Skip to main content

KUNDI LA VIIZIWI LIANZE SASA KUTENGENEZEWA MAZINGIRA YA KUPATA TAARIFA UCHAGUZI MKUU UJAO

                                                                

PICHA NA MTANDAO SIO HALISI YA VIZIWI


NA HAJI NASSOR, PEMBA

ULEMAVU ni upungufu wa uwezo wa viungo vya mwili, akili au hisi unaomsababishia mtu, kushindwa kumudu mazingira yake au kushindwa kushiriki kikamilifu katika kazi za kijamii.

Ndivyo ilivyoa toa tafsiri ya nini maana ya ulemavu, sheria ya watu wenye ulemavu (haki na fursa ) ile namba 9 ya mwaka 2006 ya Zanzibar ielezavyo.

Sheria hii ikaenda mbali zaidi na kufafanua kuwa, ulemavu unaweza kuwa wa kudumu au wakati mwengine ni wa muda, huku baadhi ya magonjwa kama vile ya akili yanaweza kusababisha ulemavu pia.

Tendo la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutunga sheria hii, ni kuona umuhimu na ulazimu ule uliomo kwenye katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kwamba binadamu wote ni  sawa mbele ya sheria.

Kumbe, serikali ilililia sana kundi la watu wenye ulemavu, na sasa najifunza kwamba, hata yule au mimi na wale, leo wanaviungo kamili, kesho wakipungikiwa, basi wamekuwa walemavu. 

Sheria hii ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar, ambao wenyewe walioutungiwa wakisema kwamba, inakidhi haja  kwa baadhi mambo, imejumuisha vifungu 48 lakini kifungu cha 15 ni kizuri.


Chenyewe kimeelezea suala la mawasiliano kwa kundi hili,  bila ya kujali aina ya ulemavu, kwamba serikali iwatekelezee, ili nao wawe sawa kwenye upatikanaji wa taarifa, kama kundi jengine.

Tena ukikichambua kifungu hichi kidogo cha (a), kimeainisha aina ya silabi ambazo zitatumika, kwamba ni  maandishi ya nukta nundu, huduma za kanda zilizorikodiwa  taarifa kwa maandishi makubwa.

Lakini hata wapatiwe huduma za kutafsiri, wasaidizi na waongozaji na lugha ya alama, imetajwa kwenye kifungu kidogo cha (d), naamini lengo ili nao waende sambamba  katika upatikanaji wa taarifa hasa za umma.

Chakufurahisha na chakutia moyo katika kifungu cha 25 cha  sheria hii, kimeeleza kwamba, lazima vituo vya kupigia kura, ikiwa ni haki ya kikatiba, vitengenezwe ili waweze kuvitumia.

CHAGUZI ZA VYAMA VINGI

Kwa mfano Tanzania na Zanzibar wameshaendesha  changuzi sita za vyama vingi nchini, lakini kundi la viziwi linaendelea kukosa taarifa rasmi.

Wanasema mchakato wa uchaguzi sio siku ya kupiga kura tu pekee, bali huanzia tokea uandikishaji na kisha upachikaji majina kwenye vituo.

Tena kwenye kundi hili, mpaka wenye ulemavu wa usikivu (viziwi) walishiriki, ingawa wenyewe wanalilia kutotekelezwa ipasavyo sheria yao namba 9 ya mwaka 2006, juu ya upatikanaji wa taarifa kwa mujibu wa mazingira yao.


Kubwa wanasema, walianza kutengwa kwa kukosa taarifa tokea hatua za uandikishaji, uchaguzi wa wagombea ndani ya vyama, kampeni na kisha tukio kubwa la kupiga kura.

Wanasema kwenye vituo vya kupiga kura, Tume za uchaguzi za ZEC na NEC walishindwa kuwawekea wakalimani, ili kuwapa taarifa za kituo wanachopaswa kwenda ili kupiga kura.

Walitarajia sana, kama walinyimwa haki ya kufahamu kinachoendelea wakati wa kampeni, kwa kukosekana wakalimani, walau kwenye vituo kwa siku ya kupiga kura wengekuwepo.

Hidaya Mjaka Ali ambae anasimamia miradi ya watoto kutoka Umoja wa watu wenye Ulemavu Zanzibar ‘UWZ’ anasema alipokea malalamiko toka kwa wanachama wao, juu ya kukosa taarifa sahihi.

“Ni kweli wenzetu viziwi kwenye uchgauzi mkuu uliofanyika, waliachwa nyuma maana ile sheria yetu, kwenye kifungu cha 15 ya kupewa taarifa ikutekelezwa,’’alilalamika.

Yeye anasema, inawezekana kukosekana kwa wakalimani ni jambo lililofanywa kwa maksudi, maana hiyo haikuwa ni fursa bali ni haki kwa mujibu wa sheria, iliyopitishwa na baraza la wawakilishi mwaka 2006.

Bilali Mohamed Bilali Katibu wa Jumuiya ya wasioona wilaya ya Wete, ingawa kwa upande wao hakukuwa na mashaka makubwa, lakini kwa ndugu zao viziwi walikosa haki ya taarifa.


“Viziwi ni kweli walikosa mtu wa kuwapa taarifa sahihi kwenye vituo vya kupigia kura, ingawa sheria inasema kila mmoja apate taarifa za mawasiliano,’’alisema.

Asha Hilali Juma (kiziwi) wa Wete, akizungumza nami chini ya mkalimani wake, anaona vituo vya kupigia kura havikuwa rafiki kwao, kutokana na ulemavu wa usikivu walionao.

“Nilipofika sikukaa kwenye foleni, lakini sijui wapi jina langu lipo, na niliokuwa nikizungumza nao hawaelewi, maana mimi natumia lugha ya alama ’’,alilamika.

