NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
CHIMBO la mwenge wa Uhuru, ni nia ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kuweka mwenge juu ya kilele cha mlima Kilimanjaro.
Lengo ni kuleta matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale penye chuki na heshima pale palipojaa dharau.
Ambapo nia hiyo, aliitoa kwa mara ya kwanza mwaka 1959 huko New York, alipohutubia Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa.
Kwa wakatu huo, alimteua Luteni Alexander Gwebe Nyirenda kutekeleza azma hiyo iliyoitwa “Operesheni Mwangaza”, ambapo yeye na wenzake, walianza maandalizi mwezi Novemba 1961.
Kabla ya Tanganyika kupata uhuru, ambapo hatimaye usiku wa mkesha wa sherehe za uhuru tarehe 9 Desemba 1961, Luteni Nyirenda na wenzake, waliwasha na kusimika mwenge wa uhuru na Bendera ya Tanganyika kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro.
Hiyo ilikuwa kama ishara ya kuwa huru, kwa kupandisha mwenge kileleni ilikuwa kwanza, ni kuonesha kazi ngumu iliyoko mbele ya kulijenga taifa changa la Tanganyika.
Pili, ilikuwa ni kuuwasha mwenge uangaze nje ya mipaka, kutoa matumaini pasipo na matumaini, upendo palipo na chuki na heshima palipo na uonevu na dharau.
Makamu wa wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Philipi Mpango, kwenye hutuba yake aliyoitoa Aprili 2, mwaka 2025 mkoani Pwani, kwenye uzinduzi wa mwenge huo, alisema wazo la kukimbiza mwenge wa uhuru nchi nzima na kila mwaka.
Akisema lilitolewa na vijana wa TANU katika kikao chao kilichofanyika Juni 26 mwaka, 1964, ambapo lengo kuu likiwa ni kutekeleza kwa vitendo, azma ya Baba wa taifa ya kuhamasisha umoja, upendo, amani na ujenzi wa taifa.
Akaeleza kuwa, tangu wakati huo, mwenge huo umekuwa ukikimbizwa katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kupitia mbio hizo hamasa kubwa hutolewa.
Akasisitiza kuwa, lengo ni kuendelea kudumisha amani, na kujenga uzalendo, umoja na mshikamano miongoni mwa watanzania waote.
Ndio maana anasema, katika kipindi chote hicho, mbio za mwenge wa uhuru, zimekuwa na mafanikio makubwa yanayosadifu maono ya waasisi wa taifa la Tanzania.
‘Mwenge wa uhuru 2025 unaowashwa leo (mwaka jana) utakimbizwa kwa muda wa siku 195, katika mikoa 31 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kufikishwa kwa ujumbe wake,’’alisisitiza.
Makamu huyo wa Rais, mwaka jana aliiagiza mikoa na mamlaka za serikali za mitaa kutoa ushirikiano wa hali ya juu, kwa wakimbiza mwenge wa uhuru kitaifa, ili waweze kutekeleza jukumu la kizalendo, walilokabidhiwa la kuhakikisha kuwa wanawafikia wananchi.
MGENI RASMI MWAKA 2026
NI Rais wa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, ndie anayetarajiwa kuwa mgeni rasmi, kwenye uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka huu 2026.
Ambapo hafla ya uzinduzi huo, utafanyika Aprili 2 mwka huu, katika Uwanja wa michezo Gombani wilaya ya Chake Chake, mkoa wa kusini Pemba.
Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa mkoa huo, Rashid Hadid Rashid, wakati akizungumza na waandishi wa habari, juu ya uzinduzi huo, aliwakumbuhsa jambo wananchi.
Aakasema kuwa, katika uzinduzi huo Dk. Mwinyi atawahutubia wananchi, pamoja na kuzindua rasmi mbio za mwenge wa uhuru na kuendelezwa kwa ufunguzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo, katika wilaya nne kisiwani Pemba na Tanzania kwa ujumla.
Maana alisema, mwenge wa uhuru hukimbizwa nchi nzima, ikiwa ni sehemu ya kuenzi uhuru wa taifa, kuenzi maendeleo ya nchi, sambamba na kudumisha amani, mshikamano na maelewano.
"Mwenge wa uhuru mwaka huu 2026, unatarajiwa kuzinduliwa Pemba kitaifa Aprili 2, mwaka 2026 katika uwanja wa michezo Gombani, wilaya ya Chake chake, hivyo tunawaomba wananchi kuujza uwanja,’’anasisitiza.
Anaeleza kuwa, matayarisho ya uzinduzi wa mbio za mwenge huo, yamekamilika na serikali ya Mapinduzi Zanzibar, imejipanga kikamilifu kuhakikisha tukio hilo la kihistoria, linakamilika kwa mafanikio.
Mkuu wa mkoa huyo anafafanua kuwa, vikundi vya hamasa na halaiki, wasanii vimejipanga ipasavyo na kuhakikisha viongozi na wananchi kwa ujumla, wanapa burudani.
Alieleza, tukio la uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru, linatarajiwa kudhuriwa na viongozi mbali mbali pamoja na wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Zanzibar na Tanzania bara.
‘’Hapa nichukuwe nafasi hii, kuwataarifu wanachi wa mkoa wa kusini Pemba, kwamba wanaugeni mzito, hivyo aliwaomba kushiriki kikamilifu, katika tukio hilo la kihistoria,’’anasiistiza.
Mkuu huyo aliwataka wananchi kuendeleza umoja na mshikamano ulipo Zanzibar, ili kudumisha taswira nzuri iliopo katika Mkoa wa Kusini Pemba.
Aliwahakikishia wananchi usalama wa kutosha katika uzinduzi huo, huku akieleza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga, katika kuhakikisha hali hiyo inadumu katika mkoa huo.
"Niwahakikishie wananchi usalama upo katika mkoa wa kusini Pemba na vikosi vya ulinzi na usalama, vimejipanga ipasavyo, kuhakikisha hali hiyo inadumu muda wote", alisisitiza.
Aidha, aliwataka wananchi kutoka maeneo yote ya Tanzania kufika katika mkoa wa kusini Pemba, kujumuika kwa pamoja ili kufanikisha kwa kiasi kikubwa, uzinduzi huo.
Alifahamisha kuwa, baada ya kukamilika uzinduzi huo, mwenge wa uhuru, utaanza mbio zake katika wilaya ya Chake chake na Mkoani, pamoja na kuendelea kukimbizwa katika wilaya nyingine.
Hivyo aliwataka wananchi kuendelea kudumisha amani na mshikamano uliopo nchini hususan katika kipindi hicho cha uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru, ili kuhakikisha tukio hilo linamalizika kwa salama na amani.
Hata hivyo aliwasihi wafanyabiashara na wajasiriamali kutumia fursa hiyo kutangaza bidhaa zao, pamoja na kudumisha usafi, katika maeneo yao ili kudumisha haiba ya maeneo yao.
‘’Tuna vivutio vingi vya utalii kwenye mkoani mwetu na Pemba yote kwa ujumla, hivyo tunawaomba wageni watakaofika kisiwani hapa, pia wakajionee historia zetu ambazo ni za kusisimua,’’alifafanua.
WANANCHI WANASEMAJE
Idda Haji Mohamed wa Chake chake, anasema ni fahari kubwa, kwa serikali kuamua kfanya uzinduzi huo ndani ya mkoa wa kusini Pemba.
Haji Mohamed Said, dereva wa tax, amesema ni faraja ya kuongeza pato lake, kupitia biashara hiyo, ambayo huneema wanapopata wageni.
Fatma Omar Haji, mmiliki wa mgahawa Machomane Chake chake, anasema jambo hilo litasaidia kuendesha shughuli zake.
Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, amesme mpango wa serikali wa kuweka mkoa wa kusini Pemba, eneo la uzinduzi ni kuongeza historia nyingine.
‘Amani, Umoja na Mshikamano wa Kitaifa,’’ndio kauli mbiu ya mwenge wa uhuru mwaka 2026.
MWISHO
NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...



Comments
Post a Comment