Skip to main content

UNAIFAHAMU KAULIMBIU YA MWENGE WA UHURU WA MWAKA HUU?

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

……..MWENGE wa uhuru ni chombo cha kitaifa.

Baada ya taifa la Tanzania kupata huru, kilianzisha chombo hicho, kikiwa na malengo kadhaa ndani yake.

Kwa wakati huo, taarifa zinaeleza ni hayati Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ndie aliyeuasisi.

Kumbe unaweza kuthibitisha kuwa, chimbo la mwenge huo wa uhuru, ni maono ya Baba wa taifa, hasa pale alipousimamisha juu ya mlima Kilimanjaro.

Akatamka kuwa, ‘lengo ni kuleta matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale penye chuki na heshima pale palipojaa dharau’.

Mwenge huo, kwa mara ya kwanza, uliwashwa mwaka 1961, baada ya Mwalimu Nyerere kumteua Luteni Alexander Gwebe Nyirenda kutekeleza azma hiyo iliyoitwa “Operesheni Mwangaza”.

Kwa mwaka jana, aliyekua Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Philipi Isdori Mpango, wakati akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Pwani, kwenye uzinduzi, alisema mwenge ni kielelezo cha umoja na mshikamano.

Akafafanua kuwa, tangu wakati huo, mwenge huo umekuwa ukikimbizwa katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bara na visiwani, na kupitia mbio hizo hamasa kubwa huonekana.

Ingawa kwa mwaka huu, heshima ya uzinduzi wa mwenge huo wa uhuru, umepewa Mkoa wa kusini Pemba, tena ndani ya wilaya ya Chake chake.

Pamoja na mambo mingine, tayari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, imeshaandaa zaidi ya kamati saba kwa lengo la kufanikisha maandalizi.

Maana, Mkuu wa huo Rashid Hadid Rashid, anasema zipo kamati kadhaa, ikiwemo ya hamasa, usafiri, afya na zote zinafanyakazi kwa kushirikiana.

Kwenye uzinduzi wa mbio hizo za uhuru kwa mwaka huu, ipo kaulimbiu, ambayo inamaana pana na halisi kwa watanzania.

‘’TANZANIA NI YETU SOTE, TUSHIKAMANE KWA PAMOJA, KULETA MAENDELEO’



Hii ndio kauli mbiu ya ujumbe wa mwenge wa uhuru wa mwaka 2026, ambapo ndani yake imebeba vijumbe vidogo vidogo kadhaa.

Kauli mbiu hii, ilichambuliwa vyema na Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid, akisema Tanzania ni ya watu wote.

Akafafanua kuwa, hakuna haja ya kujitokeza kwa wachache, kuichafua Tanzania, kwa maslahi ya mtu mmoja.

‘’Kwa mfano, ukichambua neno Tanzania ni yetu sote, hapa inakukataza wizi, uchafuzi wa amani, rushwa na hata matuzi ya dawa za kulevya,’’anasema.

Akaeleza kuwa, neno ‘tushikamane’ inamaana pana zaidi, ikiwemo kila mmoja anawajibu wa kuliletea maendeleo taifa hili.

Akiwa na maana, kuwa suala la kuwa na maadili ya kazi, kwenye ofisi za umma na binafsi, linasaidia mno, kwa watanzania kuheshimiana.

‘’Tunapogusia maana halisi ya mshikamano, sio kwa watendaji wakuu wa serikali pekee, bali hata mwananchi wa kawaida, mtumishi wa chini na wale wa waliojiajiri,’’anaeleza.

Mratibu wa mwenge mkoa wa kaskazini Pemba Zadida Abdalla, anasema ‘kushikamana na kuleta maendeleo’ ni wajibu wa mwanachi kuungana na viongozi, pale wanapoleta miradi.

Anaona kuwa, maagizo na miradi ya serikali haiwezi kufanikiwa vyema, ikiwa kila mmoja hatoitilia maanani kaulimbiu ya mwenge ya mwaka 2026.

Mratibu huyo anasisitiza kuwa, isiwe kuwa mwenge umekuja na kufurahia pekee, bali maneno yaliotengeneza kauli mbiu, ni muhimu kuyachambua.



‘’Ndani ya maneno ya kaulimbiu ya mwenge wa uhuru kwa mwaka 2026, ukiamua kuyachambua ni darasa tosha la kila mmoja, kutekeleza wajibu wake tena pasi na kusimamiwa,’’anaeleza.

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, akizungumza na masheha, aliwataka kuwaelezea wananchi, maanali halisi ya kualimbiu ya mwenge ya mwaka huu.

Akaeleza kuwa, imekuja kuharakisha umoja, mshikamano na ulinzi wa taifa, bila ya kujali mtu dini yake, rangi wala wapi anatokea.

Hata Katibu Tawala mkoa wa Kusini Pemba, Mwalimu Amour, wakati akizungumza na kamati za matayarisho ya uzinduzi wa mwenge huo, alisisitiza kuizingatia kauli mbiu.

‘’Kauli mbiu huwepo nyingi kila mwaka na kila kwenye uzinduzi wa mwenge, lakini hii ya mwaka huu, imekusanya kila kitu,’’anasema.

WANANCHI NA KAULIMBIU YA MWENGE 2026

Issa Haji Machano wa Mkoroshoni Chake chake, anasema kaulimbiu ya mwaka huu, inafahamika kwa haraka, maana halisi iliyokusudiwa.



‘’Ukiisoma kama inakutaza kula rushwa, kuacha wizi, viya dhidi ya dawa za kulevya, maana ndani yake mna neno ‘Tanzania ni yetu sote’,’’anaeleza.

Ilyassa Hassan Omar wa Kichungwani anasema, ndani ya sentesi ya kaulimbiu ya mwaka huu, inatoa taaluma, kwa kila mtanzania.

Habiba Kombo Othman, anasema kama kila mmoja kuanzia viongizi hadi wananchi wa kawaida, wataifanyia kazi kaulimbiu ya mwenge ya mwaka huu, hakurajii mabaya.

‘’Maana kama vile inakataza udhalilishaji, matumizi mabaya ya ofisi, rushwa, lishe bora, maana sentensi zake zimepangika,’’anasema.

Mwanahija Hassan Kassim wa Pondeani Chake chake, anasema kama sio Tanzania kuzidiwa na wanasiasa wapotoshwaji, basi ujumbe huo ni darasa tosha, kwa wananchi.

‘’Wapo wingine wanaweza kuubeza, lakini kama utatulia na kuusoma kwa umakini, na kisha kuanza kuuchambua, utagundua umebeba kitabu kizima,’’anaeleza.  

VIJUMBE VYA KUDUMU VYA MWENGE

Kwa kawaida, kila mwaka kaulimbiu ya mwenge, hubadilika kwa aina ya mazingira, ingawa vipo vijumbe vyingine kadhaa, ambavyo ni vya kudumu.

Mfano, suala la lishe bora, ni ujumbe ambao upo kwa muda mrefu, ambapo wakimbizwa mwenge hutakiwa kuwachambulia wananchi.

Eneo jingine ni vita dhidi ya dawa za kulevya, malaria, ukimwi na janga jingine la kupinga suala la rushwa Tanzania.

MGENI RASMI KWA MWAKA 2026  

Kwa mujibu wa Mkuu wa mkoa mwenyeji wa uzinduzi wa mwenge huo wa uhuru kitaifa, anayetarajiwa kuwa mgeni rasmi ni, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Juzi akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, alisema Dk. Mwinyi atawasili ndani ya uwanja wa Gombani Chake chake, kwa ajili ya kazi hiyo na kisha kuwahutubia wananchi.

Akaeleza kuwa, baada ya zoezi hilo, mwenge huo utakabidhiwa kwa uongozi wa wilaya ya Chake chake, kwa ajili ya kukimbizwa na ufunguzi wa miradi na uwekaji wa mawe ya msingi utafuta.

Kumbe kabla ya April 4, kwenye mkoa wa kaskazini Pemba, siku inayofuata itakuwa ni zamu ya wilaya ya Mkoani, ambapo mwenge huo utaifungua na kuitembelea miradi iliyopangwa.

BURUDANI

Mkuu huyo wa Mkoa, aliwaalika wananchi wake na wale wa kaskazini Pemba, ambapo pamoja na mambo mingine, ni kuburudishwa na wasanii.

Akasema, wameshamualika msanii Mau Mpemba, Maswga classic, K-Official, msewe wa vijana Mchangamdogo, Kirobo na Dula Makabila kutoka Tanzania bara.

Eneo jingine, alisema watakaohudhuria watawaona mubashara, watoto wa halaiki, waliofunzwa na kufunzika, wakiandika maumbo kadhaa.

Utenzi na kwaya zenye nyimbo za ufafanuzi wa kaulimbiu ya mwenge na vijumbe vyake vya kudumu, zitatikisa ndani ya uwanja wa Gombani.

 Akaongeza kuwa, mwenge wa uhuru hukimbizwa nchi nzima, ikiwa ni sehemu ya kuenzi uhuru wa taifa.

Pia ni kuenzi maendeleo ya nchi, sambamba na kudumisha amani, mshikamano na maelewano, miongoni mwa wananchi.

Anaeleza kuwa, matayarisho ya uzinduzi wa mbio za mwenge huo, yamekamilika na serikali ya Mapinduzi Zanzibar, imejipanga kikamilifu kuhakikisha tukio hilo la kihistoria, linakamilika kwa mafanikio.

Akwasihi wafanyabiashara na wajasiriamali kutumia fursa hiyo, kutangaza bidhaa zao, pamoja na kudumisha usafi, katika maeneo yao ili kulinda haiba ya maeneo yao.

                                          MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...