Skip to main content

MAJAJI WAMALIZA KAMBI KUSIKILIZA RUFAA ZA MWAKA 2018 PEMBA


NA ZUHURA JUMA, PEMBA:::


MAJAJI wawili wa mahkama kuu Zanzibar, wamemaliza kambi ya mwezi mmoja kisiwani Pemba, iliyokuwa na lengo la kusikiliza kesi za rufaa, zikiwemo za jinai ambazo zimefikishwa mahakamani kuanzia mwaka 2018 hadi mwaka 2021.

Akizungumza na waandishi wa habari hizi, Naibu Mrajisi wa Mahkama kuu Pemba Faraji Shomari Juma alisema, baada ya uchunguzi mdogo uliofanywa na mahkama, uligundua kuwa kuna mrundikano mkubwa wa kesi za rufaa za mahkama kuu kisiwani humo.

Alisema, licha ya majaji kuwa na utamaduni wa kwenda Pemba kwa ratiba zao za kawaida kufuatilia kesi, lakini Jaji mkuu ameona ni vyema, kuwapeleka Pemba majaji wawili kwa muda wa mwezi mmoja, ili kupunguza kesi.

“Baada ya kuonekana kuna kesi nyingi ndipo Jaji Mkuu amewaleta majaji wawili, ambao walipiga kambi kwa muda wa mwezi mmoja, tunashukuru kesi nyingi zimeshatolewa maamuzi”, alisema.

Alieleza kuwa, wameona zipo rufaa zaidi ya 25 ambazo nyingine ni tangu mwaka 2018, jambo ambalo lilikuwa likiwatesa wananchi kutokana na kukaa kwa muda mrefu bila ya kupata haki zao.

“Kwa wananchi sasa wamekuwa na imani kubwa na mahkama kwa sababu kesi nyingi zimepatiwa hatia, hii ni mafanikio kwetu”, alisema.

Naibu huyo mrajisi wa mahkama kuu Pemba alisema, moja ya sababu zilizopelekea kuwepo kwa mrundikano huo, ni janga la corona, lililopelekea majaji kutofika kisiwani Pemba kuendelea na kesi zao.

“Lakini hata ufinyu wa bajeti wa kuwasafirisha majaji Pemba, nao ulikuwa sehemu ya kusababisha mrundikano huo, ambapo kwa sasa hali ya fedha imeruhusu, ndio maana wameletwa majaji hao”, alifafanua.

Katika hatua nyingine, aliwapongeza mawakili kwa ushirikiano waliouonesha kwa mahkama katika kupunguza kesi hizo licha ya kuwa ni za muda mrefu.

Hata hivyo amewashukuru wananchi kwa ushirikiano wao waliouonesha kwa kufika kwa wingi mahkamani, jambo ambalo limesaidia kesi hizo kupata hatia kwa haraka.

“Awali katika kipindi cha kuanzia Septemba 8 hadi 21 mwaka huu majaji hao walikuwepo kisiwani hapa kwa lengo la kushughulikia rufaa 47, ambapo walifanikiwa kumaliza kesi 35 na kubakia 12 tu”, alifafanua.


Akizungumza kwa njia ya simu, wakili wa kujitegemea Pemba Zahran Mohamed Yussuf, alisema kuja kwa majaji hao imekuwa ni faraja kwao, kwani haki inapocheleweshwa ni sawa na kukosekana.

‘’Haki inapocheleweshwa huwa kama iliyokosekana, kwani hata wananchi wanakata tamaa, lakini sasa kama majaji watakuwa na tabia hii ya kupiga kambi kama hii iliyofanyika, kwetu sisi mawakili wa kujitegemea itatusaidia kwa kiasi kikubwa,’’alieleza.

Mwanasheria dhamana wa Ofisi ya Mkurugenzi mashataka Mkoa wa kaskazini Pemba, Mohamed Ali Juma alisema, kuja kwa majaji hao kumezaa faraja, kwani mrudikano wa kesi mahakamani umepungua kwa kiasi kikubwa.

“Sisi ujio wa majaji wa kupiga kambi kwa muda mwezi mmoja Pemba, umesaidia kupunguza mrundikano wa kesi za rufaa, maana zipo nyingine tangu mwaka 2018 hazijaguswa,’’alisema.

Baadhi ya wananchi kisiwani Pemba, wamesema uamuzi uliofanywa Mahkama kuu ya kuwasafirisha majaji wawili kwa lengo la kusikiliza kesi ni jambo jema.

Majaji waliokuja kisiwani Pemba kuweka kambi kwa muda wa mwezi mmoja ni Abdull-hakim Ameir Issa na George Joseph Kazi, huku ikiwa tayari mwezi Disemba mwaka 2021, kisiwa hiki kilipata Jaji mkaazi Ibrahim Mzee Ibrahim.

                             MWISHO.

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch