Skip to main content

'THE FUTURE LIFE FOUNDATION' YAMWAGA MSAADA KWA WATOTO 320 PEMBA

 




NA ZUHURA JUMA, PEMBA::::

MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali amesema, jamii inapaswa kuweka mifumo na mipango imara ya kuondoa huzuni za watoto yatima kwa kuwapatia haki zao za msingi.

Alisema kuwa, watoto hao wamekuwa wakikumbana na kadhia mbali mbali ikiwepo kufanyiwa udhalilishaji, hivyo kuna haja ya kushirikiana pamoja katika kuhakikisha wanapata haki stahiki kama watoto wengine wanaoishi na wazazi wao.

Akikabidhi msaada wa mcehele kwa watoto 320 uliotolewa na taasisi ya kusaidia mayatima, wajane, watu wenye ulemavu na wasiojiweza (The Future Life Foundation), Mkuu huyo alisema, watoto yatima wanahitaji kusaidiwa kwa hali na mali ili wasiwe na huzuni katika maisha yao ya kila siku.



“Mara nyingi watoto yatima wanadhalilishwa katika familia zile wanazoishi, hivyo ili kuona hawaishi na huzuni, tuwasaidie wajihisi kama wapo sawa na watoto wenzao”, alieleza Mkuu huyo.

Aliishukuru taasisi hiyo kwa mambo wanayoyafanya kusaidia jamii na kusema kuwa atahakikisha anasaidia kutatua changamoto zinazowakabili, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa umeme katika shamba lao la mboga mboga.

“Tutafanya mpango kuona kwamba umeme unafika katika shamba hili, ili uweze kuwarahisishia kupata maji ya uhakika na muweze kupata faida ambayo ndio mnayowapatia mayatima wetu”, alisema.



Aliwaomba wawazi na walezi wenye watoto yatima wajitahidi kuwalea vizuri watoto hao, kwani ni mkombozi wao hapa nduniani na kesho akhera.

Akisoma risala, Rais wa Jumuiya hiyo Sheikh Mbarouk Seif Salum alisema, katika taasisi yao wanasaidia watoto yatima, wajane, watu wenye ulemavu na wasiojiweza, kujenga visima, misikiti na kusaidia maskulini.

Alisema kuwa, watoto yatima ni watu wanaopata mitihani mikubwa katika jamii, hivyo kuna ulazima wa kushirikiana pamoja katika kuwatunza na kuwasaidia kwa kila hali.

“Wako ambao kwa makusudi wanafukuzwa, wananyanyaswa na kudhulumiwa haki zao ambazo zimewekwa kwa sheria za kiislamu, hivyo ni vyema na wao tukawajengea mazingira mazuri”, alieleza.

Alisema kuwa, katika juhudi zao za kusaidia watoto hao wameanzisha kilimo cha mboga mboga katika shehia ya Mjiniole, ingawa wamekuwa wakipata hasara kutokana na kukosa umeme ambao ungewasaidia kupandisha maji na kumwagilia.

“Tunatumia jenereta kupandishia maji, jambo ambalo ni hasara kubwa kwa sababu kwa siku tunatumia mafuta ya shilingi 30,000, hivyo inapofika mavuno hatupati faida kubwa na kushindwa kuwasaidia mayatima wetu”, alisema.



Alieleza kuwa, lengo la kuanzisha kilimo hicho ni kuhakikisha wanasaidia makundi hayo wakiwemo watoto yatima, ambapo katika shamba hilo waliekeza kiasi cha shilingi milioni 45, ingawa gharama zao bado hazijarudi, hivyo aliiomba Serikali kuiwasaidia zaidi ili malengo yao yafanikiwe.

Kwa upande wake sheikh Abdalla Mohamed Abdalla alisema, watoto yatima wamekuwa wakikumbwa na udhalilishaji wa aina mbali mbali katika jamii, kuna haja ya kulindwa na kusaidiwa.

“Baadhi ya walezi wa watoto hawa, wamekuwa wakiwatesa sana kiasi kwamba muda wote wanajisikia unyonge, kwa hiyo iwapo tutashirikiana kuwasaidia tutafanikiwa”, alifafanua.

Nae mshughulikiaji wa shamba hilo Ali Msanifu alieleza kuwa, shamba hilo wamelianzisha kwa ajili ya kupata fedha za kuwasaidia watoto yatima, hivyo wanahitaji kusaidiwa kutatuliwa changamoto zinazowakabili, ili waweze kuendesha shughuli zao za kila siku.

Mmoja wa wazazi wa watoto hao Maryam Mohamed Muhene aliishukuru taasisi hiyo kwa kuwapatia misaada mbali mbali, ambayo inawasaidia katika kutatua changamoto zao ndogo ndogo.

“Tulichokipata sio kidogo kwa kweli, tunawashukuru sana, Allah awawezeshe zaidi ili watupe misaada mara kwa mara, kwa sababu watoto yatima wana mahitaji kama watoto wengine”, alisema mama huyo.

Hafla hiyo ya kukabidhi msaada kwa watoto yatima ulifanyika katika ukumbi wa Judo Gombani Chake Chake Pemba.

                                                      MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch