Skip to main content

‘JUMWAMPE’ YAGUNDUA HAYA KWA WAKULIMA



NA HAJI NASSOR, PEMBA

KAMATI ya Ushawishi na Utetezi kutoka Jumuia ya mtandao wa wakulima wa matunda na mboga mboga Kisiwani Pemba JUMWAMPE, imesema imegundua changamoto kadhaa zinawazowakabili wakulima wao, ikiwa ni pamoja na kukosa elimu ya matumizi sahihi ya pembejeo za kilimo.

Kamati hiyo, ilipita kwa wakulima zaidi ya 100 kisiwani humo, na baada ya kuwajazisha dodoso maalum, waligundua kuwa wakulima hao, hawana elimu ya matumizi ya dawa za mimea, hali inayotishia usalama wao na walaji.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Chakechake mara baada ya kumalizika kwa safari ya kuwatembelea wakulima, Katibu wa Jumuia Mtandao huo Hamad Ali Mussa, alisema wapo waliowagundua kutumia dawa ya kuulia kunguni kwa kutumia kwenye mazao.

Alisema jengine waliloligua wakati wakiwa na wakulima hao, ni kutokuwa na kipimo sahihi cha kunyunyizia dawa hizo, kwenye mboga mboga zao, ambpo hupelekea muda mfupi baada ya kutia dawa kuvunwa na kuuzwa sokoni.

Katibu huyo alieleza kuwa, hilo pia linaweza kusababisha athari ya kimwili kwao, walaji na hata wanyama wanaowapa malisho, baada ya kumalizika kwa uvunaji.

“Huu tuliofanya sio utafiti hasa, ni kama tumewatembelea na kuonana nao, lakini utafiti hasa tutaufanya baadae, ili kugundua changamoto hasa zinazowakabili wakulima wetu na wafugaji, maana wao ndio tegemeo letu kwa ajili ya chakula”,alifafanua.

Makamu Mwenyekiti wa Jumuia hiyo Mtandao, Zainab Rajab Iddi, alisema kwenye msafara wao huo, piwa wamegundua baadhi ya wakulima hao, kutokuwa na uhakika wa matumizi ya maji, kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao.

Alieleza kuwa, wapo wanaolalamiki bili kubwa ya maji au kukatiwa maji na ZAWA, jambo ambalo wamesema linawarejesha nyuma, katika sekta hiyo walioichagua.

“Wapo waliolalamikia kuwa hukatiwa maji na ZAWA hata kama ndio kwanza mazao au mboga mboga zao hazijapevuka, hali ambayo huwakosesha mwendo wa kufikia maendeleo yao”,alieleza.

Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo ya ushawishi na utetezi kutoka ‘JUMWAMPE’ Saada Hamad Kombo, alisema  ambalo jengine walioligundua na kuamua kuitafuta sera ya kilimo, ni kuwepo kwa maduka ya wauza pembejeo bila ya mpangilio, hali inayosababisha na wakulima nao kununua wapendavyo.

Aliongeza kuwa, hilo linawapa shida wakulima, kwanza kununua dawa wasizozijua matumizia yake sahihi wala vipimo vyake, maana muuza pembejeo yeye anachotaka ni biashara yake iende tu, na sio kuangalia usalama wa anaemuuzia”,alifafanua.

Kufuatia safari hiyo ya kuwatembelea wakulima, Mjumbe mwengine wa Kamati hiyo, Hassan Shamis Hassan, alisema sasa wanachotarajia kukifanya, ni kuipitia kwa umakini sera ya kilimo, ili kuona inasemaje hasa kwa uingiaji, uuzaji na utumiaji wa pembejeo zenye kimikali.

“Ingawa pia tulishakwenda ZAWA na kupendekeza tuwe na mikatab, au wizara ya biashara na viwanda kuahidi kuzitangaaza biashara za wakulima wetu, lakini pia lazima serikali iangalie uwezekano wa kutupia macho biashara ya pembejeo”,alieleza.

Aidha kamati hiyo, imeshauri kuwepo kwa umakini mkubwa wa uingiaji wa pembejeo kisiwani Pemba, aina ya mbegu za matunda na mboga mboga, sambamba na kuwajengea uwezo mabibi na mabwana shamba, ili wakulima wapate utaalamu na ushauri wao wakati wote”,alifafanua.

Mkulima wa mboga mboga shehia ya Vitongoji wilaya ya Chakechake Mkubwa Ali Mkubwa, alisema kwake yeye kubwa analoliona linamrejesha nyuma ni ukosefu wa soko la uhakika.

Nae mkulima wa vitango, mchicha na tungule wa Vitongoji Mohamed Khamis Song, alisema hivi karibuni alikuwa na vitango 700 ambavyo alikosa soko la uhakika na kuviuza chini ya bei.

“Kitango kimoja nililazilimika kukiuza kwa bei ya shilingi ya 150 na shilingi 200, maana tulikosa soko la uhakika, sasa lazima serikali ituangalie sasa tumeshatekeleza agizo la kujikusanya pamoja”,alifafanua.

Jumuia Mtandao wa wakulima wa mboga mboga na matunda kisiwani Pemba ‘JUMWAMPE’ ambayo iliasisi tokea mwaka 2008 kwa kuanza mkoa wa kaskazini Pemba pekee, na sasa kuwa ya Pemba nzima, inadhamira ya kuwawezesha wakulima hao, ili wazalishe bidhaa zenye ubora na zinazokubalika sokoni.

                        

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch