Skip to main content

Kigwangallah: Sihongeki na Wala Sipo Tayari Kuuza Utu Wangu Kisa Umasikini na Tamaa

Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kigwangalla amesema ataendelea kuwepo ndani ya wizara hiyo kama kilichowafanya watangulizi wake kuondoka ni masilahi binafsi, kwa kuwa hahongeki, hashawishiki na aliyemteua analifahamu hilo.


Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kigwangalla amesema ataendelea kuwepo ndani ya wizara hiyo kama kilichowafanya watangulizi wake kuondoka ni masilahi binafsi, kwa kuwa hahongeki, hashawishiki na aliyemteua analifahamu hilo.

 “Sitakuwa tayari kupoteza heshima yangu, aliyeniteua anajua kuwa mimi ni muarobaini wa hayo yote, hata nilipoteuliwa walianza kunidhihaki kupitia mitandao ya kijamii kuwa ninakwenda kuharibikiwa huko, eti kwa sababu mawaziri hawadumu, haipo hiyo,” alisema Dk Kigwangalla jana Jumapili Oktoba 22,2017 mjini Dodoma.

Alisema hayo akijibu kauli ya Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro aliyemtahadharisha kuwa mawaziri wamekuwa hawadumu ndani ya wizara hiyo kutokana na kununulika na wadau kwa kuwa kuna ushawishi mwingi.

Hayo yameibuka kwenye mkutano wa wadau wa sekta mbalimbali zinazofanya kazi na Wizara ya Maliasili na Utalii ambao Dk Kigwangalla alikutana nao akiwa na Naibu Waziri wake, Japhet Hasunga.

Katika mchango wake, Meya Lazaro alisema, “Niliwahi kumtahadharisha waziri mwenzako Hamisi Kagasheki kuwa hatadumu katika wizara hiyo kutokana na wadau kuwa na vishawishi vingi, leo hii naomba kukuambia kuwa sheria hizo mnazosema kuwa ni mbovu si kweli bali zinakosa usimamizi wa kutosha kwa sababu ya masilahi ya watu.”

Meya Lazaro alimtaka waziri kukutana na kila sekta ili kusikiliza kilio chao akisema ndani ya wizara hiyo kama atapatikana mtu wa kuisimamia vizuri inaweza kutoa mchango mkubwa ambao haujapata kutokea lakini akaahidi kuwa watamsaidia ili adumu kuliko mawaziri wengine.

Alisema “Napenda uendelee kubaki katika wizara hii, wewe ni kijana mdogo nisingependa uwe geti la kutokea.”

Mawaziri waliowahi kuiongoza wizara hiyo ni Anthony Diallo (2005-2006), Profesa Jumanne Maghembe (2007-2008; 2016-2017), Shamsa Mwangunga (2008-2010), Ezekiel Maige (2010-2012), Balozi Hamis Kagasheki (2012-2013) na Lazaro Nyalandu (2014-2015).

Meya Lazaro alisema baadhi ya mawaziri wamekuwa wakiitwa na makundi mbalimbali akitoa mfano wa wawindaji na kuzungumza nao lakini hushawishika kuegemea huko na wakiitwa na watu wengine huegemea huko, hivyo kushindwa kubaki katikati ya sekta zote.

Akijibu hoja hiyo, Dk Kigwangalla alisema hana shaka ya aina yoyote kuhusu kupewa wizara hiyo.

Dk Kigwangalla aliwatahadharisha wadau akisema wanapofika ofisini kwake wajiandae vyema, vinginevyo anaweza kusimama na kumuacha mtu kama atagusa suala la rushwa.

“Mimi sihongeki, kwa hivyo siko tayari kung’oka kwa sababu yoyote ile, kama ni umasikini ni bora kufa njaa, kwangu fedha haiwezi kunitolea heshima licha ya kuwa wote tunazitaka,’’ alisema.

Waziri huyo amejisifu kuwa hata aliyemteua anajua yeye ni muarobaini, hivyo imani yake ni kubwa kwake na kwa upande wake hatakuwa tayari kuona akiharibikiwa njiani.


 “Sitakuwa tayari kupoteza heshima yangu, aliyeniteua anajua kuwa mimi ni muarobaini wa hayo yote, hata nilipoteuliwa walianza kunidhihaki kupitia mitandao ya kijamii kuwa ninakwenda kuharibikiwa huko, eti kwa sababu mawaziri hawadumu, haipo hiyo,” alisema Dk Kigwangalla jana Jumapili Oktoba 22,2017 mjini Dodoma.

Alisema hayo akijibu kauli ya Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro aliyemtahadharisha kuwa mawaziri wamekuwa hawadumu ndani ya wizara hiyo kutokana na kununulika na wadau kwa kuwa kuna ushawishi mwingi.

Hayo yameibuka kwenye mkutano wa wadau wa sekta mbalimbali zinazofanya kazi na Wizara ya Maliasili na Utalii ambao Dk Kigwangalla alikutana nao akiwa na Naibu Waziri wake, Japhet Hasunga.

Katika mchango wake, Meya Lazaro alisema, “Niliwahi kumtahadharisha waziri mwenzako Hamisi Kagasheki kuwa hatadumu katika wizara hiyo kutokana na wadau kuwa na vishawishi vingi, leo hii naomba kukuambia kuwa sheria hizo mnazosema kuwa ni mbovu si kweli bali zinakosa usimamizi wa kutosha kwa sababu ya masilahi ya watu.”

Meya Lazaro alimtaka waziri kukutana na kila sekta ili kusikiliza kilio chao akisema ndani ya wizara hiyo kama atapatikana mtu wa kuisimamia vizuri inaweza kutoa mchango mkubwa ambao haujapata kutokea lakini akaahidi kuwa watamsaidia ili adumu kuliko mawaziri wengine.

Alisema “Napenda uendelee kubaki katika wizara hii, wewe ni kijana mdogo nisingependa uwe geti la kutokea.”

Mawaziri waliowahi kuiongoza wizara hiyo ni Anthony Diallo (2005-2006), Profesa Jumanne Maghembe (2007-2008; 2016-2017), Shamsa Mwangunga (2008-2010), Ezekiel Maige (2010-2012), Balozi Hamis Kagasheki (2012-2013) na Lazaro Nyalandu (2014-2015).

Meya Lazaro alisema baadhi ya mawaziri wamekuwa wakiitwa na makundi mbalimbali akitoa mfano wa wawindaji na kuzungumza nao lakini hushawishika kuegemea huko na wakiitwa na watu wengine huegemea huko, hivyo kushindwa kubaki katikati ya sekta zote.

Akijibu hoja hiyo, Dk Kigwangalla alisema hana shaka ya aina yoyote kuhusu kupewa wizara hiyo.

Dk Kigwangalla aliwatahadharisha wadau akisema wanapofika ofisini kwake wajiandae vyema, vinginevyo anaweza kusimama na kumuacha mtu kama atagusa suala la rushwa.

“Mimi sihongeki, kwa hivyo siko tayari kung’oka kwa sababu yoyote ile, kama ni umasikini ni bora kufa njaa, kwangu fedha haiwezi kunitolea heshima licha ya kuwa wote tunazitaka,’’ alisema.

Waziri huyo amejisifu kuwa hata aliyemteua anajua yeye ni muarobaini, hivyo imani yake ni kubwa kwake na kwa upande wake hatakuwa tayari kuona akiharibikiwa njiani.


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch