Skip to main content

WADAU WA KUPINGA UDHALILISHAJI PEMBA, WATAKA SHERIA INAYOTAJA KIWANGO CHA FIDIA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WADAU wa haki jinai kisiwani Pemba, wamesema wakati umefika sasa, kuwepo kwa kifungu maalum cha sheria, kinachotaja kiwango mahasusi cha fidia, kwa mtu aliyedhalilishwa.

Walisema, kifungu hicho cha sheria, pamoja na kutaja kiwango, kiweke ulazima wa kulipwa kwa muhanga huyo, na hasa pia kuilazimisha Mahakama, kuzingatia maumivu ya muathirika huyo.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema kwa sasa hakuna kifungu cha sheria, kinachoonesha kiwango maalum, hasa kulingana na maumivu aliyoyapata aliyedhalilishwa, hali inayopelekea kupata athari mara mbili.

Walisema, kwa sasa Mahakama hufanya makisio ya kutamka kiwango cha fidia, ingawa imekuwa vigumu kutaja kiwango kwa upana wa maumvivu.

Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-Hya Mussa Said, alisema wapo watoto hudhalilishwa na wengine kupoteza utu wao na wengine kupata ulemavu, ingawa fidia inayotajwa huwa ni ndogo.

Alieleza kuwa, haiwezekani mtoto aliydhalilishwa na kisha kutakiwa alipewa shilingi 100,000 au shilingi milion1, kama fidia, jambo ambalo linamzidishia maumivu.

‘’Lazima sasa kuwepo kwa sheria maalum, au kuwepo kwa kifungu ndani ya sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, ikitaja kwa upana, fidia kwa wahanga wa udhalilishaji.

Nae mwanaharakati Mwanakhamis Issa Ali wa Chake chake, alisema thamni ya mtu, ni kutokuchezewa sehemu yake, hivyo kama atatokea mwengine kumvunjia haki yake, kusiwe na adhabu ndogo.

‘’Kwa mfano mtoto wa kike aliyeondoshewa utu wake, walau fidia ianzie shiligi milioni 100, lakini sio jambo la shilingi mioni 1 au shilingi 500,000 kama ilivyo sasa,’’alieleza.



Kwa upande wake Mkurugenzi wa PEGAO, Hafidh Abdi Said, alisema kinachosikitisha hata hiyo fidia ndogo inayotangaazwa mahakamani, waathirika haiwafikii.

Alifafanua kuwa, zipo hukumu kadhaa ambazo, mahakama imemkuta na hatia mshitakiwa, na hutakiwa kumlipa fidia mutahirika, lakini hatimae hakuna malipo.

‘’Ni kweli wakati umefika sasa kwa kuwepo kwa kifungu kipana cha sheria, kinachofafanua aina ya fidia, njia za kulipwa kwa haraka na isiwe kama ilivyo sasa, kuishia kwenye maandishi,’’alieleza.

Mama wa mtoto aliyebakwa mwaka 2022 na kisha kesi yake kutolewa hukumu mwezi Januari mwaka huu, alisema sasa ni miezi mitano, hajapokea fidia ya shilingi milioni 1.

‘’Niliambiwa kuwa, pamoja na mshtakiwa kufungwa miaka 20, alitakiwa anilipe fidia, lakini hadi sasa mwanangu anaendelea kuuguza maumivu, sijaona jambo lolote,’’alieleza.

Mzazi mwengine wa Mchanga mdogo, alisema katika kesi ya mtoto wake yenye namba 36/2022 ilihusisha kosa la kubaka, mshitakiwa ni Ali Hassan Hamad, alifungwa miaka 30 na kutakiwa kumlipa fidia ya shilingi 2,000,000, ingawa hadi sasa hajapokea.

‘’Ni kweli kama kunataka kufanyiwa marekebisho ya kifungu cha sheria, ni sawa maana, watoto wetu wanadhalilika mara mbili, ikiwemo kukosa fidia,’’alilalamika.

Aidha baba wa mtoto wa miaka 9, wa mkoa wa kusini Pemba, ambae alikuwa na kesi yenye namba 37/2022, kwenye kosa la kulawiti, mshitakiwa Masoud Khamis Mussa, alifungwa miaka 20 na kutakiwa kulipa fidia ya 1,000,000 ingawa naye, hajalipwa.



Wahanga hao walisema, adhabu inayotolewa kwenye mahakamani, zimekua haziwasaidii waathirika, bali huwaacha na maumivu, mara baada ya kesi kumalizika.

Mwanasheria wa serikali Mohamed Ali Juma, alisema bado kunachangamoto katika sheria zinazosimamia jinai, na kama hazikuangaliwa, zinaweza kuongeza changamoto.

‘’Kama mtoto ameshadhalilishwa, kisha kuna fidi hata hiyo ndogo haitoki, inakuwa ni shida, lazima sheria zibadilishwe na kuwe na fidia kubwa inayotolewa.

Naibu Mrajis wa Mahakama Kuu Pemba Faraji Shomar Juma, alisema ni wakati sasa, kuanzishwe kwa vifungu maalum vya kisheria, vitakavyoanzisha mfuko maalum wa wahanga wavitendo vya udhalilishaji.

Katibu wa Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar Mussa Kombo, alisema kwa sasa, maeneo hayo ndio wanayoyafanyiwa kazi, ili kuona kunakuwepo sheria maalum, ambayo itawasaidia waathirika wa vitendo vya udhalilishaji kupata haki zao.

“Maeneo hayo ndio tunayoyafanyia kazi na tunampango kazi wakukutana na wadau mbali mbali, ili tuone kasoro iko wapi na waathirika waweze kupata fidia zao,” alisema.

 Uchunguzu imebaini kuwa, kwa upande wa Mahakama mkoa wa Kaskazini Pemba, zipo kesi 11 zilitolewa hukumu, 10 zilitakiwa kulipwa fidia na zote hazijalipwa.

Wakati hayo yakifanyika, sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, kifungu cha 109 (1) cha sheria hiyo, kimebainisha kuwa, mshitakiwa akitiwa hatiani pamoja na adhabu atakayopewa, pia mahakama imtake alipe fidia kwa kiwango ambacho, mahakama itaona inafaa.



Kifungu cha 313 (1) (2) na kifungu cha 314 vya sheria ya mwaka 2018 sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, kinailazimisha mahakama itoze fidia kwa muathiriwa, baada ya kuombwa au bila ya kombwa na Mwendesha Mashtaka.

                     MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch