Skip to main content

WATAALAMU ECD PEMBA WATAJA ATHARI ZA KUINGILIA FARAGHA MTOTO

 



NA HAJI NASSOR,  PEMBA

WAZAZI na walezi visiwani Zanzibar, wametakiwa kutoingilia kimabavu, faragha za watoto wao, kwani kufanya hivyo, kunaweza kuwa chanzo cha ukosefu wa nidhamu kwao, katika maisha yao ya baadae.

Ushauri huo umetolewa na wataalamu wa malezi na makuzi ya kisayansi ya awali ya watoto ‘SECD’ kisiwani Pemba, wakati wakizungumza na mwandishi wa habari, juu ya dhana ya faragha kwa watoto wadogo.

Walisema, suala la faragha na umri wa mwanadamu halina uhusiano wowote, hivyo watoto kama walivyo watu wazima, hawatakiwi kubugudhiwa na kuingiliwa kimabavu faragha zao.

Mmoja kati ya wataalamu hao, Rashid Said Nassor, alisema faragha hata ya mtoto mdogo, mzazi, mlezi au mtu mwengine, hatakiwi kuiingilia, kwani kufanya hivyo ni kumvunjia haki zake.

Alieleza kuwa, mtoto ni mwanadamu kama walivyo wengine, hivyo anaowakati hujiweka kwenye faragha yake, na kufanya mambo yake binafsi, na mzazi au malezi hatakiwa kumyima uhuru huo.

‘’Mtumzima gani ambae anafurahia anaponyimwa haki yake ya faragha, bila shaka hakuna, basi na hata kwa mtoto, nae anayohaki ya faragha na haitakiwi kuingiliwa kiholela na mtu yeyote,’’alieleza.

Nae mtaalamu wa malezi hayo ya kisayansi na makuzi ya awali ya mtoto ‘SECD’ Omar Mohamed Ali, alieleza kuwa suala la kila mmoja kuwa na faragha yake iliyohalali, halitakiwi kuingiliwa wala kutikishwa na mtu mwengine.

‘’Ndio maana, hata vipo vyombo vya habari vimeshashtakiwa kwa kuingilia faragha za watu, vivyo hivyo kwa wazazi na walezi wasiangalie umri wa watoto wao na kuingilia faragha zao,’’alishauri.

Hata hivyo, alisema katazo hilo halimzuii mzazi kumfundisha malezi na makuzi yenye maadili mtoto wake, au kumzuia kushiriki kwenye vikundi viovu, bali kinachokatazwa, ni kuingia faragha yake halali pasi na sababu ya msingi,’’alieleza.

Nae Khadija Omar Haji, anasema kitaalamu watoto huwa na muda wa kujiweka pahala peke yao, na kufanya shughuli zao binafsi za halali, mfano kulala, kufikiria jambo au kuangalia burudani isiyoharibu maisha yake.

‘’Wazazi na walezi hawana haki ya kuvuruga wala kuingilia uhuru wa faragha wa watoto wao, maana ukuaji wa ubongo unahitaji mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na heshima ya awali,’’alieleza.

Nae muuguzi wa mama na mtoto wa Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani, dok. Rabia Mohamed, alisema faragha ya watoto ni sehemu ya kibailojia inayompa nafasi, kukuza ubongo wake.

Msimamizi wa kitengo cha lishe Wilaya ya Chake Chake, Harusi Masoud Ali, alieleza kuwa, mtoto baada ya kushiba huhitaji kupata faragha ya kujipumzisha, ili kukipa nafasi chakula kusagika kwa urahisi.

‘’Kama alivyomtu mzima anahitaji kuthaminiwa na kuenziwa kwa uhuru wake wa faragha, na vivyo hivyo watoto wetu wanahitaji uhuru huo kwa upana zaidi,’’alifafanua.

Meneja ‘ECD’ tasisi ya Maendeleo ya binadamu kutoka Chuo Kikuu cha Aga Khan, Mombasa Joyce Marangu, alisema huduma za wazazi kwa mtoto wao, ni pamoja na kutii uhuru wa watoto wao.

Mkuu wa wilaya ya Mkoa Khatib Juma Mjaja, alisema endapo wazazi na walezi watathamini uhuru wa faragha kwa watoto wao, watakua katika malezi na makuzi hayo, nao kufikia kuwaheshimu wengine.

Wazazi Khadija Haji Khamis, Wahidi Omar Kassim na Maua Othman Ziadi wa mji wa Chake chake, walisema wamekuwa hawatambui hilo, na kuona mtoto hana haki hiyo.

Mwanasheria dhama wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kisiwani Pemba Ali Haidar, alisema sheria ya mtoto ya Zanzibar nambari 6 ya mwaka 2011, imetambua uhuru wa faragha kwa watoto.

‘’Ukiangalia katika sheria hiyo moja ya haki za mtoto ni pamoja na wazazi au walezi, wanawajibu wa kuheshimu faragha ya watoto na kutambua utu wao na ulinzi kamili,’’alieleza.

Wataalamu wa malezi ya kisayansi, makuzi na uchangamshi wa mtoto kwa hatua za awali ‘SECD’ wametaja njia tano ambazo familia ikizifuata, itakuwa ni chac hu ya ukuaji wa ubongo wa matoto, ikiwa ni pamoja na kumpa uhuru wa kuchangamana na wenzake.

Nae sheikh Ramadhan Mohamed wa Chake chake, alisema dini inatambua hilo, na ndio maana imewaelekeza waumini kutaja jina la muumba mara mtoto anapozaliwa.

Mchungaji wa kanisa la KKKT Chake chake Benjamen Kissanga, alisema maandiko yako wazi na kuwa yataka kila mtu kwa utu wake aheshimiwe pasi na kuangali umri.




Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch