Skip to main content

WANANCHI PEMBA, WAMPA TANO DK. MWINYI KWA HUTUBA YA UJENZI WA AMANI

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa mkoa wa kusini Pemba, wameipongeza hutuba ya uzinduzi wa mwenge wa uhuru kitaifa kwa mwaka 2026, iliyotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Walisema, hutuba hiyo ilitoa mwelekeo wa umoja, mshikamano, upendo miongoni mwa wananchi wa Tanzania, jambo linalofaa kuungwa mkono.

Wakizungumza mara baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa mwenge huo, jana uwanja wa michezo Gombani, walisema hutuba imewakumbusha watanzania wajibu wao, kwa maslahi mapana ya taifa.

Mmoja kati ya wananchi hao Ali Ameir Haji wa Mchangamdogo, alisema hutuba hiyo kama wananchi waliifuatilia kwa makini, basi ni darasa tosha wa ujenzi wa amani.

Alieleza kuwa, hutuba nyingi anazozitoa Dk. Mwinyi kwenye hafla kadhaa za kitaifa, huwa na mwelekeo mpana, ingawa hiyo ya kwenye uzinduzi wa mwenge wa uhuru, imeongezeka mara dufu.

‘’Kwa hakika hutuba hiyo, ilijaa kila kitu mfano, imehamasisha upendo, nidhamu, umoja na mshikamano wa dhati miongoni mwa wananchi wa makundi mbalimbali,’’alifafanua.



Nae Ibrahim Haji Machano wa Mkoani, alisema yeye hutuba hiyo ilimnasa, hasa alipozungumzia suala la kuulinda na kuuendeleza Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Alifahamisha kuwa, mara nyingi Dk. Hussein Ali Mwinyi, huwa haachi kuugusa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ingawa kwenye hutuba yake ya jana, alionesha vitu tofauti vya kuulinda.

‘’Kwanza alisema kila mmoja anaowajibu wa kuhakikisha, Muungano huo anauenzi, na alionesha faida kadhaa ikiwemo ulinzi, usalama, upendo na kuwaunganisha wananchi wote,’’alifafanua.



Kwa upande wake Mwanaisha Haji Makame wa Mtambile, alisema hutuba hiyo inafaa kutengenezewa kitabu maalum, na kusambaazwa kwa wanafunzi na makundi ya kijamii.

Alishauri kuwa, kwa vile imejaa nasaha, rai, ushauri na mwelekeo wa taifa kwa ujumla, ni vyema wananfunzi hasa wa skuli za msingi na makundi mingine, kuwafikia.

‘’Ushauri wangu hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alioitoa wakati wa uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, ichapishwe na iwekwe pamoja na kusambaazwa,’’alishauri.

Mwajuma Haji Kombo wa Ole, alisema mwananchi alikuwa kwenye usikivu mzuri, wakati Dk. Mwinyi anatoa hutuba hiyo, iliyogusia pia njia za kupamba na dawa za kulevya.

‘’Kwanza alisema, kila mmoja anawajibu wa kushirikiana na Mamlaka husika, katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya, maana kwa serikali pekee vita itakuwa ngumu,’’alisema.



Mapema Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid, akitoa salama za mkoa huo, alizipongeza serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Zanzibar, kwa kuwaamini na uzinduzi, kufayika mkoani humo.

Alisema, naamini utulivu, upendo, usikivu na mazingira bora yaliomo ndani ya mkoa huo, yamechangia kwa mkoa wa kusini Pemba, kuingia katika historia kwa mara ya pili.

Kaimu Mkuu wa wilaya ya Chake chake Rashid Abdalla, alisema uzinduzi wa mwenge huo mkoa wa kusini Pemba, ni ishara ya umoja, upendo na mshikamano miongoni mwa wananchi.

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, aliwakumbusha wananchi wajibu wao katika vita dhidi ya udhalilishaji.



Alisema, kila mmoja anaowajibu kushirikiana na mamlaka nyingine, katika kuhakikisha Tanzania, inaendelea kubaki salama.



Kabla ya uzinduzi wa mwenge huo wa uhuru, wananchi na viongozi mbalimbali waliohudhuria, walikonga nyoyo zao kwa ngoma asili, utenzi, halaiki na mchezo wa sarakasi.

         Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...