Skip to main content

'THBUB' YAWAHIMIZA WAZAZI, WALEZI KUVUNJA UKIMYA DHIDI YA UDHALILISHAJI WA WATOTO


NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIBAR@@@@

AFISA Uchunguzi kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) Ofisi ya Zanzibar, Abdul-latif Ali Sheha amewasihi wazazi na walezi wa Shehiya ya Kinuni, kujenga utamaduni wa kuzilinda na kuziishi haki za watoto kwa vitendo.

Abdullatif alitoa nasaha hizo kwa wazazi na walezi 637 katika Madrasatul Thamaraatul Jannah iliyopo Shehia ya Kinuni, Mkoa wa Mjini Magharibi wakati akiwapa hao elimu ya haki za watoto na wajibu wa jamii katika kuzuia vitendo vya ukatili wa watoto na uvunjwaji wa haki za binadamu ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu na msaada wa sheria wakati wa mwendelezo wa zoezi la Kampeni ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia Awamu ya Pili (MSLAC II) unaoendelea katika Wilaya tatu za Mkoa wa Mjini Magharibi.

“Mtoto ana haki ya kuishi katika mazingira salama, kupatiwa elimu na kulindwa dhidi ya aina zote za unyanyasaji" Alisisitiza bw. Abdullatif.


Pia aliwaeleza wazazi hao kuwa jamii inapaswa kuachana na tabia ya kuoneana muhali katika kushughulikia matukio ya udhalilishaji. Sambamba na kuwahimiza wazazi hao kujenga utamaduni wa kuripoti mara moja matukio ya udhalilishaji kwa mamlaka za kisheria badala ya kuyamaliza kwa maelewano yasiyo rasmi au kuwalazimisha watoto wa kike kuolewa na watu wanaodaiwa kuwafanyia udhalilishaji.

Aliongeza kuwa hatua hizo humwongezea mtoto madhara ya kisaikolojia, humkatiza haki yake ya elimu na huathiri maendeleo yake ya baadaye.




Wakati huo huo kwa maeneo mengine tofauti ya Mkoa wa Mjini Magharibi Ofisa huyo wa THBUB Bw. Abdullatif, akishirikiana na maafisa wengine wa Sheria na Mawakili kutoka Wizara za Katiba na Sheria za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kwa ushirikiano na Maofisa kutoka Jeshi la Polisi kanda ya Zanzibar waliwafikia wanafunzi wengine 465 na walimu wa Madrasa tatu zilizomo ndani ya Mkoa huo zikiwemo "Madrasatul Answaar", "Madrasatul Fatma Islamia" na "Madrastul Nurrul Islamiyya" katika kutoa msaada wa kisheria na elimu ya haki za binadamu wakti wa mwendelezo wa  Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili (MSLAC II) inayoendelea visiwani Zanzibar.

Halikadhalika maofisa hao waliwaelekeza wanafunzi hao, kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria, pamoja na kujiepusha na vikundi viovu vinavyojihusisha na dawa za kulevya, vibanda vya gemu chafu, tamaa, pamoja na kuwaelimisha juu ya kujiepusha na michezo ya kubeti.

Kwa upande wa Jesho la polisi liliwafunza wanafunzi wa Madrasa hizo kujenga utamaduni wa kutoa taarifa kwa mamlaka za kisheria hasa wanapokumbana na matukio yanayohatarisha usalama wao na uvunjifu wa amani.



Mafunzo ya haki za binadamu na msaada wa kisheria yaliyotolewa kwa wanafunzi wa Madrasa hizo ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili (MSLAC II), yenye kaulimbiu isemayo "Msaada wa Kisheria kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo" ambayo ilizinduliwa rasmi visiwani Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi Juni 20, 2026 ambapo maonesho ya Kampeni hizo yaliendelea katika viwanja vya Nanenane vilivopo Dole Kizimbani, Wilaya ya Magharibi A na maonesho hayo yanaendelea kwa wilaya tatu za mkoa wa Mjini Magharibi ambayo yanatarajiwa kutamatika, Julai 05, 2026.

Aidha, THBUB imeendelea kutoa wito kwa jamii kushiriki kikamilifu katika kulinda haki za watoto kwa kuvunja ukimya dhidi ya vitendo vya udhalilishaji kwa kushirikiana na mamlaka husika kuhakikisha kila mtoto anapata ulinzi, haki na fursa ya kukua katika mazingira yenye usalama, utu na heshima.

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...