Skip to main content

WALIOKEZA SHILINGI MILION 1.6 KWA UFUGAJI MATANGO BAHARI KUVUNA 20 MILIONI

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAKIKUNDI cha ufugaji wa majongoo bahari, ‘tumuombe mola’ cha Makangaale wilaya ya Micheweni Pemba, wanatarajia kujipatia shilingi milioni 20 mwishoni mwa mwaka huu, ikiwa watafanikiwa kuuza bidhaa hiyo, baada ya kuekeza vifaranga vyenye thamani ya shilingi million 1.6 mwaka jana.

Fedha hizo, ni uwekezaji wa vifaranga 3,300 vya majongoo habari, walivyovinunua kwa shilingi 1,650,000 wastani wa shilingi 500 kila kifaranga kimoja, chenye urefu kati ya nchi nne hadi tano.

Wanakikundi hao cha tumuombe mola wamesema kati ya vifaranga hivyo, wanatarajia kuvuna majongoo yaliokwisha pevuka 2,500 na kisha kila moja kuliuza kwa bei ya shilingi 8,000 na kujipatia shilingi milioni 20.

Mwenyekiti wa kikundi hicho Hator Hassan, alisema haiwezekani kuotesha vifaranga vya idadi 3,300 kisha kuvuna kama ilivyo.

‘’Zipo changamoto kama za kufa na hasa wakati wa usafirishaji wa vifaranga kutoka eneo moja kwenda kwenye bwawa lao, wizi na wingine kufa kabla ya kufikia kupevuka,’’alifafanua.

Alifafanua kuwa mara ya kwanza, wakati wanaanza kazi hiyo, walitumia shilingi milioni 1,000,000 kwa ununuzi wa vifaranga 1,000 ingawa hatimae, walivuna majongoo 340 na kujipatia shilingi milioni 1.7.

Aliongeza kuwa, ingawa hawakula hasara, kama inavyoonekana, lakini hawakuvuuka lengo lao la kujipatia fedha zaidi shilingi milioni 5.

‘’Kama sio changamoto ya vifaranga kufa au kuibiwa wakiwa ndani ya bwawa letu, hata ule mwaka 2021 wakati tunaanza, tungejipatia faida ya shilingi milioni 4,’’alifafanua.

Aidha Mwenyekti huyo, aliongeza kuwa, hata mwaka 2023, walitarajia kujipatia faida ya shilingi milioni 9, ingawa hatimae, walipata shilingi milioni 1.5.





Aliongeza kuwa, tayari wameshafuga mara mbili, tokea waanze kazi hiyo mwaka 2021, na kutumia gharama ya shilingi milioni 3.1 kwa ununuzi wa vifaranga 4,000.

Hata hivyo, alisema kwa sasa wanasubiria hadi mwishoni mwa mwaka huu, na ikiwa vifaranga walivyovitia ndani ya bwawa hilo, havitapitia changamoto ya wizi na kufa, hawana wasiwasi wa kuvuna shilingi milioni 20.

Mmoja wa wanachama hao Hamad Omar Hamad, alisema wamekua wakibadilisha maisha yao, kupitia kazi hiyo, ikiwemo kujihakikisha fedha za matumizi.

‘’Ni kweli kabla ya kuanza kazi hii ya ufugaji wa majongoo bahari, sikuwa na uhakika wa wapi naweza kujipatia fedha za haraka, ingawa kwa sasa nnapo,’’alisema.

Hata hivyo, waliwaomba wafadhili kadhaa, kuzitatua changamoto zao, ikiwemo kuwapatia boti dogo kwa ajili ya doria, viatu vya kuvulia, ili kuepusha hasara za miguuni.


Afisa Ustawi wa mkoa wa kaskazini Pemba Nassra Massoud Sanani, alikiri kukifahamu kikundi hicho, na kusema amekuwa akiwaunganisha na wadau mbali mbali wakiwemo FAWE-Zanzibar.

Alisema, FAWE wamekuwa wakifanyakazi na taasisi kadhaa za kimataifa kama vile UN-Women na wameshaanza kuwapatia mafunzo kadhaa.

Afisa miradi FAWE -ofisi ya Pemba Hija Hamad Issa, alisema hivi karibuni, walikuwa na mafunzo ya siku nne ya mnyororo wa biashara, ambapo mwakilishi wa kikundi hicho, alikuwa miongoni mwao.

‘’FAWE unao mradi wa pamoja, ambao unawaangalia wajasiriamali wanaojishughulisha na kilimo cha mwani, majongoo bahari, migomba, ndizi na mihogo ili kuwa wabunifu,’’alifafafanua.

Alisema, wamekuwa wakifanyakazi kwa karibu na UN-Women katika mradi huo, ambao wapo wajasiriamali 20 wa wilaya za Wete na Micheweni wameshanufaika.





Mapema Mwakilishi wa shirika la kimataifa la UN-Women Tanzania Emile Kivugo Mwakafundu, alifafanua mradi huo, unawalenga wajasiriamali wa mazao ya baharini na nchi kavu.

Alisema, mradi huo wa miaka mitatu, utamalizika mwakani, ambao lengo ni kuona wajasiriamali hao, wanaziongezea thamani bidhaa zao.



Alieleza kuwa, kupitia wadau wao wa FAWE- Zanzibar wanawafundisha namna ya kutoziuza bidhaa zao, kama walivyozivuna na badala yake, waweza kuzisarifu ili wauze kwa mfumo wa bidhaa.

Kwa mwaka wa fedha 2024/2025 wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, katika kuimarisha ufugaji wa majongoo bahari na upatikanaji wa vifaranga, Idara kwa kushirikiana na Kampuni ya Zanzibar Marine Hatchery imezalisha vifaranga milioni 1.5.

Ambapo kati ya hivyo vifaranga 80,000 vimegawiwa kwa wafugaji wa Unguja na Pemba na vyingine 70,000 kwa ajili ya biashara na uzalishaji.

                       Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...