Skip to main content

MATAMU HAYA HAPA RIPOTI YA 'CAG' MASHIRIKA YA UMMA ZANZIBAR

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::::


MOJA ya mashirika ya serikali yaliotajwa kuongeza mapato yake, kupitia ripoti ya Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, ni Shirika la Umeme Zanzibar ‘ZECO’ lililongeza mapato yake, kutoka zaidi ya shilingi bilioni 33.579 mwaka 2019/2020, hadi kufikia zaidi ya shilingi bilioni 34.344 mwaka 2020/201.

Hayo yamebainika, kwenye ripoti hiyo ya mwaka 2020/2012, ambayo iliwasilishwa mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za serikali, Dk. Othman Abass Ali.

Ripoti hiyo imebainisha kuwa, kwa upande wa ZECO kulikuwa na ongezeko la zaidi ya shilingi milioni 764.207 sawa na asilimia 2, huku kwa mwaka 2020/2021, shirika hilo limepata faida ya zaidi ya shilingi bilioni 16.171, ikilinganishwa na faida iliyopatikana mwaka 2019/2021, ambayo ni zaidi ya shilingi bilioni 19.863 na upungufu ikiwa ni shilingi bilioni 3.692 sawa na asilimia 19.

Shirika jengine ambalo mapato yake yametajwa kuimarika ni kupitia ripoti hiyo, Shirika la Bima Zazibara ‘ZIC’ ambapo yameongezeka, kutoka zaidi ya shilingi bilioni 19.853 kwa mwaka ulioishia disemba 2019, hadi kufikia shilingi bilioni 20.020 kwa mwaka 2020.

Ripoti hiyo ikafafanua kuwa, ZIC kwa kipindi hicho, imepata faida ya shilingi bilioni 2.358 ikilinganishwa na faida iliyopatikana, kwa mwaka ulioishia 2019 ambayo ni zaidi ya shilingi bilioni 2.939 kukiwa na upungufu wa shilingi milioni 580.078 sawa na asilimia 19.7.

Kwa upande wa Shirika la Bandari Zanzibar ‘ZPC’ mwaka fedha 2020/2021, limepata mapato ya shilingi bilioni 39.897 kutokana vyanzo vya mapato, ikilinganishwa na makusanyo ya zaidi ya shilingi billion 34.848 kwa mwaka 2019/2020 kukiwa na ongezeko la shilingi bilioni 5.048.

Aidha ripoti hiyo ya Mkaguzi na Mdhibiti wa hesabu za serikali imeitaja Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar ‘ZSTC’ katika kipindi cha mwaka 2020/2021, limepata shilingi bilioni 11.217 ikilinganishwa na makusanyo ya shilingi bilioni 56.795 kwa mwaka 2019/2020, sawa na upungufu wa shilingi bilioni 45.577 sawa na asilimia 80.

Aidha shirika hilo linadai wakulima wa zao la karafuu shilingi milioni 7.005 kwa ajili ya mkopo wa zao hilo, ambapo ilikuwa kinyume na mkataba ya ukopeshaji uliofanyika.

Ambapo wa wilaya ya Chake chake ‘ZSTC’ wanawadai wakulima shilingi milioni 4,050,000, Wete shilingi 945,000, Micheweni shilingi 2010, 000 na wilaya ya Mkoani shilingi milioni 1.800 kuanzia mwaka 2011 hadi 2018.

Meneja wa Shirika la Umeme Zanzibar ZECO, tawi la Pemba Mohamed Juma Othman, amesema wamefarajika kuona kunaongezeko la mapato kwa shirika hilo.

Alisema, moja ya kichecheo cha kukuza mapato yao, ni kuondosha gharama za nguzo na kuwepo kwa mkopo wa huduma ya umeme kwa wananchi.

‘’Tunaendelea kujipanga ili kuhakikisha mapato ya ZECO yanaongezeka mara mbili, na vipo vijiji vyenye wastani wa nyumba 80 hadi 120 katika wilaya ya Micheweni na hata Mkoani hazijafikiwa na huduma yetu,’’alieleza.

Baadhi ya wananchi wakizungumza na mwandishi wa habari mjini Chake chake, wamesema kama mashirika yameongeza mapato, hakunabudi kuandaliwa mazingira zaidi ili kuimarisha kazi zao.

Hassan Omar Haji ambae ni mfanyabiashara wa chakula, alisema wakati umefika sasa kwa serikali, kuhakikisha hakuna shirika la serikali litakaloporomoka kimapato.

Nae Aisha Hilali Makame wa Mtambile, alisema kama mashirika yameongeza mapato, yake hakuna budi kuimarisha miradi na miundombinu ya jamii.

Kazija Himid Mohamed wa Mizingani alisema, anamatumaini makubwa na uongozi wa rais Dk. Mwinyi kuwa, kuongezeka huko kwa mapato, iwe chanzo za kuimarisha miundombinu.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa ripoti hiyo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alitaka wote waliotajwa kwenye ripoti hiyo kuchukuliwa hatua.
                             Mwisho

   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch