafunzi wa skuli, vyuo vikuu, waandishi wa habari, wakulima, watumishi wa umma na viongozi wa dini,’’anasema.

Hivyo anasema hakumbuki kuwa, na mpango maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa uziwi peke yao, bali walikuwa na mikutano ya elimu kwa makundi mchanganyiko.

Anakiri kuwa, kwa Pemba, hakuna hata kundi moja ambalo halikufikiwa na elimu ya Chanjo ya Ukivo 19, ingawa akaweka wazi kuwa, kama litajipanga kundi la watu wenye viziwi wakiwa na mkalimani wao wako tayari.

 NINI ATHARI YAKE?

Himid Mcha Khamis kiziwi mkaazi wa kisiwa kidogo cha Fundo wilaya ya Wete, anasema ni kuwa rahisi wao kushambuliwa na uogonjwa wa Corona au mengine ya mfumo wa hewa.

Aisha Haji Makame wa kisiwa cha Makoongwe, anasema wamevunjiwa haki zao ambazo zimeainishwa kwenye mikataba na sheria mbali mbali.

Afisa Mdhamini wizara ya Afya Khamis Bilali Ali, anasema moja ni kukumbwa na maambukizo kwa wepesi, kama hawakuwa na elimu ya kujikinga.

Afisa wa Chama cha Viziwi wilaya ya Chake chake Mohamed Khamis Shehe, anasema ni kuwaweka wao katika msingi wa kukumbwa na magonjwa.

MIKATABA INAVYOHESHIMU HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU   
Mkataba  wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu, ambao Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliusaini, Machi mwaka 2007 na kuthibithisha mwaka 2009, unalazimisha huduma za afya kwa watu wenye ulemavu.

Ibara ya 25, inasisitiza nchi wanawachama, zitumbue kuwa, watu wenye ulemavu wanayo haki ya kunufaika kwa kiwango cha juu, huduma za afya bila ya ubaguzi wowote.



Mkataba ukafafanua, nchi husika zitachukua hatua zinazostahiki, kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata huduma bora za afya.

‘’Nchi wanachama, zitatoa huduma za afya, zinazohitajika kwa watu wenye ulemavu, hasa kutokana na aina ya ulemavu wao, yakiwemo maeneo ya vijijini,’’umefafanua Mkataba huo.

Ukaongeza kuwa, nchi hizo zitawataka wataalamu wa afya, kutoa huduma za kiwango sawa, kwa watu wenye ulemavu, kama zinavyotolewa kwa watu wengine, ikiwa ni pamoja na misingi ya kutoa ridhaa kwa uhuru na ufahamu wa kutosha.

Mwaka 1983 hadi 1992 hatua mbali mbali zilichukuliwa, ikiwani pamoja na maamuzi ya mwisho ya Umoja wa Mataifa, kuitangaza Disemba 3 ya kila mwaka, iwe ni siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu duniani.

Ambapo siku hiyo pamoja na mambo mengine, kundi la watu wenye ulemavu hujadili, mafanikio na changamoto zao, zikiwemo huduma za afya.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nayo, iliunda Mkakati wa Kitaifa wa Ujumuishi wa mwaka 2010 hadi 2015 na sera ya taifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2004, ukitaja uhitaji wa lazima wa huduma za afya wa watu wenye ulemavu.

Ipo sera ya kitaifa ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2018 kwa upande wa Zanzibar, ambayo nayo kwenye Ibara ya 20, ikasisitiza uimarishwaji wa upatikanaji huduma bora na endelevu kwa watu hao.

Kuhusiana na hatua za kisheria, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ilitunga sheria ya Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2010, ambapo ilikuja kuharakisha pia suala la huduma bora za afya.

Zanzibar, ambayo ilikuwa na Sheria ya Watu wenye Ulemavu, nambari 9 ya mwaka 2006, ambayo sasa imefutwa na kuwa na sheria mpya nambari 8 ya mwaka 2022.

Kifungu cha 28 (1) (c) cha sheria hiyo, kimeanisha haki ya kupata huduma za afya kwa watu wenye ulemavu, ikiwemo matibabu, matengenezo au marekebisho yanayohusiana na aina ya ulemavu wao.

Tanzania bara pia iliunda Mpango Mkakati wa Sekta ya Afya ambao unatoa mwongozo wa ufikiaji wa huduma za afya kwa makundi yote yakiwemo ya watu wenye ulemavu kama viziwi.

Kwa upande wa Zanzibar, kulikuwa na Mpango Mkakati wa sekta ya afya wa miaka tisa, ambao uliishia mwaka 2019, wenyewe ulitaja hatua za kuchukuliwa, ili kuwakinga na utapia mlo wanawake, watoto na watu wenye ulemavu.



UGONJWA WA CORONA NA CHANJO YAKE

Wakati hayo yakifanyika, Machi 11, 2020, Shirika la Afya Ulimwenguni ‘WHO’ iliiratibisha rasmi ugonjwa COVID-19 kama janga la dunia.

 Hii baada ya ugonjwa huo wa mlipuko wa kuenea kwa kasi duniani kote, ambao huenea kwa haraka katika mataifa na mabara mbali mbali.

Aidha WHO iligundua kuwa, watu 4,291 walikuwa wameshaaga dunia na maelfu zaidi walikuwa wamelazwa hospitalini kwa muda mfupi.

 

Baada ya janga hilo, wataalamu wa afya waliibuka na chanjo za aina mbali mbali, ambazo baada ya majaribio zikabainika kuwa, zinaweza kuwa kinga.

 

Na hapo sasa wizara ya Afya Zanzibar kwa upande nwake, ilidhamiria hadi ikiingia mwaka 2023 iwe wazanzibari 70 kila 100 wameshapata chanjo za Corona.

 

Huku hayo yakipangwa, Shirika la Afya Duniani (WHO) lilisema Julai 27, mwaka 2022 kuwa hadi kufikia Julai 25, 2022 jumla ya dozi bilioni 12.24 za chanjo ya Covid-19 zilitolewa duniani kote.

 

Utoaji wa chanjo dhidi ya Covid-19 hapa nchini ulizinduliwa Julai 28, mwaka 2021 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ambapo chanjo aina ya Pfizer, Moderna, Sinopharm, Sinovac na Jansen ziliidhinishwa kutumika.

TAKWIMU YA WALIOCHANJA

Katika kipindi cha tarehe 29 Oktoba hadi 02 Disemba, 2022, jumla ya visa vipya 442 vimethibitika kuwa na maambukizi ya Uviko19.

Imebainika kuwa, idadi hii ni kubwa ukilinganisha na takwimu za mwezi uliopita ambapo kulikuwa na visa vipya 272, sawa na ongezeko la asilimia 62.5.

Hadi kufikia tarehe 02 Desemba 2022, jumla ya watu milioni 29,123,387 kati ya walengwa 30,740,928 ambao ni sawa na asilimia 94.7 wamepata dozi kamili ya chanjo ya UVIKO- 19.

                              Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch