Skip to main content

ITATUENI MIGOGORO YA MADAI MSIKIMBILIE MAHAKAMANI: SEARCH

 


JAMII Kisiwani Pemba, imetakiwa kuwa na mwamko wa kujua kuwa, jukumu la utatuzi wa migogoro kwa makosa ya madai, kwa njia ya amani ni lao wenyewe kabla ya kufika katika vyombo vya sheria.


Kauli hiyo imetolewa na mwakilishi wa taasisi ya foundation for civil society Khamis Abass katika kikao cha kubadilishana mawazo, na kuandaa mikakati itakayosaidia kuondowa changamoto zilizojitokeza katika hatuwa za awali za utekelezaji wa mradi wa 'Dumisha amani Zanzibar' kilichofanyika shehia ya Ngwachani Wilaya ya Mkoani Pemba.

Alisema katika utekelezaji wa mradi huo kumeweza kuibuliwa migogoro mingi ikiwemo ya ardhi, ndoa, siasa, na mengine ambayo inaweza kusuluhishwa kwa kukaa pamoja wanajamii wenyewe.

Alifahamisha kuwa, ukosefu wa amani unatokea baada ya jamii kutokuwa na mazungumzo ya pamoja pale baada ya kutokezea migogoro hasa yale ya madai.

"Iwapo jamii itaipa nafasi migogoro kutawala ni wazi kuwa amani itakuwa tunu na wakati huohuo shughuli za kimaendeleo ziakosekana",alisema.

Mapema akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mradi huo Mratibu Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, alisema bado kuna changamo za ushirikishwaji mdogo kwa wanawake na watu wenye ulemavu, katika ngazi za maamuzi.

Aidha aliwaasa wanawake kushiriki katika vikao vinavifanywa kupitia shehia zao, kwani kufanya hivo kitasaidia kuongeza idadi ya ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi.

Akitaja mikakati ya kamisheni ya ardhi itakayopunguza migogoro ya ardhi kwa jamii, mwanasheria kutoka kamishemi hiyo Asha Suleiman Said, alisema ni pamoja na kutoa elimu kwa jamii katika kujua umuhimu wa hati miliki na vipi wanaweza kuipata.



Wakati huo huo aliwataka wanajamii kurithi mali zao kupitia taasisi ya wakfu na mali ya amana na kuepusha kugaiana ardhi bila utaratibu ili kuepusha migogoro hapo baadae.

"Jamii tufahamu kuwa ardhi haigawiwi na unapompa mtu ardhi kwa muda wa miaka 12 bila usumbufu kisheria huyo ndio mmiliki husika wa ardhi hiyo"alisema.

Akichangia mada Asha Hamad kutoka shehiya ya Ngwachani alisema chanzo cha migogoro mingi ya ardhi ni usumbufu kutoka kwa watendaji, katika kupima na kutoa kibali hivyo ni vyema kwa taasisi husika kujitahidi kuifikia jamii pindi anapohitaji msaada huo.

Issa Nassor Mohamed na Said Mohamed Ali wameiomba taasisi ya foundation for civil society  kuendeleza juhudi za utoaji wa elimu, kuanzia ngazi za chini katika jamii ili kuepusha migogoro na kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi.

Mradi wa Dumisha amani Zanzibar umeanza mwaka 2021 na umetekelezwa kwa muda wa miezi 18 kupitia taasisi ya Search For Common Ground na Foundation For Civil Society lengo ni kuisaidia jamii katika utatuzi wa migogoro na kudai haki kisheria.

                                                    Mwisho


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...