Skip to main content

CFP YAONGOZA MCHAKATO WA KUANZISHA COFMA PEMBA KWA AJILI YA KULINDA MISITU YA MIKOKO

 


Na Khelef Nassor

Community Forests Pemba - CFP kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Idara ya Misitu, Idara ya Mazingira, Kamisheni ya Ardhi, viongozi wa shehia na wananchi wameanza rasmi mchakato wa kuanzisha Mikataba ya Usimamizi Shirikishi wa Misitu ya Jamii – CoFMA kisiwani Pemba. Hatua hii inalenga kuweka mfumo wa ushirikishwaji wa jamii katika usimamizi endelevu wa misitu ya mikoko.

Lengo kuu la CoFMA ni kuhakikisha misitu ya mikoko inalindwa dhidi ya uharibifu na ukataji ovyo unaosababisha kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabianchi. Mikoko ni ngao muhimu kwa fukwe na jamii kwani huzuia mmomonyoko wa ardhi na pia hufyonza hewa ya ukaa.

Mchakato huo umeanza kwa zoezi la kupima maeneo ya uhifadhi, ambalo linahusisha kubaini mipaka ya shehia na kutambua maeneo maalum ya uhifadhi na yale yatakayotengwa kwa matumizi endelevu ya jamii.

Wataalamu kutoka Kamisheni ya Ardhi wamepewa jukumu la kuongoza zoezi hilo la upimaji, kwa kushirikiana na viongozi wa shehia na wananchi wa maeneo husika ili kuhakikisha kila hatua inafanyika kwa uwazi na ushirikiano wa pande zote.

Baada ya zoezi la upimaji kukamilika, hatua inayofuata itakuwa ni utengenezaji wa ramani za maeneo hayo. Ramani hizo zitakuwa dira ya wazi kwa jamii na wadau wote katika kutambua kwa usahihi maeneo ya uhifadhi na maeneo ya matumizi endelevu.

Kupitia ramani hizo, jamii itakuwa na mwongozo wa pamoja unaotambua mipaka, hivyo kupunguza migogoro ya matumizi ya ardhi na kuongeza uwajibikaji wa pamoja katika kulinda misitu ya mikoko.

Mchakato wa kuanzisha CoFMA ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa ZanzADAPT, unaotekelezwa na CFP kwa kushirikiana na Community Forests International - CFI, na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania – TAMWA upande wa Zanzibar, chini ya ufadhili wa Serikali ya Canada kupitia Global Affairs Canada.

Akizungumzia hatua hiyo, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa mradi wa ZanzADAPT kutoka CFP, Omar Mtarika Msellem, alisema kuwa baada ya maeneo kutambuliwa rasmi, jamii zenyewe zitaunda sheria ndogo ndogo za uhifadhi zitakazotumika kusimamia matumizi na kulinda mikoko.

 "Hili si jambo la CFP peke yake, bali ni mchakato unaomilikiwa na jamii wenyewe. Wao ndiyo watakuwa wamiliki wa mikataba hii, na wao ndiyo watakaoamua sheria ndogo ndogo za uhifadhi zitakazowaongoza," alisema Msellem.

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa mradi wa ZanzADAPT kutoka CFP Omar Mtarika Msellem akiongoza timu ya wataalamu wa upimaji na wanajamii katika zoezi la upimaji na utambuzi wa maeneo ya uhifadhi

Zoezi hili linafanyika katika shehia nne za mradi ambazo ni Kambini, Mchangamdogo, Chwale na Kiuyu, ambazo zina utajiri mkubwa wa mikoko lakini pia zinakabiliwa na changamoto za uharibifu kutokana na shughuli za kibinadamu.

Asha Yussuf Nour, Afisa Mikoko kutoka CFP, alisema kuwa mchakato huo umepokelewa vizuri sana na wananchi. Tangu kuanza kwake, serikali za mitaa na viongozi wa shehia wamekuwa mstari wa mbele kutoa msaada wa kila aina.

"Tumefarijika kuona jinsi wananchi wanavyoshiriki. Wamekuwa wakihudhuria vikao, kutoa maoni, na hata kushirikiana na wataalamu wa upimaji kuhakikisha kila eneo linatambulika vizuri," alisema Asha.

Kwa upande wake, Awesi Sharif Kombo, Afisa Upimaji Ardhi kutoka Kamisheni ya Ardhi, alisema kuwa zoezi hili ni msingi muhimu wa uhifadhi endelevu. "Huwezi kufanya shughuli ya uhifadhi bila kutambua mipaka ya maeneo. Hii ndiyo hatua ya kwanza ya kuweka msingi wa ulinzi wa rasilimali zetu," alifafanua.

Wanajamii wenyewe pia wameonyesha furaha yao kwa kushirikishwa moja kwa moja katika mchakato huo. Walisema hatua hiyo imeongeza uelewa juu ya thamani ya mikoko na nafasi yao katika kuhakikisha misitu hiyo inalindwa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Sharif Juma Omar, Mwenyekiti wa kamati ya doria ya Kiuyu Minungwini, alisema kuwa ushirikishwaji wa jamii ni hatua kubwa. "Hapo zamani tulikuwa tunaona mikoko ni miti tu ya kukata mbao. Lakini sasa tunafahamu thamani yake katika kulinda mazingira yetu na maisha yetu," alisema.

Aidha, alisisitiza kuwa mikoko si tu kinga ya mazingira bali pia fursa ya kiuchumi. Wanawake wanaoshiriki katika vikundi vya ufugaji wa samaki na biashara ya uvunaji wa asali walieleza matumaini yao kuwa uhifadhi wa mikoko utawasaidia kupata kipato endelevu.

Zoezi la CoFMA pia limechukuliwa kama jukwaa la kujenga mshikamano wa kijamii. Watu kutoka makundi mbalimbali wanashirikiana kwa karibu zaidi, jambo linaloongeza mshikamano na mshirikiano katika jamii.

Viongozi wa shehia walipongeza CFP na washirika wake kwa kuhakikisha serikali, jamii na taasisi binafsi zote zinashirikishwa. Walisisitiza kuwa kwa mara ya kwanza wananchi wanaona matokeo ya kushirikishwa katika maamuzi yanayohusu rasilimali zao.

Mradi wa ZanzADAPT unaendelea kuonesha kuwa suluhu za kimazingira zinaweza kufanikishwa kupitia mshirikiano kati ya serikali, jamii na wadau wa maendeleo. Ushirikiano huu wa kuanzisha CoFMA unatarajiwa kuwa mfano wa kuigwa na maeneo mengine ya Zanzibar.

Kupitia mchakato huu, Pemba inatarajiwa kuweka historia chanya ya usimamizi wa misitu ya mikoko. Hatua hii inatoa matumaini kwamba vizazi vijavyo vitarithi rasilimali zilizo salama, mazingira yaliyo imara, na jamii zilizo na mshikamano katika kulinda na kuendeleza utajiri wa asili wa visiwa vya Zanzibar.

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...