Skip to main content

DK. MWINYI KUINGIA KWENYE HISTORIA UZINDUZI MWENGE WA UHURU PEMBA

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, utakaofanyika Aprili 2 mwka huu katika Uwanja wa  michezo Gombani Chake Chake Pemba.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa  Mkoa wa Kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kwa mwaka 2026 ofisini kwake  Chake Chake Pemba.



Alisema kuwa, katika uzinduzi huo Dk. Mwinyi atahutubia wananchi pamoja na kuzindua rasmi mbio za mwenge wa uhuru na kuendelezwa kwa ufunguzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo katika wilaya nne kisiwani Pemba.



Alisema, mwenge wa uhuru hukimbizwa nchi nzima ikiwa ni sehemu ya kuenzi uhuru wa taifa, kuenzi maendeleo ya nchi sambamba na kudumisha Amani, mshikamano na maelewano ya wananchi katika shughuli mbali mbali za maendeleo ya taifa.



"Mwenge wa uhuru mwaka huu 2026 unatarajiwa kuzinduliwa Pemba kitaifa mnamo tarehe 2 Aprili, 2026 katika uwanja wa Michezo Gombani wilaya ya Chake chake  Mkoa wa Kusini Pemba, hivyo tunawaomba muzifikishe taarifa hizi kwa wananchi ili wahudhurie kwa wingi,’’

Alieleza kuwa, matayarisho ya uzinduzi wa mbio za mwenge huo yamekamilika na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imejipanga kikamilifu kuhakikisha tukio hilo la kihistoria linakamilika kwa mafanikio makubwa.

Mkuu wa mkoa huyo alieleza kuwa, vikundi vya usalama, vikundi vya hamasa na halaiki vimejipanga ipasavyo na kuhakikisha viongozi na wananchi kwa ujumla wanakua salama.

Alieleza, tukio la uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru linatarajiwa kudhuriwa na viongozi mbali mbali pamoja na wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Tanzania, hivyo aliwaomba wananchi kushiriki kikamilifu katika tukio hilo la kihistoria.

Mkuu huyo aliwataka wananchi kuendeleza umoja na mshikamano ulipo Zanzibar, ili kudumisha taswira nzuri iliopo katika Mkoa wa Kusini Pemba.

Aliwahakikishia wananchi usalama wa kutosha katika uzinduzi huo, huku akieleza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga katika kuhakikisha hali hiyo inadumu katika mkoa huo.

"Niwahakikishie wananchi usalama upo katika Mkoa wa Kusini Pemba na vikosi vya ulinzi na usalama vimejipanga ipasavyo kuhakikisha hali hiyo inadumu muda wote", alisisitiza.

Aidha, aliwataka wananchi kutoka maeneo yote ya Tanzania kufika katika Mkoa wa Kusini Pemba kujumuika kwa pamoja ili kufanikisha kwa kiasi kikubwa uzinduzi huo.

Alifahamisha kuwa, baada ya kukamilika uzinduzi huo,  mwenge wa uhuru utaanza mbio zake katika wilaya ya Chake chake na Mkoani, pamoja na kuendelea kukimbizwa katika wilaya nyengine na mikoa ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo na kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo.

 Hivyo aliwataka wananchi kuendelea kudumisha amani na mshikamano uliopo nchini hususan katika kipindi hichO cha uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru, ili kuhakikisha tukio hilo linamalizika kwa salama na amani.

Hata hivyo aliwasihi wafanyabiashara na wajasiriamali wa bidhaa mbali kutumia fursa hiyo kutangaza bidhaa zao, pamoja na kudumisha usafi katika maeneo yao ili kudumisha haiba ya maeneo yao.

Alisema, iwapo wafanyabiashara watatumia vizuri fursa hiyo watawawezesha wageni kuona bidhaa mbali mbali sambamba na kujionea fursa za kiutamaduni na utalii zilizopo kisiwani Pemba.

‘’Tuna vivutio vingi vya utalii kwenye Mkoa wetu na Pemba yote kwa ujumla, hivyo tunawaomba wageni watakaofika kisiwani hapa pia wakajionee historia zetu ambazo ni za kusisimua, kufurahisha na kujifunza,’’ alifafanua Mkuu huyo.

Mwenge wa uhuru kitaifa mwaka huu utazinduliwa Aprili 2 katika uwanja wa Michezo Gombani Chake Chake Pemba, ambapo hilo ni tukio la pili kufanyika kisiwani Pemba, kwani miaka kumi iliyopita mwenge wa uhuru kitaifa ulizinduliwa Chokocho wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba.

                                          MWISHO

 

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...