Skip to main content

WANANCHI PEMBA WAONESHWA NJIA KUJIKINGA 'TB'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

WANANCHI kisiwani Pemba, wametakiwa kuendelea kuchukua hatua za kuchunguuza afya zao mara kwa mara, ili wajielewa ikiwa wanaishi na vimelea ambavyo vinaweza kusababisha ugonjwa wa kifua kikuu ‘TB’.

 

Ushauri huo umetolewa na mtaalamu kutoka kitengo shirikishi cha maradhi ya ukoma, kifua kikuu na Ukimwi Zanzibar, Said Khamis Ahmada, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi.

 

Alisema, moja ya njia ya kujikinga ama kuwahi matibabu ya ugonjwa huo, ni kuwa na tabia ya kuchunguuza afya mara kwa mara, ii upatikane ufumbuzi kwa wataalamu wa afya.

 

Alieleza kuwa ugonjwa wa kifua kikuu kitaalamu unaoitwa (‘Tuberculosis’ TB) ni miongoni mwa magonjwa 10 yanayosababisha vifo kwa wingi duniani kote.

 

Alifahamisha kuwa tafiti zilizofanywa na Shirika la Afya Ulimwenguni ‘WHO’ zinaonesha kuwa, inakisiwa watu milioni 10 wameugua ugonjwa huo, duniani kote, na hadi mwaka 2020, na kati ya hao watu milioni 1.5 wamefariki dunia.

 

‘’Utafifi huo ukagundua kuwa, kwa Zanzibar inakisiwa kuna wagonjwa 124 katika kila watu 100,000 ambapo hii ni sawa na wagonjwa 1, 612 kwa mwaka, hivyo nasi hatuko salama,’’alifafanua.

 

Katika hatua nyingine mtaalamu huyo, alibainisha kuwa, hadi mwaka 2021, Zanzibar kuligundulika wagonjwa 1, 090 ambapo hao ni sawa na asilimia 68, na vifo vilikuwa swa na asilimia sita katika mwaka 2020.

 

Kwa upande wake Mratibu wa Kikfua kikuu na Ukoma kanda wa Pemba Dk. Hamad Omar Hamad, alisema moja ya dalili za za ugonjwa huo ni kikohozi cha muda mrefu kuanzia wiki 2 au zaidi.

 

Alieleza kuwa, dalili nyingine ni kukohoa makohozi ambayo wakati mwengine huchanganyika na damu, ambayo huanza mapesi mepesi mfano wa mafuta ya nazi na kisha kuwa mazito mfano wa mafua mapevu.

 

‘’Hata kutokwa na jasho jingi wakati wote na hasa nyakati za usiku, hata kama hali ya hewa ni ya baridi, ambapo mtu huyo hushauriwa kufanya vipimo,’’alisisitiza.

 

Nae mtaalamu wa magonjwa ya kifua kikuu na ukoma kutoka kitengo shirikishi Zanzibar Valeria Rashid, anasema matibabu ya ‘TB’ huchukua kati ya miezi sita (6) hadi mwaka mmoja.

 

Ambapo anasema mgonjwa anatakiwa kula dawa chini ya usimamizi (nyumbani au kituo cha afya) kilichokaribu naye, ili kupata uhakika wa dozi vizuri.

 

Akizugumza hivi karibuni, ‘Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui anasema vituo vyote vya afya vya watu binafsi na serikali, vinatoa matibabu bila ya malipo, kwa wagonjwa wa TB.

 

‘’Ni fursa kwa wananchi kufanya uchunguuzi wa afya zao, na ikiwa wamegundulika na TB wanapewa matibabu bure katika vituo na hospitali zote za serikali na watu binafsi,’’anaeleza.

 

Meneja Mpango wa Shirikishi wa magonjwa ya Ukimwi, Kifua kikuu na Ukoma Pemba Khamis Hamad Khamis, alisema vyombo vya habari ni nyenzo pana ya kutoa elimu ya kupambana na magonjwa hayo.

             mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...