Lakini Ali Ali Makame wa Mkoani mweye ulemavu wa uziwi, alichokifurahia kwenye uchaguzi wa mwaka jana, ni kupewa kitambalisho maalum.

Anasema hicho kilimfanya asipange foleni, ingawa alipata tabu kujua chumba chake cha kupigia kura.

“Kila ninae muuliza kiwapi chumba changu cha kupigia kura kwa lugha ya alama, ananisemesha kama mimi sio kiziwi, kisha nikarudi nyumbani bila ya kupiga kura’’,alisema.

Baada ya kukaa zaidi ya saa moja kwenye kituo, aliamua kurudi nyumbani, bila ya kuitumia haki yake ya kupiga kura, baada ya kutokuwepo mkalimani kituoni.

Ingawa Mwanajuma Kombo Hija wa Kengeja Mkoani ambaye nae kiziwi, kwamba alifanikiwa kupiga kura, baada ya kuhangaika.

“Walikua wananifanya kama runinga, kisha wananicheka maana wao wananisemesha kama vile mimi sio kiziwi, sasa ilikuwa tabu,’’alifafanua.


Aliyekuwa Afisa wa tume ya Uchaguzi ZEC Pemba, Ali Mohamed anasema isingewezekana kwamba kila kituo kimoja awepo mkalimani, maana hilo halikupangwa.

“Sisi kama ZEC tumejitahidi walau kwepo kwa kifaa maalumu kwa wasioona, ili waweze kupiga kura kwa uhakika, jambo ambalo chaguzi zote walikuwa wakipigiwa’’,alisema.

Mkalimani wa lugha ya alama Pemba Asha Suleima, anakubali kuwa uchaguzi mkuu uliomalizika hivi karibuni Zanzibar, kundi la viziwi hawakupata taarifa sahihi za umma.

“Mimi ni mkalimani, lakini haikuwezekana kwenda kila jimbo ili kuwasaidia wenzetu hawa, sasa lazima serikali ijipange, ili kuhakikisha viziwi wanapata tarifa kwa uchaguzi mkuu ujao mwaka 2025’’,alishauri.

Mratibu wa Kituo cha huduma za sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, akizungumza katika moja ya makongamano, alishauri lazima sheria zitekelezwe.

“Zanzibar tunaongoza kwa kuwa na sheria nyingi na mzuri, lakini ubaya wake unakuja kwenye utekelezaji, maana hata hii ya watu wenye ulemavu, kama ikitelezwa, basi ubora wake utaoonekana’’,alisema.

Yeye anaona ili sheria ionekane kama mzuri au inamapungufu lazima itumike “tested” na kinyume chake itakuwa kama nyumba iliojengwa pasi na kuhamiwa.

Taasisi mbali mbali za Zanzibar kama vile Chama cha waandishi wa habari Tanzania TAMWA -Zanzibar kabla ya  kuingia kwenye ngwe ya kuchagua, ilitoa mafunzo kadhaa kwa kundi la watu wenye ulemavu.

Akisisitiza jambo katika moja ya mafunzo hayo Mratibu wa TAMWA Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, aliziomba tume zinazosimamia uchaguzi, kuhakikisha hakuna kundi la binadamu lenye sifa ya kuchagua au kuchaguliwa, kudhalilishwa kikatiba.

“Hata unapowakosesha wakalimani wenzetu viziwi ni aina nyengine ya udhalilishaji wa kidemokrasia, maana inawezekana wasipate haki ya kumchagua kiongozi kwa mujibu wa sera zake kwa kule kukosa taarifa sahihi’’,alisema.

Lakini hata Shirika la Internews Tanzania, ambalo liliwawezesha waandishi wa habari kimafunzo, ili kuandika habari na kutayarisha vipindi ambavyo vitawakumbusha wenye mamlaka kuwapa haki za wau wenye uziwi.

“Nyinyi waandishi wa habari lazima muziambie mamlaka husika, juu ya hawa wenzetu wenye ulemavu wa viziwi, kwamba, lazima wapatiwe haki zao hasa za kuwepo wakalimani kwenye mikutano na vituo vya kupigia kura’’,alisema mkuu wa Program wa Internews Shaaban Maganga.

Lakini hata aliyewahi kuwa mkufunzi kutoka shirika hilo Ofisi ya Zanzibar Ali Haji Mwadini, alisisitiza haja kwa waandishi wa habari kuandika habari za juu ya haki za kundi la watu wenye ulemavu.’


Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu Zanzibar ‘SHIJUWAZA’ Mwandawa Khamis Mohamed, amesema moja ya changamoto kubwa ni kundi la viziwi kukosa taarifa za umma.

Mjumbe wa baraza kuu la viziwi Zanzibar Mohamed Khamis, alisema bado wamekuwa wakifuata mkubo katika kila chaguzi kwa kukosekana mkalimani.

Aidha Said Khatibu kiziwi wa Mtemani Wete, anasema zisipotekelezwa sheria zao ipasavyo, ni kuongezewa unyonge katika taifa.

Mkurugenzi wa baraza la taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar mwalimu Ussi Khamis, alisema jamii inapaswa kusimamia haki za watu wenye ulemavu kikamilifu.

Mtendaji mkuu wa Shirikisho la Jumuiya za watu wenye ulemavu taifa Tanzania, Ernest Kimaya, anasema lazima tume za uchaguzi ziwajali viziwi.

“Viziwi ni jamii ya watu kama walivyo wengine, hivyo lazima uimarishaji kwa chaguzi zijazo ufanyike ili wapate taarifa zaote za mwenendo wa uchaguzi mkuu,’’anasema.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch