Skip to main content

DK. MWINYI: ASIFU ZANZIBAR ILIVYOWEKA MAZINGIRA RAFIKI YA USALAMA, USAWA WA KIJINSIA

 


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar imepiga hatua kubwa kulinda haki za wanawake kwa kuwa na sera na sheria bora zinazohakikisha usalama, usawa wa kijinsia na kuwepo kwa miji na maeneo salama ya kijamii.

Dk. Mwinyi, aliyasema hayo wakati akifungua mkutano wa saba wa dunia wa viongozi wa miji na maeneo salama kwa jamii uliofanyika katika hoteli ya Madinat Al- Bahr Mazizini.

Alisema serikali imekuwa mstari wa mbele kuimarisha usalama wa maeneo ya umma na kutokomeza ukatili wa kijinsia kupitia sera madhubuti na utekelezaji wa mikakati maalum.

Aidha alisema mkutano huo ulioandaliwa kwa ushirikiano na UN Women, unaakisi jitihada za kimataifa za kujenga jamii salama kwa wote, hasa wanawake na wasichana kupitia utekelezaji mzuri wa sera na sheria zinazohakikisha fursa na ustawi wao.


Rais Mwinyi alibainisha kuwa Zanzibar imepiga hatua katika kuhakiksha usalama wa miji ambao umegusia ujumuishwaji wa wanawake na wasichana katika utekelezaji wa sera na sheria za nchi.

“Safari ya maendeleo ya Zanzibar inalenga mabadiliko ya kijamii kupitia ajenda ya Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2050, usalama na usawa wa kijinsia ni nguzo kuu za mafanikio haya,” alisema Rais Mwinyi.

Hata hivyo alisema serikali imetenga fedha mahsusi za kusimamia usalama wa wanawake, wasichana na watoto, sambamba na kuunda kamati za kitaifa zinazoshughulikia masuala hayo kwa ushirikiano na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Alibainisha kuwa bila usalama wa watu wote, maendeleo hayawezi kuwa endelevu na kuamini kuwa usalama ni haki ya kila mtu na si suala la anasa au hiyari.

“Tunaamini kuwa hakuna maendeleo ya kweli bila jamii yenye amani, usalama na haki, miji salama ni sehemu ya mikakati yetu ya muda mrefu ya kuhakikisha ushirikishwaji na ustawi wa wote,” alisisitiza.

Alifahamisha kuwa Zanzibar imekuwa ni nchi salama na watu wanafanya majukumu yao bila kubugudhiwa hata katika kuelekea kipindi cha uchanguzi.


Aliahidi kuwa serikali itaendelea kuweka mikakati ya kuimarisha usawa wa kijinsia na kuondoa unyanyasaji wa kijinsia na kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Dk. Mwinyi ameipongeza taasisi ya UN Women kwa mikakati na juhudi zake kuhakikisha wanawake duniani kote wanalindwa dhidi ya vitendo vya udhalilishaji.

Alizitaka taasisi za kikanda na za kimataifa kuungana pamoja kwa lengo la kuendeleza miji na maeneo salama na rafiki kwa maendeleo ya wanawake.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Masoud Ali Mohammed, alisema Zanzibar imechaguliwa kwa heshima kuwa mwenyeji wa mkutano huo kutokana na juhudi zake katika kulinda haki za wanawake na usalama wa miji.

Alisema hayo yote yametokana na uongozi imara na wenye kujali amani na utulivu kwa watu wake unaoongozwa na Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Mapema Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee na Watoto,  Riziki Pembe Juma, alisema Zanzibar ina sera imara katika masuala ya jinsia pamoja na utekelezaji wake ikiwemo sera ya jinsia ya mwaka 2017, sera ya hifadhi ya jamii ya mwaka 2018 na sheria ya mtoto nambari 6 ya mwaka 2011.

Sheria nyengine alisema ni ya kulinda mwari na mtoto wa mzazi mmoja na sheria nyengine mbalimbi ambazo zote hizo zimelenga kusimamia usawa wa kijinsia na ustawi wa kamii katika nchi.

Zainab Katimba ni Naibu Waziri, TAMISEMI Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alisisitiza kuwa usalama katika maeneo ya umma hauwezi kutenganishwa na dhana ya usawa wa kijinsia.

Alisema jamii salama ni ile inayolinda wanawake na kuwashirikisha kikamilifu katika shughuli za kijamii, kiuchumi na kisiasa.

“Ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha udhalilishaji wa kijinsia unakomeshwa na miji salama inapatikana kwa wote kwani usalama wa wanawake ni msingi wa maendeleo ya jamii,” alisema.

Mstahiki Meya wa Jiji la Zanzibar, Mahmoud Mohamed Mussa, ni wajibu kulinda maadili ya jadi na kutumia utamaduni wa amani kama daraja la kujenga miji jumuishi.



Mratibu kutoka UN Women, Susan Ngogi Namondo, alisema wanawake wanakumbana na changamoto nyingi katika miji, hasa ukatili wa kijinsia, na ndio sababu ya mkutano huo kuwepo kama jukwaa la kutafuta suluhisho la pamoja.

“Miji jumuishi na salama imeongeza ushirikiano na ushirikishwaji wa wanawake katika nyanja mbalimbali za maendeleo na Zanzibar ni mfano wa eneo lenye amani na mazingira bora ya kuwawezesha wanawake,” alisema.

Alisema zaidi ya asilimia 20 ya wanawake nchini Tanzania wanakumbwa na ukatili wa kijinsia hali inayokwamisha maendeleo yao.

Alisema ni wajibu wa kila taifa kuunganisha nguvu na kuweka sera thabiti za kulinda wanawake.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...