Skip to main content

‘ZIC’ YAGAWA CHAKULA MAANDALIZI YA SIKUKUU KWA MAYATIMA, WAFUTARI NAO PAMOJA MTAMBWE

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MKUU wa wilaya ya Wete Rashid Abdalla Rashid, amesema jambo la kugawa chakula kwa mayatima, lililofanywa na Shirika la Bima Zanzibar ‘ZIC’ ni la kiutu na linafaa kuigwa na mashirika mingine.

Mkuu huyo wa wilaya, aliyasema hayo jana, kwenye kijiji cha kulelea mayatima, Bwagayamoyo Mtambwe Wete, mara baada ya kumaliza hafla ya ugawaji wa chakula kwa ajili ya sikukuu, iliyoandaliwa na ‘ZIC’.

Alisema, ‘ZIC’ imefikiria jambo jema kwa watoto hao, kwani wameondokewa na baba zao, hivyo wanapopata mashirika kama hayo, hurejesha matumaini na furaha.

Alieleza kuwa, ijapokuwa kuondokewa na jambo kubwa na linalochelewa kusahaualika, lakini ugawaji huo wa chakula hicho, na kwa uhakika, inawapunguzia machungu watoto hao.



‘’Kwanza niwapongeza sana wenzetu wa ‘ZIC’ kwa uamuzi wao, kwanza kuwagawiya futari mayatima tena hawa, waliopo hapa Mtambwe,’’alisema.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa wilaya ya Wete, aliwataka wazazi na walezi wanaowalea watoto hao mayatima, kuendelea kuvumilia, kwani ulezi wa mzazi mmoja, huwa na changamoto zaidi.

‘’Hata ulezi wa watoto ambao wazazi wao wote wawili bado wapo hai, huwa ni mgumu, hivyo na nyinyi endeleeni kuvumilia, katika hili,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, amelitaka shirika la Bima Zanzibar ‘ZIC’ kuendelea kuwa karibu na makundi mbali mbali, ili matunda yake yarudi kwa jamii.



Mapema Mkurugenzi Utawala ‘ZIC’ Juma Khamis Hija alisema, wamekuwa na utamaduni wa kushirikiana na jamii, katika nyanja mbali mbali, ikiwemo elimu.

Alieleza kuwa, hata msaada huo wa chakula kwa ajili ya mayatima, ni eneo moja wapo la kushirikiana jamii.



‘ZIC ni shirika la wananchi wenyewe, hivyo kila muda tumekuwa tukikutana nao, iwe ni kwenye huduma za kibinaadamu, elimu au afya kwa ajili yao,’’alifafanua.

Hata hivyo, amewakumbusha wananchi kundelea kukata bima mbali mbali, ikiwemo ya vyombo vya maoto, nyumba, bima za maisha na mali nyingine.






Mapema Kaimu Meneja wa ‘ZIC’ Pemba Saida Baraka Saleh alisema, wamekuwa wakiwajali mno wananchi wote, na hasa wale waliokatika mazingira magumu, wakiwemo mayatima.

Alieleza kuwa ‘ZIC’ itaendelea kushirikiana na kuwa karibu na jamii, kwani ni shirika lao, kama yalivyo mingine kutoka serikalini.









Hata hivyo, alisema jambo la kuwapa chakula mayatima ni jema, na ndio maana uongozi wa ZIC, umeamua kukutana nao na kuwapa chakua hicho.

‘’Sisi ZIC tunawajali wananchi wote, na ndio maana leo tumeshagawa vyakula kwa mayatima na familia zao,’’alifafanua.

Akisoma risala ya kijiji hicho, mwakilishi wa wazazi hao Mohamed Sharif Mohamed, alisema wamekuwa wakikabiliwa na chagamoto ya ukosefu wa umeme kijijini hapo.

Alisema jingine, ni umbali wa kituo cha elimu ya maandalizi kwa watoto, ukosefu wa usafiri hasa nyakati ya usiku, inapotokezea dharura, jambo linalowapa ukakasi wa maisha.


Wakati huo huo, ungozi wa ZIC uliungana na watoto hao mayatima na familia zao, katika futari ya pamoja, iliyofanyika kijijini hapo.







Kijiji cha kulelea watoto mayatima kilichopo Bwagamoyo Mtambwe, ambacho kina nyumba 14, kinajumuisha watoto 52, wakiwemo wakike 32 na wanaume 20.

            Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...