Skip to main content

'THE FUTURE LIFE FOUNDATION' YAMWAGA MSAADA KWA WATOTO 320 PEMBA

 




NA ZUHURA JUMA, PEMBA::::

MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali amesema, jamii inapaswa kuweka mifumo na mipango imara ya kuondoa huzuni za watoto yatima kwa kuwapatia haki zao za msingi.

Alisema kuwa, watoto hao wamekuwa wakikumbana na kadhia mbali mbali ikiwepo kufanyiwa udhalilishaji, hivyo kuna haja ya kushirikiana pamoja katika kuhakikisha wanapata haki stahiki kama watoto wengine wanaoishi na wazazi wao.

Akikabidhi msaada wa mcehele kwa watoto 320 uliotolewa na taasisi ya kusaidia mayatima, wajane, watu wenye ulemavu na wasiojiweza (The Future Life Foundation), Mkuu huyo alisema, watoto yatima wanahitaji kusaidiwa kwa hali na mali ili wasiwe na huzuni katika maisha yao ya kila siku.



ā€œMara nyingi watoto yatima wanadhalilishwa katika familia zile wanazoishi, hivyo ili kuona hawaishi na huzuni, tuwasaidie wajihisi kama wapo sawa na watoto wenzaoā€, alieleza Mkuu huyo.

Aliishukuru taasisi hiyo kwa mambo wanayoyafanya kusaidia jamii na kusema kuwa atahakikisha anasaidia kutatua changamoto zinazowakabili, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa umeme katika shamba lao la mboga mboga.

ā€œTutafanya mpango kuona kwamba umeme unafika katika shamba hili, ili uweze kuwarahisishia kupata maji ya uhakika na muweze kupata faida ambayo ndio mnayowapatia mayatima wetuā€, alisema.



Aliwaomba wawazi na walezi wenye watoto yatima wajitahidi kuwalea vizuri watoto hao, kwani ni mkombozi wao hapa nduniani na kesho akhera.

Akisoma risala, Rais wa Jumuiya hiyo Sheikh Mbarouk Seif Salum alisema, katika taasisi yao wanasaidia watoto yatima, wajane, watu wenye ulemavu na wasiojiweza, kujenga visima, misikiti na kusaidia maskulini.

Alisema kuwa, watoto yatima ni watu wanaopata mitihani mikubwa katika jamii, hivyo kuna ulazima wa kushirikiana pamoja katika kuwatunza na kuwasaidia kwa kila hali.

ā€œWako ambao kwa makusudi wanafukuzwa, wananyanyaswa na kudhulumiwa haki zao ambazo zimewekwa kwa sheria za kiislamu, hivyo ni vyema na wao tukawajengea mazingira mazuriā€, alieleza.

Alisema kuwa, katika juhudi zao za kusaidia watoto hao wameanzisha kilimo cha mboga mboga katika shehia ya Mjiniole, ingawa wamekuwa wakipata hasara kutokana na kukosa umeme ambao ungewasaidia kupandisha maji na kumwagilia.

ā€œTunatumia jenereta kupandishia maji, jambo ambalo ni hasara kubwa kwa sababu kwa siku tunatumia mafuta ya shilingi 30,000, hivyo inapofika mavuno hatupati faida kubwa na kushindwa kuwasaidia mayatima wetuā€, alisema.



Alieleza kuwa, lengo la kuanzisha kilimo hicho ni kuhakikisha wanasaidia makundi hayo wakiwemo watoto yatima, ambapo katika shamba hilo waliekeza kiasi cha shilingi milioni 45, ingawa gharama zao bado hazijarudi, hivyo aliiomba Serikali kuiwasaidia zaidi ili malengo yao yafanikiwe.

Kwa upande wake sheikh Abdalla Mohamed Abdalla alisema, watoto yatima wamekuwa wakikumbwa na udhalilishaji wa aina mbali mbali katika jamii, kuna haja ya kulindwa na kusaidiwa.

ā€œBaadhi ya walezi wa watoto hawa, wamekuwa wakiwatesa sana kiasi kwamba muda wote wanajisikia unyonge, kwa hiyo iwapo tutashirikiana kuwasaidia tutafanikiwaā€, alifafanua.

Nae mshughulikiaji wa shamba hilo Ali Msanifu alieleza kuwa, shamba hilo wamelianzisha kwa ajili ya kupata fedha za kuwasaidia watoto yatima, hivyo wanahitaji kusaidiwa kutatuliwa changamoto zinazowakabili, ili waweze kuendesha shughuli zao za kila siku.

Mmoja wa wazazi wa watoto hao Maryam Mohamed Muhene aliishukuru taasisi hiyo kwa kuwapatia misaada mbali mbali, ambayo inawasaidia katika kutatua changamoto zao ndogo ndogo.

ā€œTulichokipata sio kidogo kwa kweli, tunawashukuru sana, Allah awawezeshe zaidi ili watupe misaada mara kwa mara, kwa sababu watoto yatima wana mahitaji kama watoto wengineā€, alisema mama huyo.

Hafla hiyo ya kukabidhi msaada kwa watoto yatima ulifanyika katika ukumbi wa Judo Gombani Chake Chake Pemba.

                                                      MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ā€˜ Mkapaā€™ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ā€˜ Makababu ā€™ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. ā€œBaada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,ā€™...

ā€¦ā€¦.SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ā€˜SUZAā€™ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...