NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
MKUU wa mkoa wa kusini Pemba Rashid
Hadid Rashid, amesema jumuiya ya kitaifa ya wafanyabiashara Zanzibar ‘ZNCC’ imekuwa
chanzo kikuu cha kuwaonesha njia za kujiajiri vijana, kutokana na juhudi zake
mbalimbali.
Mkuu huyo wa mkoa, aliyasema hayo leo Julai 11,
2026 ukumbi wa Kiwanja cha kufurahishia watoto Tibirinzi Chake chake,
kwenye hafla ya kukabidhi ruzuku kwa wajasiriamali, kupitia mradi wa ‘Inclucities’,
unoaendeshwa kwa pamoja na jumuiya hiyo na Trias na Enabel kama mtekelezaji
mkuu.
Alisema ZNCC, imekuwa ikihangaika huku na kule, ili
kuhakikisha wajasiriamali, wanaendelea kujiajiri wakiwa na uhakika wa
uwezeshaji, kama mfano wa ruzuku kama hizo zilizotolewa.
‘’Kwanza niwapongeze sana wenzetu wa ZNCC kwa
kushirikiana na Trias na Enabel, ambapo leo tunashuhudia utoaji wa ruzuku, kwa
wajasiriamali wetu,’’alieleza.
Akizungumzia kuhusu mchango wa jumuiya za kimataifa,
alisema wamekuwa wadau wakuu wa kuisaidia serikali na wananchi wake, bila ya
ubaguzi.
Alieleza kuwa, kupitia mradi huo mkubwa wa
Inclucities, umetoa dira kwa vitendo, kwa namna gani, wanavyoisaidia serikali na
watu wake.
Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa wa kusini Pemba Rashid
Hadid Rashid, amewataka wanavikundi vilivyokabidhiwa ruzuku hizo, kwanza kuheshimu
na kuzitumia kwa malengo husika.
Mapema Mkuu wa wilaya ya Chakechake Zuhura Mgeni Othman, aliwasisitiza wanavikundi hao, kuhakikisha sasa hawarudi tena kwenye utegemezi, baada ya kukabidhiwa ruzuku hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa ZNCC, Hamad Hamad, alisema
moja ya jukumu kubwa la jumuiya hiyo, ni kuhakikisha wajasiriamali, wanafanyakazi
zao kwenye mazingira rafiki.
‘’Mfano wa upatikanaji wa rukuzu hizi, ni moja wapo
lakini pia tunawasadia kupata masoko, kwa njia ya kidijitali na kushiriki
katika maonesho ya kimataifa,’’alifafanua.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jumuiya ya Trias Ritha Tarimo, alisema kupitia mradi huo, wamekuwa wakiendesha shughuli mbalimbali, ikiwemo, kukuza ujuzi kwa wajasiriamali.
Alieleza kuwa, mradi huo ni sehemu tu ya kuwasaidia
wajasiriamali hao, lakini wamekuwa na shughuli nyingine kadhaa, kama za kuwaonesha
masoko ya kimataifa.
Akiwasilisha majukumu ya jumuiya ya Enabel, mtendaji
wa jumuiya hiyo Mohamed Rashid, alisema kwa upande wa Pemba, pekee wapo vijana
300 ambao, wameshawaingiza kwenye vyuo vya amali vya Daya na Vitongoji.
‘’Vijana hawa wamejifunza, usarifu wa chakula, mwani
pamoja na utaalamu wa kuchakata vyuma na mbao,’’alifafanua.
Aliongeza kuwa, kwa vile wanafanyakazi kwa karibu na
benki ya CRDB, tayari zipo shilingi milioni 300 kwa Pemba pekee, ambazo zimeelekezwa
kwa wafanyabiashara.
Akiwasilisha ripoti ya ZNCC, Mratibu ofisi ya Pemba
Khalfan Amour Mohamed, alisema leo wanajisikia faraja kuona, wajasiriamali hao,
wanakabidhiwa rukuzu hizo.
Alisema, moja ya changamoto kwa vikundi vingi, vya ujasiriamali,
ilikuwa ni upatikanaji wa mitaji, nambari za utambulisho wa bidhaa na elimu ya
uendelezaji wa kazi zao.
‘’ZNCC imekuwa haipati usingizi, kuhakikisha wajasiriamali
wa Unguja na Pemba, wanaendelea kuzalisha bidhaa bora, zinazovutia soko la
kimataifa,’’alifafanua.
Aidha, alisema bado wanaendelea na juhudi za kuhakikisha,
vikundi vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu vinawezeshwa, ili nao kumudu
kuajiri wingine.
Baadhi ya wajasiriamali waliokabidhiwa ruzuku hiyo,
waliahidi kuzitumiaka kama ilivyokusudiwa.
Hata hivyo Mjumbe wa bodi ya ‘ZNCC’ Haji Khatib,
alisema amefarajika kuona, ZNNC imekuwa tegemeo kwa wajarisiriamali na wafanyabiashara
wa Unguja na Pemba.
Vikundi vingine ‘Mwanzo mgumu’ cha Michakaini
Chakechake shilingi milioni 2.5, vikundi vyingine vilivyokabidhiwa shilingi
milioni 2 kila kimoja, ni ‘Juhudi zetu’, ’Nguvu moja’, ‘Bora hatima’ na ‘Tushkamane
kutoka Wingwi.
Mwisho
Comments
Post a Comment