Skip to main content

NAIBU WAZIRI MAJI ZANZIBAR ASEMA YUKO TAYARI KUONESWA NJIA

 


Na Salma Lusangi 

NAIBU  waziri Wizara ya Maji, Nishati na Madini Zanzibar  Shabaan Ali Othman amesema uongozi wa wizara yake uko tayari kukosolewa pamoja  na kupokea maelekezo yaliyotolewa na kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, ili kuleta ufanisi katika  majukumu ya  wizara hiyo.

  Akizungumza katika kikao cha majumuisho kilichofanyika  jana katika ukumbi wa ZURA Maisara Zanzibar, baada ya kamati hiyo kumaliza ziara ya  kutembelea miradi ya umeme na maji kwa Unguja na Pemba ambayo  inatekelezwa na  WMNM, alisema wapo tayari kukosolewa kiutendaji  pamoja na kupokea ushauri ili kuleta ufanisi katika kuwahudumia  wananchi. 

 “Kwanza nawapongeza watendaji wote hasa nampongeza Katibu Mkuu Kilangi, kama wizara tumepokea maelekezo ya kamati,tutayatekeleza kama tulivyotumwa naomba kamati  isisite kutukosoa  zaidi naona kamati imetoa ushauri mzuri utatusaidia sana katika kutekeleza majuku yetu, tumeyapokea maelekezo yote” alisema Othman.

  Alisema wizara yake itaongeza kasi ya kufuatilia utekelezaji wa miradi ya Maji na Nishati pamoja na kuangalia upya mikataba ya wakandarasi kwa lengo la kumaliza miradi yote kwa wakati ili kuwaondolea shida wananchi.

 Naye Mwenyekiti wa kamati hiyo Abdallah Rashid Aballah ameitaka  WMNM kukamilisha miradi ya maji na umeme kwa wakati ili kutimiza  ahadi  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Mwinyi aliyowaahidi wananchi kuwafikishia  huduma ya maji na umeme mjini na vijijini.           


   Alisema   miaka mitano sio mengi, lazima ahadi za Mhe. Rais zikamilike kabla ya kufikia muda huo kwani wananchi bado wanalalamikia ukosefu wa kupata huduma ya maji.

 Alieleza kwamba kamati yake  imeshatoa maelekezo kwa changamoto walizoziona katika  Miradi ya Maji na umeme  ikiwemo kuwashirikisha  waakaazi wa eneo husika wakati wa kufanya  utafiti kabla ya kuanza  utekelezaji wa  mradi/ miradi ili kuepusha migogoro isiyonaulazima.

 Aidha amepongeza  ripoti na utekelezaji  wa miradi inayosimamiwa na WMNM kwani kamati imeona vifaa vya miradi ya umeme ambavyo vimenunuliwa na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) pamoja kuona maendeleo ya miradi ya Maji ikiwemo uchimbaji wa visima, ujenzi wa matangi na utandazaji wa mabomba ya maji kwa unguja na Pemba.

 Mapema katibu Mkuu WMNM  Joseph Kilangi aliwasilisha ripoti ya utekezaji wa wizara hiyo kwa kipindi cha Febuari hadi June ,2022 ikiwemo mafanikio na changamoto zilizowakabili katika utekelezaji wa miradi ikiwemo idadi ya visima vilivyofanikiwa kuchimbwa, pamoja changamoto za kiutalamu, vifaa vya miradi kuchelewa kufika kwa wakati hali ambayo ilisababisha baadhi ya miradi kusita kidogo kiutendaji.

  Alisema hivi sasa vifaa vingi vya miradi vimeshawasili nchini ikiwemo mita za umeme, mabomba ya maji , kokoto , saruji nk hivyo  kazi itaendelea kwa kasi zaidi kwasababu  watendaji wa wizara yake wanafanya kazi kwa mashirikiano ya karibu ili kuleta ufanisi zaidi.



  Kwa Upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Maji ( ZAWA) Mhandisi Dkt Salha Mohammed Kassim alisema  wanafanya kazi kwa usimamizi mkubwa bali amekabiliwa na changamoto ya  ukosefu wa watalaam hivyo wakati mwengine anahitaji  kuazima wahandisi na mafundi kutoka Tanzania Bara ili kuongeza kasi ya utendaji.

  “Naomba Serikali kuekeza nguvu ya elimu kwa vijina katika fani ya Mechanical engineer, Civil engineer na Electrical engineer  kwani wakati mwengine huwa na lazimika kuomba  wataalamu kutoka Tanzania bara kwasababu nimetafuta hapa Zanzibar nimekosa” alisema Mhandisi Dkt Salha.
                         Mwisho


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch