Skip to main content

WANAUME WANAOKWEPA KUWASINDIKIZA WENZA WAO KLINIKI CHANZO KUFIFIA AFYA YA MAMA NA MTOTO

 


 HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ 

 NENO ujauzito si geni katika maisha ya kila siku ya binadamu.

 Kwa kawaida hali hiyo ya ujauzito, mama hupitia matatizo mengi hadi pale anapofikisha wiki 38 yaani miezi tisa ambapo ndio wakati wa kujifungua kwa  kawaida ya umri  wa  mimba ya binadamu kiafya.

 

Kuumwa mara kwa mara kichwa, tumbo, kutapika, kutojiskia hamu ya kula humkumba mjamzito wakati mimba inapoendelea kukua  ndani ya tumbo la uzazi.

 

Hii inatokana na mabadiliko ya makuzi ya  mtoto na mabadiliko ya afya  ya mama ambayo hubadilika kutokana na makuzi ya mimba ,uzito na mengine. 

 

Wataalamu wa afya wanasema makuzi ya mtoto  tumboni huambatana na mabadiliko ya afya ya mama,  ama mauzi na hata baadhi ya magonjwa .

 

Maudhi kama kujisikia uchovu wa mwili, kutapika , hamu ya kula sana ama kutopenda kula, kuchagua ama kupenda chakula cha aina fulani , hasira , kutokuwa mchangamfu na baadhi ya kinamama kusikia aibu. 

Uangalizi wa masuala ya lishe bora , kufuatilia afya ya mama  na mtoto, matunzo ya familia wakati wa ujauzito ni jambo la muhimu.

 

Katika kipindi chote cha ujauzito ushiriki wa  mwenza ni muhimu, kwa kulinda afya ya mama na mtoto, ingawa ndani ya miezi tisa kuna miezi mitatu ya kwanza ndiyo yenye hatari zaidi ya  kuharibika ama kupata matatizo ya  kiafya.

 

Ndio maana, watalamu wa afya wakasisitiza kula mlo kamili, kwa usalama wa mjamzito na mtoto wake, ambapo ni jambo la msingi kutafuta ushauri wa daktari, kulinda usalama wa  mama na mtoto.

 

Katika ukuwaji na maendeleo mazuri ya ujauzito huo mchango wa baba (mume), unahitajika kwa asilimia 100 ikiwemo kuhudhuria klinik kwa lengo la kupata taarifa kamili juu ya maendeleo ya ukuwaji wa mimba hiyo.

 

Sio tu kufahamu maendeleo, lakini pia na kujuwa changamoto zinazoweza kujitokeza na namna ya kuweza kukabiliana nazo na kuhakikisha ukuwaji bora wa mimba hiyo. 

 

Kutokana na hali hiyo ni wazi kuwa baba ana wajibu wa kuhakikisha kuwa lishe bora, inapatikana ipasavyo kwa mke au  mwenza wake anapokuwa mjamzito.

 Pamoja na kuwa wapo akina baba waliowengi sasa wanajuwa  umuhimu wa kuwasindikiza wenza wao kituo  cha afya wakati wa ujauzito, bado wapo wingine wenye dhana  tofauti na lengo lililokusudiwa.

 

MAMA WAPEWA HUDUMA 

Akisimulia  baada ya kumshauri  mume wake kuongozana nae kituo cha afya  baada ya kujibaini na ujauzito Asha Faki Juma wa Mkoani, anasema mume wake, alikataa huku akidai sababu kubwa ni  kuhofia kupimwa Virusi Vinavyosababisha UKIMWI (VVU) .

 

“Aliniambia nikishapimwa mimi inatosha na ni sawa na alopimwa na yeye jambo ambalo lilinitia unyonge”anasema. 



Fatma Kombo Makame wa Mwambe anasema baada ya mume wake kuongozana nae mara moja, alimwambia hawezi kurejea tena kwani yeye ameshajiona yuko salama. 

 

Zuhura  Juma wa Chake chake  anasema hufanya kazi kubwa hadi pale mumewake anapokubali kwenda nae klinik anachodai humpotezea muda katika shughuli zake za kazi.  

WANAUME 

 

Ali Omar Makame wa Mkoani, anasema suala la kumsindikiza mke wake kituo cha afya, halipi kipaumbele maana sie aliyebeba ujauzito, 

 

Hassan Mbarouk anasema  kwa sasa baada ya kupewa elimu na mke wake, anamsindikiza ingawa si mara zote.

 

Ali Hilali wa Mkanyageni anasema  kwa vile yuko salama kiafya huenda klinik kwa kumridhisha mke wake tu na sio kwa hiari yake.

 

 AKINA BABA WALIOPATIWA ELIMU YA AFYA YA UZAZI 

 Khamis Mohamed wa Mkoani  anasema kwenda pamoja klinik na mke wake hana pingamizi, kwani humsaidia kujuwa afya ya mama ili kuweza kumlinda yeye na  mtoto mtarajiwa.

 

 "Mimi namsindikiza mke wangu, kwani kunanizidishia mapenzi kati yetu na mke wangu na pia kunamfanya kuwa na furaha,"anasema. 

 

Khatib Juma wa Mbuyuni, anasema kumsindikiza mwenza wake klinik sio jambo baya, kwani unapimwa vipimo vinavyosaidia kumlinda mtoto mtarajiwa iwapo atakuwa na magonjwa kama  virusi vya ukimwi. 

 

Kwa vile klinik ya uzazi hutolewa elimu na ushauri bora kwa mama, humsaidia kujuwa jinsi ya kumtafutia huduma za lishe bora. 

 

Akitowa mfano baada ya mke wake kupata mimba ya mwanzo Said Sharif Omar wa Kengeja, ndipo alipojuwa mabadiliko ya kimaumbile na tabia kupitia elimu aliyoipata klinik.  

 UTOWAJI WA ELIMU UKOJE

Muhudumu wa afya ngazi ya jamii wilaya ya Mkoani Raya Deyyum anasema, elimu kwa akina baba majumbani kuhusu kuongozana na wenza wao kwenda klinik inatolewa. 

 


Anasema hali ya kukubali kwa wanaume kuwasindikiza wake zao klinik kwa sasa inatia moyo ingawa bado wapo akina mama kwa mara ya kwanza hufika klinik bila ya waume zao ingawa huwataka wanaporudisha vipimo waende na waume zao.

 

Mkuu wa vituo vinavyotoa  huduma na tiba kwa watu wanaoishi na virusi  vya ukimwi  kanda ya Pemba Dokta Rahila Salim Omar anasema kwa vile wanaume ndio viongozi wa familia ni wajibu wao kujuwa elimu ya afya ya uzazi.

 

Anasema ni vyema baba kwenda klinik na kuelezwa na daktari  ama muhudumu wa afya ana kwa ana, kwani ni rahisi kuliko kuelekezwa na mke wake huchangia kukosa amani pia.

 

 Akigusia matatizo yanayoweza kujitokeza iwapo baba hatokuwa na elimu ya afya ya uzazi ni ndoa kuvunjika, kupata ufanisi mdogo wa utumishi wa uzazi wa mpango na kupata mimba zisizotarajiwa.

 

Dk. Rahila  anafafanua kwamba , kwa upande wa  uchunguzi  wa VVU ni  vyema mke na mume kuchunguuza pamoja kwa sababu inawezekana mmoja akawa ameambukizwa na  mwengine yuko salama na VVU.

 ‘’Tunao wana ndoa ambao ni ‘’discordant couples’’ yaani  mmoja ameambukizwa na mwengine hana  VVU ‘’ na  kupima pamoja ni vyema kwani  kunazuia maambukizo kwa mtoto  au  wenza wao,’’anasema.

 

 NI IPI FAIDA YA BABA KUMSINDIKIZIKA MKE KLINIK

 Mwenyekiti wa jumuiya ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi VVU ZAPHA+ wilaya ya  Chakechake Maryam Said Abdalla, anasema moja ya faida ya baba kumsindikiza mke wake klinik ni kujua afya zao, ili kumlinda mtoto mtarajiwa. 

 Dokta Rahila anasema, husaidia baba kuongeza uelewa wa majukumu yake, ikiwemo lishe bora kwa mama ili mtoto tumboni akue vizuri, pamoja na kumfanya mama kuwa na furaha kwa ujauzito alionao.  

Msimamizi wa vituo vya huduma rafiki kwa vijana Pemba Fatma Hassan Khamis, anasema akina baba wasione tabu kwenda klinik, kwani kuna vipimo ambavyo hupimwa akina mama pekee,navyengine hupimwa pamoja ikiwemo cha virusi vya ukimwi .

 DINI INASEMAJE 

Sheikh Said  Abdalla Nassor kutoka ofisi ya Mufti Pemba anasema, kwa dini ya kiislamu haijakataza mume kumsindikiza mke wake klinik ama katika kituo cha afya. 

Anasema Mtume Muhammad (S.A.W) amesisitiza kwa wanaume kuwaanagalia kwa huruma wanawake na kuwasimamia, hivyo katika hali ya ujauzito amabayo anakuwa na mabadiliko ya kimwili, mume anahitajika kuwa nae karibu.

 “Mwenyezi Mungu anasema kaeni na wanawake kwa wema hivyo kuwasindikiza klinik ni miongoni mwa wema huo, kwani wanapata kupima afya zao kwa pamoja wao na mtoto pia. 



 Mchungaji wa kanisa la TAG Makangale na mwangalizi  upande wa Pemba, Samwel Elias Maganga, anasema dini haijakataza mume kumsindikiza mke wake katika kituo cha afya .

 

 Anasema katika bibilia kitabu cha mwanzo mlango wa pili  mstari wa 18 mpaka 24, inasema Mwenyezi Mungu alimuumba mwanamme na mwanamke, ili waishi pamoja kwa mashirikiano ya mambo yote ikiwemo ya afya.

 

MIKAKATI YA SERIKALI IKOJE 

Mkuu wa vituo vinavyotoa  huduma na tiba kwa watu wanaoishi na virusi  vya UKIMWI   kanda ya Pemba Dokta Rahila Salim Omar, anasema miongoni mwa mikakati ya serikali ni kutoa elimu, kuhusu wanaume kwenda pamoja na wake zao klinik.

 

Anasema elimu hiyo ambayo inatolewa kupitia vituo vya afya , hospitalini na hata wahudumu wa afya ngazi ya jamii, amabao hupita majumbani. 

Serikali imeanzisha  mkakati wa makusudi  wa ushiriki wa wanaume kwenye masuala ya afya  yaani ‘male involvement’ ili kusaidia akinamama na watoto, kwenye masuala ya afya na uangalizi wa familia ya afya ya mama.  

 Akiainisha vipaombele 10 wakati akisoma bajeti ya mwaka 2024/2025 waziri wa Wizara ya Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui, ni pamoja na kupunguza vifo vya mama wajawazito kutoka 145 kwa kila vizazi hai 100,000. 

Kupunguza vifo vya watoto wachanga kutoka 28 kwa kila vizazi hai 1000.

 Kwa mujibu wa malengo endelevu ya Umoja wa Mataifa lengo ni kufikia vifo 12 kwa kila vizazi hai 1000 ifikapo mwaka 2030.  

Sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022, imebainisha kuwa, wanawake wenye umri wa kuzaa kati ya miaka 15-49 kwa Tanzania ni 14,992,288, ambapo kwa Tanzania bara ni 14,501431, wakati kwa  Zanzibar ni 490,859.  

 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...